Zikiwa zimebaki takriban siku sita kabla ya ule mtanange wa timu mahili ya Mashariki (East Mass) kumenyana na timu kongwe ya Magharibi (West Mass) katika kusherehekea miaka saba toka tuanze shughuli hizi, masikio na macho ya wengi yamewaelekea wenyeji wa hafla hii kubwa ya mwaka katika majimbo yetu ya New England ambapo watanzania huja kukutana kuzungumza, kubadilishana mawazo na kufurahi sisi wenyewe,familia zetu, jamaa na marafiki.


Tunapenda kukumbusha tena wewe ndugu yetu kwamba, shughuli hii ya kukata na shoka itafanyika Greenfield,Massachusetts Jumapili tarehe 20 Julai, 2008 kuanzia saa tatu asubuhi (9am) mpaka saa tatu usiku(9pm). Habari zilizonifikia punde kutoka kwenye kamati maalum ya ufundi ya shughuli hii, inasema maandalizi yamekamilika na yule ngo'mbe jike kweli yupo!


Katika kuyaweka mambo sawa chanzo changu cha habari kimeitanabaishia Globu hii ya jamii kwamba yule mtaalam wa kuchoma nyama katika ukanda huu wa East Coast anawasili mapema mwishoni mwa wiki na "yuko fit" kwa kazi hiyo!


kama umewahi kula mishikaki au nyama choma ya mnadani Dodoma basi ladha ile na ya huyu jamaa haipishani hata kidogo!


Kulingana na mratibu wa shughuli hii ametonya kwamba ni bora watu wafike mapema hasa wale wenye kutaka supu ya utumbo kwa vitumbua, baada ya hapo kutakuwa na michezo ya soka kwa watoto na watu wazima, mpira wa vikapu kwa watoto na watu wazima, netball kwa kina mama na ndipo tutapumzika na kupata chakula kizuri cha mchana.


Baada ya hapo ndipo burudani ya mitindo ya mavazi ya kitanzania kwa watoto, kina mama na kina baba yatafuata. Shughuli ya ubunifu wa vipaji tofauti kama kuimba,kufoka n.k. vitakuwepo.


Bila kusahau dansi maalum ya kiafrika ambayo mwaka jana ilikonga nyoyo za watanzania wengi kuona vijana wetu wenye umri wa miaka 15 mpaka 18 pia wanaweza kucheza "pinda mgongo".


Ni muhimu uwahi mapema wewe na familia yako na jamaa zako ili uje tufurahi pamoja.


Haya ni maisha, hapa tulipo ndipo kwetu...nyumbani mbali na nyumbani, na kama ujuavyo maisha yenyewe mafupi haya njoo tufurahi.Kama kawa "Sugu"


Mr. II atakuwepo na kutupa burudani la nguvu na kijana wetu Hasheem atakuwepo kuwapa vijana muelekeo wa kucheza mpira wa kikapu.Na kama ilivyo ada namalizia kwa kusema mwakwetu shughuli ni watu na hao watu ni mimi na wewe.


HABARI NDOO HIYO!


Naomba kuwakilisha,

Isaac A. Kibodya

Kwa niaba ya wanakamati


Ukihitaji mawasiliano zaidi basi usisite kupiga simu za wanakamati ambayo baadhi yao nimeziandika hapa chini.


Shukran!

Bwana Stephen Tomi 413.658.5253

Bi. Maria Sombe 413.364.8151

Bwana Richard Mwandemani 413.262.0400

Bwana Baraka Baraka 413.364.8151

Bwana Ahmad Mkambavange 413.221.2935

Bwana Mohamed Kibodya 413.796.9761

Bwana Severine Kiputa 413.306.2109

Bwana Kawala Mgawe 413.330.1609

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 14, 2008

    Kwanini hamfanyagi jumamosi hii party? wengi tungependa kuja huko lakini mtu ukisafiri ufike huko jumapili na sijui tutaweza kurudi na kwenda makazini monday...Au wenzetu hamfikiriii hilo au hamtaki wageni?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...