Brother Michuzi,
samahani kwa kukusumbuwa kidogo, nilikutumia email kitambo lakini sikuiona katika blog yetu ya jamii, kwa hivyo natuma tena. Naomba uniwekee suali langu hili kwenye blog yako ili ndugu zangu waweze kunisaidia na kunipa mawazo.
Suala langu ni kuwa nataka kununua gari ya aina ya landrover, natafuta kampuni, wakala au mtu binafsi nyumbani anae jishuhuisha na uigizaji na uuzaji wa magari haya.
naona contact zao iwe email, website, number ya simu au mahali walipo ili niweze kuwasiliana nao.
Tafadhali brother michuzi, usitupe ujumbe huu ndani ya gunia.
Shukrani kwa wote
Mdau Zenj

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Muagizaji na Msambazaji wa Land Rover ni Cooper Motors Tanzania Limited au CMC wako karibu na Maktaba Kuu ya Taifa oposite na ilipokuwa ofisi za Michuzi zamani (Daily News na Print Park) Mtaa wa Maktaba kama sikosei.

    ReplyDelete
  2. Nenda kwa Leodgar Tenga.Ni mtu mwenye nafasi pale Landrover Tanzania Limited.Atakusaidia.

    ReplyDelete
  3. wewe mchawi ombi lako liliwekwa kwenye hii blog siku za nyuma na ukapewa ushauri uache kununua magari ya kizamani,kwani tunakumbuka ulikuwa unatafuta landrover ya kizamani.kwani kama ulikuwa unatafuta mpya sijui umetafuta wapi kwani hata mtoto anajua ziko wapi. wewe kwanza uko zenji sasa sijui landrover ya nini wakati kandambili zinakutosha.tuondolee wanga hapa

    ReplyDelete
  4. Wewe mzenji ina maana hata yellow pages uijui? ni vyema uendelee kutumia usafiri wa punda kama mnavyotumia huko mchamba wima na kaburi kikombe.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...