habari zako kaka Michu.
mimi mpenzi wa blog yako. naomba msaada kwenye hili tuta. kama ilivyo kwa watanzania wengi wa vijijini tulikimbia umande au tulikwenda kutega ndege.
kwa hiyo kimombo shida.
swali je kumkaribisha mtu kula kwa kimombo nisemeje?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 24 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 04, 2008

    WE UNATAKA UJUE ILI IWEJE NA USHASEMA UPO BUSH SA HUYO WA KUMKARIBISHA MSOSI KITASHA UTAMPATA WAPI? WE TIA JEMBE MPINI KAKAMATE EKA ULIME, KIZUNGU WAACHIE WENYEWE NA USITAKE KUWACHANGANYA WATU KWA SHIDA ZAKO ZA KUKIMBIA KWAKO UMANDE

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 04, 2008

    Jaribu
    Please tafadhal have some maakul

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 04, 2008

    Swali lako hata kwa kiswahili lina utata....umeshapata msulivan huko nini unataka kumkaribisha nyumbani?

    Back to your question Unamkaribisha kula je umeshapika hicho chakula? au unamkaribisha nyumbani kwako ili umwandalie chakula? Au unamkaribisha chakula mkutane hoteli fulani kwa chakula cha mchana au cha usiku..

    Na pia huku tuliko kama wewe ni mama wa nyumbani humkaribishi mtu chakula ni unatangazia umma kuwa chakula kipo tayari. Kwa hiyo mwenye njaa aje mezani

    Kwa hiyo kwa swali lako itakua kama ifuatavyo

    1. dinner is ready -

    2. Lets do lunch/dinner sometimes

    3. would like to eat something?

    4. how about dinner would you mind to stay/stop by my house for dinner tonight

    5. welcome to the table the meal/dinner is ready

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 04, 2008

    lugha ni utamaduni. wazungu hawana utamaduni wa kumkaribisha mtu chakula wakati wanakula. Kwa hiyo hawana neno kabisa la kumkaribisha mtu kula. Huwezi kuwa na neno kwenye lugha yako ambalo huhitaji kulitumia. Siyo kila neno ambalo liko kwenye lugha moja litakuwa kwenye lugha nyingine. mathalani, wafaransa usema "BON APPETIT" kwa mtu anayekula. maana yale "NAKUTAKIA HAMU NZURI YA KULA". kwa sababu sisi waswahili si utamatuni wetu huo, kumwambia mtu kwamba "NAKUTAKIA HAMU NZURI YA CHAKULA" wakati anaanza kula atakushangaa sana. Kwa hiyo usifikiri kila neno lililo kwenye kiswahili au hata (lugha ya kabila lako) liko kwenye lugha nyingine pia! la hasha! Linganisha hata Kiswahili na kilugha chako huko bush.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 04, 2008

    Hii umeitunga wee mwenyewe MICHUZI. Ulishindwa kuwakaribisha Wazungu hapo Silluvan Arusha. Janja ya nyani hiyo...kwisa gundua. Na sisi hatukusaidii, utakoma mwenyewe. Hahahaha.............!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 05, 2008

    well come for food

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 05, 2008

    Yu wanna geri sam tu iri?
    Mdau ,Mtoni kijichi.

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 05, 2008

    YOU ARE WELCOMED FOR CANDLE LIGHT DINNER AT MY HOUSE. MAY BE WE CAN SIP ROEDERER CRISTAL CHAMPAGNE AND GET TO KNOW EACH OTHER..HOLLA BACK

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 05, 2008

    kuna watu waongo humu, eti wazungu hawana utamaduni wa kukaribisha watu kula, huyo mzungu uliyewahi kukaa ni mnyimi, swa tu na waswahili kibao wanyimi, lakini tusidanganyane wazungu hawana utaratibu wa kukaribishana chakula, achen stori za vijiweni na za utoto.

    nimekaribishwa mara nyingi chakula cha usiku , mchana, n.k,

    ''Would you like to eat something''??
    ''Kindly can you have a dinner with me''

    L kusema ni kuwa watu wako bize na mambo yao, na wakukaribishapo wengi huwa ni for special cases, na wakati mwingine wanatoa kadi kabisa , ya dinner/lunch invitation.

    sio watu wa kwenda nyumba za watu huna kazi upeleke umbeya au eti unasalimia halafu''karibu tule'' walivyo wengi utembeleana kwa kutaarifiana,labda hili linaweza tafsiriwa kuwa si watu wa kukaribishana.

    I remain truly to be corrected, sina msuli wala mshipa katika hili

    mdau
    canada

    ReplyDelete
  10. AnonymousJune 05, 2008

    Mdau wa Canada,

    Mzungu akikukaribiisha si kula nae sahani moja. Ni kukupeleka hotel au kutayarisha sherehe. Kukabirisha kunako zungumziwa hapa ni kwa kiswahili. Unakula mtu anakukuta unakula unasema "KARIBU tule". Narudia tena, si utamaduni wa wazungu huu. Nimekaa USA, Europe na New Zealand...kote huko nimeona hivyo!

    Mdau,

    France

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 05, 2008

    MAMA WEEEE ACHA HIYO! MZUNGU AKIJA KWAKO MPE GLASI YA MAJI NA WEWE ENDELEA NA SIMA YAKO BASI, WALA HATA SHANGAA NA KAMA ANA KAGAZETI ALIKUACHIA NDUGU YAKO ALIPOTOKA MJINI MWAKA JANA MPE ASOME.

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 05, 2008

    Mbona vingereza vingi tu hapo.

    rahisi sana.

    welcome to eat AU

    Welcome food AU

    U? Food u dont eat? hapo unamuuliza

    welcome to eat basi?

    Ni hivyo tu


    mdau Anna

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 05, 2008

    Aprochez a la table, svp.

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 05, 2008

    Mdau France, Mnaringa mlioko ugaibuni eti mi sha kaa USA, Europe, Newzeland mmmmmh!

    MTIZED

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 05, 2008

    would u mind if u wellcome food?
    sweet,
    Arusha.

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 05, 2008

    What a bunch a crap, candle -light dinner? U food u dont eat?
    Was this a business or social dinner invitation?

    ndugu, sema tu: How would you like to join me for dinner this evening at Mambo Restaurant or at my place?

    Hakuna aibu kumsaidia ndugu apanue njia au aina za mawasaliano.

    Sam - Atlanta -US

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 05, 2008

    huyo aliesema CANDLE LIT DINNER WITH SUM CRISTAL ni dinner ya kimapenzi au? afu mbona kuna broken english humu sana? eti 'a dinner' sema tu dinner. anyways mi naona umwambie 'your welcome to have a meal with me' au 'would you like to have a meal?' or 'would you like to eat' au 'do u fancy grabbing a bite?'

    miss keys

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 05, 2008

    i got french fries for dinner/lunch u want some?

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 05, 2008

    ahsanteni sana wadau. nimenyaka ngeli kibao. ahsante hata wewe mdau wa kifaransa. namna hiyo najiendeleza.

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 05, 2008

    lisikusumbue hilo kwani wenye asili ya hiyo lugha huwa hawakaribishani chakula,haya mambo ya kukaribishana chakula yapo kwa walala hoi tu, na kwa kuwa umesema kuwa ulikimbia umande kuna uwezekano mkubwa sana kuwa unalala hoi, na ninaamini kuwa unajua jinsi ya kukaribisha mtu chakula kwa kiswahili inakutosha hiyo unless otherwise unaongopa

    Mbega hapa

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 05, 2008

    Man this is funy,i like it when people commenting on stuffs like this,i know not everybody is serious commenting on the topic,they just trying be funy and yes it is funy,makes ma day going better whn reading these funy comments but i strongly disslike the hate and negativity of some people A.K.A Waosha Vinywa. Stay positive ma people.
    Mdau USA.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 05, 2008

    du jamaa kakubali kuwa kapanua lugha lakini sidhanikama amepata kitu hapo....manake kila kitu kimewekwa sasa sijui atachagua lipi na aache lipi

    pole bwana mkubwa...ila hakikisha wanao hawakimbii umande na kwenda kutega ndege tena

    Nyaningedere

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 05, 2008

    Wewe unaejiita madau wa USA watu wanachangia hoja kwa lugha ya kiswahili sasa sijui unavyo andika hicho kizungu unataka watu wajue kweli uko USA au?.Sio kila mtu anajua kizungu na wala sio wote walioko USA wanajua kizungu. Hapa bila shaka inaonyesha ni jinsi gani hauko USA kwani mara nyingi ukiona mtu anajidai ujue hamna kitu.Kwahiyo uache hiyo tabia yako ya kibwenga(kihaya) kwani sio wote wametokea kashozi

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 06, 2008

    hahaha,wadau naona tumemsakama sana huyu mdau mwenzetu,yeye anataka kujua kumkaribisha chakula tu,sasa sijui baada ya chakula hakutakua na mazungumzo mengine na huyo Msulivan!na jinsi ya kuomba Mkuki je hutaki kujua(HELA)?au kukupatia mchongo wa viza?
    Any way,mi nafkiri we ungeendelea na utamaduni wako wa kumkaribisha chakula,rather than being a slave of western calture.its simple u can just say EXCUSE ME'LETS JOIN TOGATHER FOR DINNER/LUNCH OR WHATEVER U KNOW ....INATEGEMEA NA MAZINGIRA YENYEWE.
    Na huyo msulivan we ukamuacha na utamaduni wake kama wanakaribisha au hawakaribishi.just take r easy man.
    Ila kma mtatoka wote kuspend halafu ukategemea msulivan atachanja utakuja umbuka ndugu
    Have bucks in ya wallet
    Don ger out with empty hand niggar'
    Mdau Baajun.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...