Mtaalam wa nyama choma Bi. Lemna
anakualika katika kijiwe kipya cha nyama choma na vilaji toka afrika mashariki ambacho kimeibuka jijini London. Hapo unaambiwa kila Jumapili kuanzia saa nanne mchana supu ya utumbo bure na muziki hapo ni Bongo fleva kwa kwenda mbele



Dukes Banqueting Suite

433-435

West Green Road

N15 3PJ
Dada Lemna anasema kila jumapili kuanzia saa nane mchana supu ya utumbo bure.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. kaka michuzi adress haijakamilika hiyo,muulize da lema,full adress,hajataja kuwa ni north london au east?kwa mimi najua kuwa ni north london,lakii wengine hawatajua ni wapi,nahisi ni edmunton,totenham

    ReplyDelete
  2. Unajua watu wengine hawafikirii kabla ya kuropoka!! Wewe mdau wa kwanza kwa nini usiingize hio post code kwenye google ukaona ramani na vile vile route ya kwenda huko? Au hata Sat Nav? watu wengine bwana!!

    ReplyDelete
  3. We Mdau ambae hujui kama ni North, South, East or West unaishi wapi? Post code huonyesha ni upande gani wa dira. Therefore, post code N15 3PJ inamaanisha..? Umepata kweli na aspro .....

    ReplyDelete
  4. Vichwa dafu wote nyie mpaka mliotakak umuelekeza jamaa jamaa kaandikiwa hapo All Enquiries Plz Call wamekuwekea hapo Nambari ya simu Piga uliza. Vipi Supu Utumbo bure? au sababu haipendwi msifanye vitu bure bwana Bishara hiyo. Hongera Mama jitahidini watanzania na bishara hivyohivyo.

    ReplyDelete
  5. Ni pazuri, ila kama kawaida yetu watanzania, tunapigwa bao na majirani zetu wa Kenya na Uganda, ukienda hapo Bia zote za Uganda na Kenya zipo, hakuna hata kinywaji kimoja cha kutoka Tanzania! Hivi tunalaana au ni mipango mibovu!

    Pia Chooni hakuna Maji ya moto, baada ya kula nyama na huo ugali, unaosha mikono na maji ya baridi.

    Vinginevyo kila kitu ni poa, pia watu ni wengi na wazuuuri sana.

    Mzee wa K!

    ReplyDelete
  6. mdau unaelalamikia kuosha kwa maji baridi nadhani umesahau maudhui mazima ya kuwepo kwa mama ntilie hii. maudhui ni kujikumbusha nyumbani sasa nyumbani ulikuwa unakosha mikono kwa maji ya moto? pia subiri chooni waanze kuweka magazeti ya tabloid very soon.

    ReplyDelete
  7. Safi sana, haya ndio mambo yanavyotakiwa kuwa...supu ya bure jumapili..unapata tusker yako taratiiibu....basi wabongo tuende tununue na vitu vingine...wengine watakuwa wanaagiza supu tu na maji ya kunywa..hehehe

    ReplyDelete
  8. we lemna tutakuja lakini usitutukane

    ReplyDelete
  9. BUSINESS ORIENTED LADY..wachaga kwa business starategy ni noma..nitakuja jumapili mama lema

    ReplyDelete
  10. Mdau uliesema 11:44PM jina la dada huyo ni Lemna na huyo dada ni Mmanyema wa Kigoma.
    Wanawake wa kimanyema wanfhamika kwa kua wajasiriamali wazuri na wanaweza wakatoka samba samba na wanaume.

    Unaeogopa kutukanwa na Lemna utakua una yako ambayo Lemna hakubaliani nayo. Lemna sio mwendawazimu kutukana watu bila sababu. Ukimchokoza utamjua kua yeye ni mtoto wa Mr.'P'

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...