kiongozi wa jahazi modern taarab mzee yusuf akiwa na maimatha wa jesse
Manywele Entertainment kwa kushirikiana na JahaziMorden Taarab wana (Nakshi nakshi) imeandaa onyesho la Taarabu lililopewa jina la Raha 2008 linalotarajiwa kufanyika katika Hotel ya Traveltine Magomeni siku ya jumapili 19/10/2008.
Mratibu wa onesho hilo Maimartha wa Jesse amesema vikundi vingine vilivyoalikwa kwenye onyesho hilo ni East African Melody, Khadija Kopa na Hammer Q.
Pia onyesho hilo ni kwa ajili ya kusaidia kikundi cha vijana kinachoitwa Welawela cha Kinondoni, onyesho hilo litaanza saa tatu usiku na kiingilio kitakuwa shilingi 5000 tu wapenzi wote wa Taarab mwakaribishwa sana siku hiyo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Hao WaleWale wanafanya nini?

    ReplyDelete
  2. Asante kwa taarifa ya kuvuta raha

    ReplyDelete
  3. Duu huyo dada kama katoka usingizini vile...

    ReplyDelete
  4. Huyo dada hilo ni poda au kinyago cha kibisa/sarakasi?
    Duh!

    ReplyDelete
  5. Huyu dada amependeza jamani. Hii ni blog ya heshima.pse lets pay some respect.Sio sehemu ya kuponda watu.This is not the u...blog. Sorry haters. Msituingilie na huku. balozi usibanie hii

    ReplyDelete
  6. Huyu Dada amependeza sana ni mrembo wa kupigiwa mfano Bongo kwa wasichana wengine naimani ataweza wasaidi Dada wengine kufikia kiwango alichofikia yeye ni mfano wa kuigwa naimani atawapatia wasichana wa hapa nyumbani bongo jinsi ya kujishuhulia wenyewe na kufikia kigezo anachoonekana nacho Hongera Dada yetu kwamsada wako katika jamii yetu

    ReplyDelete
  7. Mhhh mimposi ehh nafikiri kuna haja ya kudefine kwa mapana the word 'kapendeza' na 'mzuri' kwa mimi, duuu hapana dada yetu umezidisha madiko usoni. i dnt mean vibaya please

    ReplyDelete
  8. Sikuzidisha kwani wewe binafsi humuoni hivyo alivyo au wewe binafsi hutofurahia kuona wasichana wengi hapa Bongo wapo kama yeye hivyo alivyo najuwa ni harama kujishuhulikia lakuni amefanya jitihada anagara usoni na ndiomana nikasema naimani wasichana wengi hapa bongo wawe kama dada huyo mgaro tu itasaidi katika hali tuliyonayo hapa Bongo kwani watu kama yeye sio wengi

    ReplyDelete
  9. Anon October 20, 2008 11:37 PM na October 21, 2008 11:17 PM ni muhusika mwenyewe, ukisoma kwa bidii utaona anavyojichanganya.
    Pia, tuige mfano upi?, wa biashara na intertainmenta au wa urembo?

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...