Jacob Zuma wa ANC akiwa na Mzee Nelson Mandela
Zellen Zille wa DA
MH. Lekoata wa COPE

Kaka Michuzi, 
Kama wengi mjuavyo masaa machache yajayo Afrika Kusini wataingia kupiga kura kumtafuta Rais wa tatu wa Afrika kusini huru baada ya kuondolewa kwa utawala wa kikaburu mnamo 1994.

Swali tunalojiuliza ni nani atakuwa Rais mpya wa nchi hii? Kutokana na kura za maoni zilizokusanywa nchi nzima zinaonyesha kuwa mchuano mkali utakuwa kati ya Mr Jacobo Zuma(ANC), Mwanamama Mahiri Zellen Zille (DA) na Mr Lekoata wa (COPE). 

COPE ni chama kipya kilichojiengua kutoka ANC mwishoni mwa mwaka jana. Juzi jumapili katika kuhitimisha kampeni zao chama cha ANC kilifanya "Suprise" kwa kumbeba Mzee Nelson Holithatha Mandela uwanjani bila watu kutarajia kuwa angekuwepo. 

 Nitaendelea kuwaletea matokeo zaidi. 
Na Mdau James Sabuni wa Cape Town

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. Kuna kila dalili kuwa wasauzi watampa kura zao zuma. kinachonisikitisha sana ni kuwa wasauzi mbali ya kuwa wana asilimia kubwa sana ya wagonjwa wa ukimwi na wanahitaji mtu mwenye kuelewa tatizo lao hili kuwaongoza katika kupiga vita wanamnachagua mtu mwenye mawazo finyu juu ya jinsi ya mtu anavyoweza kupata ukimwi. itakuwaje unamchagua mtu kuwa kiongozi wa nchi yeye gonjwa sugu kama hili ambae amekiri kufanya mapenzi na mtu mwenye ukimwi na excuse yake ni "lakini nilikoga baada ya tendo" hi si sawa kabisa na ile excuse ya "i smoke but i did not inhale"

    ReplyDelete
  2. Mr Lekoata wa (COPE) hangombei urais..kulikoni mleta news au ndio upo nje ya ulingo wa news?

    ReplyDelete
  3. Anony wa kwanza, samahani hao wasauzi wanajua wanachokifanya, sio wababaishaji hao, wanamjua Zuma. tena ni bora Zuma aliyekiri kwamba alifanya hiyo kitu na kuoga, kwani hata wataalam huwa wanasema hivyo kama umefanya bila "kifanyio" basi maji ni moja ya njia za kuweza kukuepusha na maambukizi. Zuma ni mtu wa watu na ni mpiganaji tangu zamani sana, usije mfananisha Zuma na wauza sura wa mataifa mengine ambao uhuru waliupigania wenzao na wao kuja kuanza kuhujumu tu.

    ReplyDelete
  4. taifa la wabakaji,,,
    anyway kila kipindi kina maana yake na mtu wake

    Zuma ni kituko yan ata ukimwangalia tu yan bazaz mtupu hahahaaaaa

    mzee wa totoz,ikulu yao ntaenda na jinsi nlivyo?lazima asalende apa!

    ReplyDelete
  5. IVI JAMANI MZEE MANDELA NDO ADI ASHIKILIWE HAWEZI KABISA SIKU IZI KUTEMBEA??
    SI WANGEMBEBA KTK WHEELCHAIR SIO VIZURI WAMTESA IVI SHUJAA WA AFRIKA

    Mungu amjalie afya na siku tele

    ReplyDelete
  6. Hivi huyu anayemsaidia Mzee wetu kuinuka ni Ma Winnie?

    ReplyDelete
  7. weka basi habari za uchaguzi bondeni!
    kwanini njia wanaotumia wao na sisi tusiitumie. kwani ni nzuri.

    tunatakiwa kujua idadi ya viti vya bunge na idadi ya wapiga kura halafu tunagawanya kujua kila kiti cha bunge ni kura/kula ngapi.

    halafu watu wanakwenda kupiga kura..
    /kula!

    hakuna kampeni za wagombea viti vya ubunge ni uraisi na chama tuuuuuuu

    hapo imekaaje??

    nadhani tutaondokana na majimbo yale ya zenj yenye wapiga kura 10,000 wakati kule njombe kuna jimbo la zaidi ya 100,000

    ..kwa namana hiyo utaona mbunge mmoja wa bara ni sawa na wabunge zaidi ya 5 wa zenji...

    wadau mnasemaje???

    heri mimi sijasema!
    http://www.sowetan.co.za/News/Article.aspx?id=987257

    ReplyDelete
  8. South Africans are a joke and Zuma is a clown. Hii design si ndio iliyoifikisha Zimbabwe ilipo? Ingalikuwa ni mimi ningempa kura Mama ajaribu kuliko huyu mpuuzi Zuma.

    Mdau, Boston, US

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...