mhariri mtendaji wa magazeti ya serikali isaac mruma akiwa na mariam kinunda, mchumba wa athumani hamisi anayeishi arizona, marekani, wakiwa na mgonjwa muhimbili

Mpiganaji Athumani Hamisi ambaye alipata ajali ya gari huko Kibiti siku kadhaa zilizopita atapelekwa hospitali ya Apollo huko New Delhi, India, kwa matibabu zaidi ya mgongo na shingo ambavyo viliathirika na ajali hiyo.

Athumani alikuwa akienda Kibiti kikazi akiwa na waandishi wenzake wawili ndani ya gari lake mwenyewe.
Athumani ambaye ni mhariri wa dawati la picha katika magazeti ya Habarileo na HabariLeo Jumapili na majalida yake anaweza kuondoka wakati wowote kuanzia sasa baada ya kukamilika kwa taratibu zinaozohusu safari ya mgonjwa wa aina yake nchi za nje.
Hadi sasa kinachotafutwa ni usafiri wa ndege ya moja kwa moja hadi jijini New Delhi ili mgonjwa asiathirike zaidi endapo kama atasafiri kwa ndege za kuunganisha ambapo itabidi awe anahamishwahamishwa.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. aisee dada umenibariki sana,,,unafaa sana yan toka Arizona adi home tena fiance tu??yan ur one among millions
    Muumba atamponya tu athuman for yu

    ReplyDelete
  2. FROM DAR TO NEW DELHI MOJA KWA MOJA? LABDA CHARTER...MKUU MICHUZI HAYA MAMBO MBONA YANAJULIKANA KABISA KUWA HAKUNA NDEGE YA MOJA KWA MOJA, AU WANATAKA TU KUPOTEZA MUDA HAO MAOFISA WAKIJIFANYA WAKO BIZE KUTAFUTA NDEGE YA MOJA KWA MOJA?

    ReplyDelete
  3. Du !! dada wa MAREKANI, uguzaa tuuu then najua utaondoka tu utaniachia, hapa sina ujanja kwa HAMISI, Naomba tu apone then urudi ARIZONA.

    Tupo wengi.....lakini mshindi wa wa hili GAME atajulikana tuu...FIMBO YA MBALI HAIUWI NYOKA.


    Kaka MICHUZI ukipenda nibanie tuuu MWANGA WA JUA.

    ReplyDelete
  4. That's love men...mahaters ng'aeni tu nyuso. Big up for her. Naona na ndugu wa yule mwenzake aliyefunjika mkono na mguu amtoka pia marekani kumuuguza kaka yake.

    ReplyDelete
  5. MICHUZI KAKA YANGU MBONA UNATUCHEZEA AKILI. SIKU YA AJALI ULISMA ANAKWENDA KUFUTURU. LEO UMEBADILI HABARI KUWA LIKUA ANAKWENDA KIKAZI. AUGHHH.....JAMANI KWA VILE WAYU WAMEULIA NIAJE YEYE APELEKWE INDIA NA SERIKALI NDIO MAANA UNABADIDILI HADITHI?

    NI MCHANGO WANGU TU ...UKITUPIA KAPUNI AU UWEKE LAKINI UJUE STILL WATU WANAMUOMBEA APONE HUKO KAKA LAKINI NI PALE WATU WANAPOONA KUNAKUWA NA TOFAUTI YA USAWA KATIKA HUDUMA MUHIMU

    KUMBUKENI BINADAMU WOTE NI SAWA

    ReplyDelete
  6. Mbona watu wanaona big deal mtu kutoka marekani kwenda kumuuguza mtu home. Angetoka mtu mtwara wala msingeshangaa hivi na wala najua michuzi asingeweka sana hizo sehemu. Na wakati mtwa utakuta katumia week njiani na shida ya usafiri wetu tena mweeeee

    Jamani marekani is nothing but a name. I know kwa vile naishi huku so watuuu stop going crazy and thy love our country.

    Mdau NY City

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...