baadhi ya wanafunzi wa institute of finance management (ifm) wakibukua kwenye maktaba ya chuo hicho ambacho kiko mbioni kufanywa chuo kikuu cha univesti kamili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. Jamani leo nimegundua uandishi ni kazi na editing michuzi sijui nani anakufanyia Institute of Finance Management (IFM) Sio ifm na what is chuo kikuu cha University kamili??? I am confused!!!!!!

    ReplyDelete
  2. Kama ulivyochanganyikiwa wewe ndo nilivyo mimi. Ninavyoelewa mimi IFM siku zote imekuwa chuo kamili sasa nikiona kichwa cha habari kinasema kuwa chuo kamili naanza kutia wasiwasi kwamba huenda kuna watu walisoma na kuhitimu chuo kisicho kamili miaka ya nyuma. Kwa kuhisi tu labda ilikusudiwa "kuwa chuo kikuu". Neno kamili halipo pake kwa vyovyote kwa sababu hata kusema "chuo kikuu kamili" huwezi kwa sababu hakijawahi kuwa "nusu..."

    ReplyDelete
  3. Hivi tu kumbe kilikuwa bado hakijawa chuo kikuu cha university?? Mi nilidhani kilishakuwa zamaaaniii

    ReplyDelete
  4. Anony wa hapo juu, Michuzi sio kwamba amekosea ... huwa anafanya makusudi tu

    ReplyDelete
  5. USHAURI WA BURE: WATANZANIA KAMA MNATAKA KUIUZA NIC(NATIONAL INSURANCE CORPORATION), BASI UZENI "BUSINESS" SIO PROPERTIES. JENGO LA "KITEGA UCHUMI" WAPENI IFM WALITUMIE KWA MADARASA ZAIDI, OFISI ZA WAALIMU NA VYUMBA VYA KULALA KWA WANAFUNZI. MLIO KATIKA MAAMUZI, HUU NDIO WAKATI WA KUWARITHISHA WATOTO WENU WA KITANZANIA, SIO KUUZA KILA KITU KWA WAGENI HATA KILE MNACHOKIHITAJI WENYEWE.

    ReplyDelete
  6. Hongera serikali lakini hao wanafunzi wa hicho chuo kuna kamchezo fulani wanakapenda sanaa hasa watoto wa kike,sijui kama wataweza digrii.

    ReplyDelete
  7. hi
    mimi nilisoma chuo hicho nikamaliza 2004 then nikarudi kwa ajili ya postgraduate nikamaliza 2006 miaka yote hiyo nazisikia tu hizo habari lakini hakuna lolote lililofanyika, imani yangu naona hizo ni politics za kibongo istoshe mr michuzi hujatupa source ya hiyo info
    By
    Ismail

    ReplyDelete
  8. IFM ipewe hadhi ya chuo kikuu lakini wasibadilishe jina la chuo kwa sababu za kihistoria.


    MIT--Massachussets Inst of Technology, Loughborough Polytechnic Institute, Renselaer Polytechnic Institute, vyote ni vyuo vikuu kamili, lakini wameendelea kutumia majina yao ya kihistoria.

    ReplyDelete
  9. Kozi zinazotolewa IFM ni tofauti na mlimani, Dodoma au mzumbe? kama zinafana ila tofauti ni levo, mimi nauna ifm ibaki kama ilivyo ili itoe watu wa kada ya kati. Naaona siku hizi imekuwa fasheni kila chuo kubadilishwa na kuwa chuo kikuu na wakati huo huo hakuna ujenzi wa vyuo vya kada ya kazi na hivyo vikuu navyo havina miundombinu bora ya kufundishia. kama watu wanahitaji digrii basi waende vyuo vingine ili hapo waje watu wenaohitaji kwani siyo wote watakuwa na qualification sawa. Mimi nadhani hapa ni jitihada za walimu katika kujali manufaa yao zaidi na vinginevyo

    ReplyDelete
  10. We Anony wa 5.55.

    Naomba wakiite MKAPA UNIVERSITY. Kwani naomba tujidai na majina yetu. Huko Ulaya na Massachchussets umesema kuna majina kama MZUMBE? NA SOKOINE????
    Acha kuwa na mawazo ya kutawaliwa ndio maana Zimbabwe wameshindwa hata kulima kujilisha wenyewe wanataka Wazungu warudi wawalimie.
    Mdau

    ReplyDelete
  11. Anonymous wa April 11, 3:09pm amesema ukweli. Kamchezo kenyewe kamefanya wakufunzi wake waiite IFM kuwa ni INSTITUTE of FEMALE Management. Sijui kama ni kweli!!some females are going there to be managed by the......mhh wasije wakanishtaki bure lakini kamera ya mitaani imeinyaka hiyo.

    ReplyDelete
  12. sasa library kila mtu anajifungia kwenye ki cube chake discussion itafanyika vipi? au ndo kujifungia na kukariri

    ReplyDelete
  13. wewe Anon. wa April.11,2008 11:31 Pm.

    Nahisi wewe sio mzima. na kama ni mzima basi wewe hukufika hata secondary.

    Tangia lini na Librari ipi wana ruhusu discussion? sijawahi ona maisha yangu yote ya shule.

    tena Library ninavyoelewa mm ni pahala pa kujisomea mtu binafsi kimya na hata kuongea huruhisiwi, hata simu haziruhusiwi kuongea nazo.

    Ama kweli kazi ipo? kumbe humu ndani tuko watu wa aina nyingi.

    muwe mnauliza kabla ya ku coment plz

    ReplyDelete
  14. Hallow!!
    Naona Mchizi hapo juu hajui Discussion maana yake nini na inafanyika wapi? Kama kuna watu wanafanya discussion Libray then wanakosea,na kama ulizoea hivyo nawe pia upo mulemule!!
    Ni habari nzuri kama IFM(Institute of Finance Management) kinakaribia kuwa chuo kikuu,ila kwa upeo wangu mfupi na uzoefu pia hizo zote ni STORY wandugu.Nimesoma IFM 2004-2007 HIZO NYOMBO TUMEIMBIWA MUDA WOTE HUO.SIDHANI KAMA SAS ITAKUWA KWELI,BASI TUOMBE

    ReplyDelete
  15. Anony wa 11:31 umeenda shule kweli? Nani kakuambia Library ni sehemu ya discussion? Humo ni kama ulivyomalizia maneno yako matatu ya mwisho.

    ReplyDelete
  16. Jamani hata Library inaleta tabu, Maktaba unaweza fanyia discussion pia huo ndo Ukweli, mfano Stockholm University kuna vyumba maalum vya discussion jamani ndani ya maktaba. Lakini pia kuna Maktaba zingine hakuna hata viti kuna mashelf tu ya vitabu kwa hiyo unaazima kitabu unatoka. kwa hiyo tufanye uchunguzi kwanza si kulopoka tu.

    Mwaushe Ohiwas.

    ReplyDelete
  17. nyie ma-anon hapo juu mi ndo anon wa April 11, 2008 11:30 PM
    nimeshangaa sana kusoma comments zenu!? kuna mwingine anasema sikufika hata secondary?
    aisee Tanzania kumbe bado sana? "YES LIBRARY IS A PLACE FOR DISCUSSION AND RESEARCH" and those cubes are supposed to have computers hooked on them for research and there should be round table's somewhere around in there for discussions
    that kukariri era is past gone am so suprised you guyz still on it and humbly honor that?? WOW!
    In today's world nobody works alone people get together at work and discuss complex issues providing feedback to one another, nyie ndo mkimaliza chuo mnapewa ofisi mnaletewa mikataba mnashindwa hata kuisoma mnasaini tu instead of calling a meeting to discuss(something you have never exposed to while in school)
    You guys are still holding to the obsolete definition of library?? believe me there is a new definition fellas it just aint got to you yet! Standby it will get to you after few decades or so, lol
    You really made me feel so proud for my decision to study in the USA!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...