Mkutano wa Kwanza wa Wanajumuiya,
March 1st 2009,
Katika Ukumbi wa Safari,
Saa Kumi Jioni (4:00pm).
Uongozi wa Tanzania Houston Community unapenda kuwaharifu wanajumuiya wa Houston, Texas kwamba kutakuwa na mkutano wa kwanza kabisa wa jumuiya siku ya jumapili, 01/March/2009, Mkutano huu utafanyika katika ukumbi wa Safari uliopo 9651 Bissonnet, Houston , TX 77036 . Muda ni saa kumi jioni (4:00pm) ,

Uongozi utakutana tarehe 28 February 2009 kujalidi ajenda mbali mbali ambazo zitazungumziwa katika kikao cha kwanza. Hivyo basi uongozi wenu unakaribisha maoni na ushauri kutoka kwa wanajumuiya wote.
Tafadhali tutumie maoni na ushauri kupitia email hii makangula2001@ yahoo.com.
Uongozi unahaidi kuyatafakari na kuyachambua mapendekezo yote kutoka kwa wana jumuiya

Uongozi,
Tanzania Houston Community
------------------------------------------------------------------------
MISA YA WAFU
Ndugu Wanaumuiya,
Kutakuwa na misa ya kumuombea marehemu Mzee Sylvester Bashasha Jumapili (22/February/2009) saa kumi jioni(4:00pm) nyumbani kwa mfiwa Gerald Bashasha.
Anwani ni:
9001 Kempwood Dr #108,
Houston,
TX,
77080
Simu ya mfiwa ni 713 932 6020

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Way to go Houstonian...... Sio kelelekelele tuu

    ReplyDelete
  2. Mtoaji wa tangazo la mkutano, nadhani ingekuwa sahihi kutumia neno 'unaahidi' badala ya hilo la 'unahaidi'; nadhani ni typing error ingawaje wakati fulani utakuta mtu alidhamiria kuandika hivyo! Wengine pia kimakosa huandika 'arusi' badala ya 'harusi', 'hahadi' badala ya 'ahadi' 'hamri' badala ya 'amri' nakadhalika; otherwise nawatakieni kila la kheri katika mkutano wenu huko unyamwezi, huku bongo yetu ni macho na masikio! - Ben

    ReplyDelete
  3. Hengereni sana Watanzania wa Huston kwa kufanya mkutano pasipo kuhusisha uchama kama wale wa London na uCCM wao. Nawatakia kikao chema, tunategemea feedback kwa maadhimio ya kikao. Kila la kheri!

    ReplyDelete
  4. Tunawatakia Kikao chema. Watanzania USA tunatakiwa kujumuika namna hii bila kubagua chama, dini wala jinsia. Mwaka umeshakwenda karibia mwezi wa tatu sasa hope states nyingine viongozi wa jumuia wanajiandaa kwa vikao vya namna hii. Mambo mengi yanahitaji umoja wetu kuanzia sherehe, misiba na mipangilio mingine ya maendeleo.

    ReplyDelete
  5. Samahani naomba nisifikiriwe vibaya kwanza naomba kama itawezekana jumuiya iwe na E-mail yake na sio ya kutumia ya Mwenyekiti ili iwape viongozi wengine uwezo wa kusoma, kwani kwa kutumia Email ya Mwenyekiti inaonekana kama ni jumuiya inamilikiwa na mwenye hiyo E-mail. Samahanini wanajumuiya kama nitakuwa nimekosea naomba msamaha na kama nitakuwa nimegusa panapo husika basi pafanyiwe kazi, Nawatakia mkutano mwema na wenye amani mungu awabariki AMIN.

    ReplyDelete
  6. "YESU AKASEMA, NIFUATE MIMI, WAACHE WAFU WAZIKE WAFU WAO"- Mathayo: 8:22
    Mzawa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...