Ndugu zetu watanzania,
 
Tunasikitika kuwataarifu kwamba Jumuia ya watanzania waishio Kansas City/MO & Kansas City/KS tumepatwa na msiba mzito wa kuondokewa na mtanzania mwenzetu Ndugu Ahabokile Malele, siku ya Jumamosi 03/21/2009.
 
Tumeunda kamati ambayo inashughulikia hili jambo.  Tunaomba msaada wa hiari wa fedha na mawazo ili kuweza kumsafirisha ndugu yetu kwao Mbeya, Tanzania kwa mazishi.
 
Unaweza kuwasaliana na wanakamati kwa taarifa zaidi:-

1. Mohamed Fundikira (816) 739-5600
2. Fred Mwisomba      (913) 999-1862
3. Eric Nyimbo           (316) 214-4680
4. Deo Rutabana        (816) 812-5495

  
Pia tumefungua account #355001747541; Jina: Ahabokile Malele Memorial Fund., kwenye Bank of America Ili kuharakisha ukusanyaji wa hii michango.
 
Gharama zote, mpaka mwili na msindikizaji (Mke) wake kufika Tanzania, ni kiasi kisichopungua US dollar 15,000.00
 
Maoni, na mawazo yenu wote yanakaribishwa. Tafadhali tunaomba mumtaarifu kila mtanzania ili kuweza kufanikisha lengo letu.
 
Ahsante
Evans Mambali

Katibu SERA
(816) 606 1604 & (816) 616 0275
e-mail: seraktb@hotmail.com 
or katibu.sera@yahoo.com
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. hakuna mtu aliyetoa maoni tangu jana kwa sababu wengi wetu ni wanafiki, waoga, wajinga, wasiopenda kusema ukweli na mengine kama hayo. mwenyezimungu anisamehe kwani yeye tu ndiye mkamilifu iwapo nitakuwa nimekosea.

    kwa mara ya kwanza tanzia lilipotangazwa hapkuwa na dalili kwamba kunahitajika mchango, mimi nilidhani jamaa ameandaa/ameweka akiba ya safari yake ya mwisho duniani na pia nikadhani anazikwa huko usa na ndio maana watu wakapewa anuani ya nyumbani kwake wakatoe rambirambi kwa mjane.
    Hivi nyie mnaobobea huko wakat kipato chenu hakiwatoshi wakati wa matatizo mna mpango gani? nawahusia mpitie upia mipango yenu ya maisha,kwani wengine umechoka sana kimaisha lakini unafuata mkubmo tu hata mnachofanya hakijulikani. wajanja wanaevaluate situation na hii sio kwa ajili ya huyu bwana bali mpo wengi unabeba boxi na kuishia kubugudhi wengine kwa matukio kama haya. kama nilivyoanza kusema nawaomba msamaha wote watakaochukia pamoja na mwenyezimungu, wale ambao mtafaidika tuombeani kheri mwenyezimungu achukue roho zetu sehemu nzuri na bila aibu, amin amin.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...