Timu kamambe ya Bongo United itaelekea mjini Atlanta,ijumaa oct 24 tayari kwa mpambano wa mechi ya kirafiki na wahasimu wao Atlanta Tanzanite Fc,itakayochezwa jumamosi oct 25,mara ya mwisho timu hizo zilipopambana Bongo United waliibamiza Tanzanite 3-2.
katika mechi mbili ilizocheza za kujipima nguvu,ilizocheza oct 12 na Senegal,Bongo United iliibuka na ushindi wa 3-1.
magoli yaliofungwa na Seif,Shaban na Denis,wakati lile Senegal lilifungwa na mchezaji wao hatari wa timu hiyo Keita.na katika mechi nyingine waliocheza oct 19 Bongo United waliweza kuichakaza timu ya Malawi 4-0 timu ambayo ipo kwenye ligi,mabao ya Bongo United yalifungwa na Inno,Seif(2) na Owen.
Kikosi cha mauaji kitakachosafiri hiyo ijumaa chini ya kocha wao Rashid Lato,aliyewahi kuichezea ushirika Moshi,Small Simba na timu ya Taifa,makipa ni Dedy,Alawi,Lucas,mabbeki lemy,Evans,Beach boy,Adam ny,ray,Simon,Tobi,Marco,Mawenya,Vasco na Aris.Viungo ni Owen,Libe,Vicent,Hussein,Inno,Kheri,Dogo,Choteka na Yasin.mafoadi ni Dickson,Seif,Kendo,Denis,Shabani,Adam dc na Chichiba,wachzaji wote wako fiti tayari kufanya mauaji

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 2 mpaka sasa

  1. Majungu mbona hatumsikii hapa, au yeye majungu yake kwa fc bongo ya helsinki tu?

    ReplyDelete
  2. Kweli nimekubali Marekani mwisho, huwezi kufananisha na mansese ufini, wapika majungu wote wamesaluti.. tehe tehee ee

    KAZI IPO BONGO NI SMBA UA YANGA JUMAMOSI HII, Mdosi wa yanga ndio kasha sema yanga ikifungwa tu anakatisha mkataba na ufadhili basi...tehe tehee watu tumbo joto.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...