timu zikingia uwanjani na kipute kimeshaanza dakika kumi zilizopita kati ya taifa stars na vancounver white caps wanja jipya la neshno. hadi sasa bao ni 0-0 na wanja liko wazi kwa kile kinachoaminika kwamba mashabiki wote wako vibandani kuangalia gemu letu na mani yu ambalo nasikia refa keshatoa penati ya urongo. lakini el nino kakomboa boa hahhaaa!
Home
Unlabelled
taifa stars na vancouver white caps leo
Subscribe to:
Post Comments (Atom)
Kwa kweli inabidi turekebishe lishe tuwajaze upaja wachezaji wetu. Hii noma.
ReplyDeleteBarclays Cup Premier league England latest news:
ReplyDeleteWanja la Old Trafford jijini Manchester, ManUtd 1 Liverpool 3.
Vidic wa ManUtd kala kadi nyekundu na mpira bado dakika 14 kuisha.
Liverpool wanaelekea kuvunja mwiko uliowashinda Inter Milan jumatano ktk wanja la old Trafford.
BWAWA LA MAINI LINAONGOZA HADI SASA KWA 3 HUKU MAN U WAKIWA HOME NA KIFUTIA MACHOZI 1.....Bado dakika tatu mpira uishe....Naona Michuzi full furaha
ReplyDeleteMAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
hahahahahahahaha Bao la Nne sasa, watu weweeeeeee dakika ya 90 Mh Balozi Michuzi Galiiiii kali kinoma...Ngoja nao MAN U wapigwe kama Madrid hapo
ReplyDeleteMAKULILO Jr,
www.makulilo.blogspot.com
Man U wamekunywa goli 4 na mpira umekwisha...
ReplyDeleteVipi hapo neshno? Taifa Stars changa imeibuka kidedea? Nani ana listi?
ReplyDeleteBWAWA LA MAINI OYEEEEEEE HONGERA SANA HN.BAROZI WA ZAINI KWA USHINDI WA 4-1
ReplyDeleteWadau mniwie radhi kwa kujirudia: panapo ukweli uongo hujitenga.
ReplyDeleteOld Trafford Man U 1 Liverpool 4. Liverpool wamekuwa wageni wabaya na kuwapa kipondo cha mbwa mwizi Man U.
Barclays cup premier league England , matokeo ya mechi iliyo isha hapa Old Traffor jijini Manchester.
ReplyDeleteLiverpool leo, imetoa kichapo cha rekodi kwa ManUtd, ambacho Sir Alex Ferguson hajawahi kukipata hapo Old Trafford toka kwa Liverpool FC, baada ya Liverpool kupata magoli 4 dhini ya 1 la ManUTD.
Bao pekee la ManUTD lilifungwa kwa penalti na Ronaldo dakika ya 21 ya mchezo. Wakati mabao ya Liverpool yalifungwa na Torres dakika ya 28, Gerrard dakika ya 44 kwa penalti, Aurelio kwa free-kick dakika ya 77 na Dossena dakika ya 90 ya mchezo.
Wauzaji wa pombe za kienyeji(mataputapu) wa kule uwanja wa fisi leo watapata hasara kwa sababu wateja wao 95% ni washabiki wa Man United na leo wamejifungia ndani kuogopa kuchekwa.
ReplyDeleteTeh!!!!!Teh!!!!!Teh!!!!!!!!!!!!!!!!
Maximo ajifunze kwa liverpool kijana Steven Gerrald ana kesi mtaani.lakini uwanjani anafanya vitu vyake.maximo utasikia nidhamu ndani na nje.
ReplyDelete