baada ya kuanza upya libeneke la kuvunja mbavu mitaa ya tbc one, kundi la orijino komedi kesho linaanza shoo za wazi kwa onesho moja matata sana kwa familia katika ukumbi wa diamond jubilee hall, wakishirikiana na bendi ya vibration sound na wasanii wengine kibao. kiingilio wametaja kuwa ni sh. 15,000 kwa vip, 10,000/- kawaaida na 5,000/0 kwa watoto. shoo inaanza saa tisa mchana

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. Mbona siku hizi Joseph Shamba au Vengu [Miss Ifakara] (kama alivyojulikana EA TV) haonekani ndani ya TBC1 au ndio kishapata majani marefu sehemu nyingine???

    ReplyDelete
  2. Wajasiliamali hawa kwa sasa wanatisha, big up seki na vijana wako, ila tunaomba kuwekwa wazi yuko wapi mzee wa kiraracha(vengu) mimi nawafagilia

    Keep it up wajasiliamali

    ReplyDelete
  3. Nami naungana na mdau hapo juu kuuliza yu wapi 'mrema' wa ze commedy?

    ReplyDelete
  4. Wanajitahidi lakini tangazo lao la Daktari bingwa wa Kutoa Mimba na Lile la Changudoa halina maana kabisa ikizingatiwa kipindi hiki kinapendwa sana na watoto. Pili hayo matangazo mawili sijaelewa yana promote hayo mambo ua yana lengo gani? Naomba uongozi wao uangalie sehemu hiyo.

    tatu ni rangi ipo dark sana hasa pale mwanzoni wanapotoa picha zao wapunguzi hizo rangi za giza.
    vinginevyo ni vijana wanaokuja juu! Hongereni

    ReplyDelete
  5. Michuzi kuna jamaa mmoja haonekani kwenye kundi ni yule anayemuigiza Mrema kulikoni

    ReplyDelete
  6. PENGINE NINA MTIZAMO FINYU, LAKINI HAWA JAMAA KUWA CHINI YA TBC-1 SIJUI KAMA WANAWEZA KUTOFAUTIANA NA GAZETI LA UHURU KWA JINSI WATAKAVYOKUWA WAKIWASILISHA MAWAZO NA UTAALAMU WAO KWA JAMII.



    SAMAHANI MICHUZI KWA HILI MAANA PENGINE LINAWEZA KUKUGUSA HATA NAWE KWA NAMNA MOJA AU NYINGINE, HATA HIVYO NAJUA KUWA HIYO HAIWEZI KUWA SABABU YA KUNIMINYIA.

    ReplyDelete
  7. Wazee wa Orijino Komedi production quality ya TBC1 ni ya kiwango cha chini kuliko kule mlikokuwa.

    Siku hizi picha zimefifia, mwanga hafifu, sauti iko chini na kamera haziwavuti sura zenu kwa karibu zaidi wakati mnasoma taarifa ya habari.

    Halafu ile screen mnayoweka nyuma inadistract. Mtazamaji badala ya kufokasi kwenu anajikuta anaanza kufokasi kwenye matukio ya kwenye ile TV.

    Hebu wawekeni sawa TBC1 wasije kuwaharabia kazi yenu.

    Ni hayo tu.

    //Mdau

    ReplyDelete
  8. Sio siri waadau tanauliza yuko wapi VENGUUUUUUUUUUU???
    NAUNGANA NA MDAU KUWA MATANGAZO YENU: LA DOKTA NA CHANGUDOA NI UPUUZI MTUPU, NAMSHANGAA TIDO MHANDO KURUHUSU UPUUZI HUO KWENDA HEWANI. MIMI NI BABA NA FAMILIA, WATOTO WANGU WANAPOANGALIA WANAJIFUNZA NINI??? HUU NI UFISADI MWINGINE, UNATUMIA MALI, VIFAA, NA MUDA (AIRTIME) WA UMMA KUHARIBU JAMIII. Mithupu naomba kuwakilisha hoja, tafadhali usinibanie. Mdau

    ReplyDelete
  9. Naomba hili suala la daktari bingwa na changudoa liondolewe haraka kwenye ze komedy au labda mtoe ilani ni kwa wakubwa tu
    Tido Mhando na Suzy Mungi mmesikia?

    ReplyDelete
  10. Kwa kweli napata wakati mgumu ninapoona matangazo hayo yanarushwa. has pale lile la dokata akitoa mimba. mtoto wangu wa kiume ameaza udadis watoto huwa wanapatikanaje?sasa anapokuwa na mamaake na wanangalia hiyo orijino komedi, mke wangu anapata wakati mgumu, zaidi ya ku-flip channel.Hivi TIDo vipindi vyake unaviangalia, au kukaa kwingi ulaya umesahau sisi ni watanzania??

    ReplyDelete
  11. KWA MSISITIZO KBS KM WADAU APA
    JAMANI MATANGAZO AYO MWAWILI LA CHANGU NA Dr YATOLEWE KABISAAAAAAAA YANI HAYANA MAANA KBS NAJUA MICHU UNAWAKILISHA AYA MAWAZO YA BLOGU YA JAMII AU tiddo na wengine wa TBC1 WANASOMA HII BLOGU,,,TOENI UO UNYAMAFU APO,,,ME SII MPENZI VILE WA ZA COMEDY BT JINSI WATU WANAOANGALIA NA KUSIMULIA,WALINIPA MSISITIZO SIKU NIJIONEE YALABII SIKUAMIN KBS ZILE TANGAZO.YANA MAANA GANI??NILIJIULIZA SAAANA,JE NI BIASHARA,UPOTOSHAJI WA JAMII KM TV YA"TAIFA", WHAT the @@###*** do yu pple put thz crazy stuffs??
    SINA HAMU KBS
    TOENI IZO MATANGAZO HARAKA

    ReplyDelete
  12. tunafurahi kurudi kwenu hewani ,ila tunaomba huyo vengu arudishwe ,mimi kama mimi nilikua namfagilia sana ina maana kumsimamisha huko hakuna mipaka?

    mimi ni mshabiki mkubwa tu wa vengu otherwise mashabiki wake tunakosa uhondo

    ReplyDelete
  13. Nawapa big up sana hawa orijino comed hasa Joti kwa jinsi anavyoweza kujibadilisha mara kwa marw yaani yupo juu sana kupita maelezo kaza buti baba nakukubali sanaa wangu: celina a.k.a mama B.

    ReplyDelete
  14. Me namfil sana Macklegan kapala aka shemeji, handsome boy, aah CHURAAAAAAAAAAAAAAA!!!!!!!!!!!!!!!!!!

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 14, 2011

    MASELA MPO JUU SANA NAWAPA BIG UP

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...