Zikiwa zimebaki siku nne tu kabla ya oldskool bash la karne kutimbuka nyongo, na watu kumwagika toka kila pembe ya dunia kweli vijana wa wazamani hawajasahau kuruka nyoka.

globu hii ya jamii ikizungumza na mmoja wa waandaaji wa hili libeneke la oldskuli ya karne,amesema hii bash sio ya kukosa wala kuhadithiwa,ni mambo makubwa ambayo hayajawahi kutokea, fika utikise kichwa,urushe japo mikono na kujiachia achia ili mradi si fujo wala patashika bali ni burudani la oldskuli litakalo kuacha hoi. ukichoka sana kutakua na starehe ya macho mbele yako kama show za break dance,chacha,robot n.k.


Amesema kwamba madebe yataanzia ijumaa kuanzia saa 4 usiku mpaka majogoo adresi ni 1213 E Dublin Graville,Columbus,Oh 43229.


Vijana wote wazamani walio Bongo,Ulaya,Canada na hapa Marekani wamekubali mwaliko akiwemo mbunge wa nanihii mheshimiwa nanihii.


amesema hii bash itakua ya kwanza katika historia ya bash za wabongo ya uwakutanisha Watanzania wanao toka mabara tofauti.


ratiba yaonesha kwamba jumamosi mambo yataanzia uwanjani kwa nyama choma huku tukiangalia mpira wa miguu kati ya Simba na Yanga. ikumbukwe mara ya mwisho timu hizi zilipokutana Washington Dc,Simba ililala 5-2. Hivyo hii itakua nafasi nzuri kwa Simba kulipiza kisasi.kama uwezo upo wa kusakata kabumbu njoo na vifaa.


Usiku wa hiyo jumamosi kuanzia saa 3 mambo ni kwenye RED KAPETI ni kuruka kopo mpaka asubuhi jua chomoza,adresi ni The Gathering,847 E..11th Av,Columbus,Oh 43211.


mdau unakumbushwa USISAHAU MSWAKI ila dawa za meno zitatolewa bureee,masaladi na amerikani chips watakuwepo ndani ya ukumbi kwa supu na chapati za nguvu.


mwisho waandaaji hao wamesema Dj Boni Luv atafanya onyesho moja tu, hilo la oldskuli july 5 Columbus ohio,hataweza kufanya onyesho lingine kwani july 12 Dj Boni Luv atakua Denmak.


Unaambiwa usikose hii nafasi ya kukutana, kuona na kucheza muziki wa dj huyu mahili na maarufu Tanzania.


ONESHO NI MOJA TU KWA DJ BONI LUV OLDSKOOL BASH COLUMBUS OHIO JULY 5

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 02, 2008

    TUMAINI(INDEPENDENT SCHOLAR) NITAKUPITIA ALHAMIS USIKU TUKAJIKUMBUSHE ENZI ZETU.
    JF WOTE VILE VIKAO VYETU KAMA KAWA.
    MWANAKIJIJI ......VENUE ZOTE NI WHEELCHAIR FRIENDLY.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 02, 2008

    hili bash,je litakuwa live bongo radio? na if yes,tunaomba starting time in GMT

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 03, 2008

    mimi niko mbali na marekani lakini nimeona mmeandika hii bash itakuwa live kwenye bongo radio. nataka sana kusikiliza show yote sasa ni saa ngapi show itaanza.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...