Kaka michuzi asante sana kwa kutupa nafasi ya kuweza kutoa taarifa za msiba wa dada yetu mpendwa Amina kipaya[kisigo].
lengo letu si baya ila ni ktk kucahanganyikiwa na msiba huu mzito ulotukuta hapa jp.kuhusu kwa watu walio nje ya japan tuliomba usd 100 ila ni makosa ya kiuandishi tu yaliyotokea mpaka tukakosea na kuandika usd 1000 hivyo basi tunachukua fursa hii kuwaomba msamaha ndugu zetu wote jambo hili lililowachanganya kiasi.
Ila tunashukuru wote waliotoa michango yao na wale waloshindwa kutokana na majukumu mbalimbali ila ila tunaamini wapo pamoja nasi ktk maombolezo haya michango inaendelea na tutawapa taarifa zaidi kwa kila njia hatua tutakayofikia asante.
Natanguliza shukrani
Ktb mwenezi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. Poleni na msiba ila kuwaomba watu viwango si vizuri. Ina maana kama nina $50 nisiwape? au nikiwapa hamtapokea? Wote tumefiwa na tumeshasafirisha mwili lakini hatujatoa viwango vya pesa. Haba na haba hujaza kibaba.

    ReplyDelete
  2. POLENI SANA WAFIWA.
    MISIBA inatokea huku nje tulipo, na huwa tunasaidiana wakati wote.Tatizo lililojitokeza hapa ni kule kutajiwa KIASI cha kutoa rambimbi kwa watu walio nje ya Japan,nadhani ni ok kwa watu wanaoishi mahali hapo kuwa na kiasi maalum cha kuchangia ili kujaribu kuwa katika nafasi nzuri ya kukamilisha suala hilo. lakini kwa wanaotaka kutoa rambirambi nje ya Japan wapewe nafasi ya kufanya hivyo kwa nafasi zao na mioyo yao inavyowatuma. TATIZO SIO KUKOSEA KUANDIKA 100,AU 1000, BALI NI KUTAJA KIASI MAALUM CHA KUTOA MSAADA AU RAMBIRAMBI.Mungu mkubwa atajalia ndugu yetu atasafirishwa nyumbani .Shukrani kwa wote na Poleni sana ndg, jamaa na marafiki wa Marehemu.Asante.

    ReplyDelete
  3. Napata wasi wasi msije pia mkakosea matumizi ya hiyo michango na kununulia magari badala ya kumsafirisha Mpendwa wetu kutokana na kuchanganyikiwa kwa majonzi mliyonayo.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...