wadau wa washington kwenye gemu
mobhale matinyi (shoto) na hasheem thabeet walikuwepo
ngoma uwanjani
hatari langoni
kepteni wa kudumu wa houston alune mwasambiwite akiwajibika na mpira
mfungaji wa magoli yote mawili akiwa na mwenzie

kiatu mtu
watazamaji wakielekea uwanjani
refa
ngoma inogile
bongo united
houston

Timu ya soka ya Watanzania kutoka mjini Houston, Marekani, jana Jumamosi ilifanikiwa kuibana timu ya Watanzania wa mjini Washington DC na kutoka naye sare ya magoli 2-2.
Ilikuwa ni Washington DC iliyoanza kupata bao kunako dakika ya 5 kupitia kwa mshambuliaji wake Geus Tall. Kwenye dakika ya 35, Houston walisawazisha bao hilo baada ya Mudrika Majaliwa kupiga mpira wa adhabu ndogo.
Kipindi cha pili kilianza kwa Washington DC kushambulia kwa nguvu huku Houston wakihofia kukandamizwa na refa ambaye ni mkazi wa Washington DC. Hatimaye kwenye dakika ya 25, Elvis Mnyamuru alitingisha nyavu za wageni.
Haikuchukua muda, mshambuliaji Majawali alisawazisha tena kwenye dakika ya 30. Itabidi Washington wajilaumu kupita kiasi kwani mshambuliaji Majawali alikuwa mchezaji wao kutoka mjini Seattle ambaye walimtema wakati wa kupanga listi nusu saa kabla ya mechi.
Hii ilikuwa mechi ya marudiano baada ya ile ya mjini Houston, Novemba mwaka jana ambapo timu zilitoka sare ya magoli 3-3. Mchezo mwingine wa marudiano inatazamiwa kuchezwa Novemba 2009.
Aidha, Houston walilalamikia uwanja kuwa katikati ulikuwa na mgongo kama wa nyangumi na magoli kama midomo ya papa. Timu ya Houston hata hivyo imepiga hatua kubwa baada ya kuchapwa mabao 8-2 kama vidagaa katika mchezo wa kwanza uliofanyika mwaka juzi.
Baada ya mechi baadhi ya wakazi wa Washington DC walimlalamikia refa wao kwamba hakufanya jitihada za kuhakikisha timu yake inashinda nyumbani. Baada ya mchezo ilifuatia sherehe ya nyama za kuchoma ambayo ilisindikizwa na disko la nguvu katikati ya Jiji ilipofika usiku.
Mgeni wa adabu katika shughuli zote zilizofurika watu alikuwa nanihii.
Nikiripoti kutoka uwanja wa Greencasttle, ni mwandishi wako wa blogu ya jamii.












Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 18 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 24, 2009

    huyo aliyeweka filimbi mdomoni mbona anafanana na Jay-Z. Jay-Z ndo alikuwa refa??

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 24, 2009

    Huyo mrefu kuliko wote hapo picha ya kwanza si mngemuweka pembeni kabla ya kuchukua picha jamani?? manake kawafanya wenzake woote waonekane mbilikimo wakati washkaji na wenyewe warefu!!! huyo hashimu thabit nini!!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 24, 2009

    jamani ndugu zangu wa dc tusikimbilie mambo ya aggregate sasa baada ya kutoa droo ya 2-2 mnakimbilia aggregrate?? ningependa kujua ni nani aliyepost hii message kwa michuzi!! manake si mshindani wa kweli bali anataka kufurahisha umati wa watu na wanablog wakati reality ni kwamba mechi imeisha 2-2 na kwa kweli DC wametuaibisha kwa kutupeleka kwenye uwanja mbovu usio na hadhi ya kuwa kwenye jiji kubwa kama lile!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 24, 2009

    D.C mnahaibisha. Hayo magoli kama yale tuliyokuwa tunachezea shule za msingi bongo !!

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 24, 2009

    hee hao walikuwa wanacheza rede?? japokuwa sports is not rechable ila hayo mabao ya tobo hayo.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 24, 2009

    wewe chururu vipi mbona comments nyingine hutoi wewe vipi wewe,

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 24, 2009

    Duuh yote 9 mimi hayo magoli ndio yameniacha hoi kama ya ragbi hata hapa kwetu kisiju tuna magoli mazuri.
    mdau
    kisiju pwani

    ReplyDelete
  8. Yaani mlikosa kabisa uwanja hadi mkatumia uwanja wa Rugby?

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 24, 2009

    Haki ya nani, wewe anony wa kwanza umechukua comment yangu. Maana refa Jay zee mtupu, kah? Duniani kweli wanne wanne....

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 24, 2009

    Hapo ndio globu ya jamii inapoleta raha. Habari kama hizi huwezi kuzipata kwenye Uhuru na Mzalendo.

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 24, 2009

    mleta habari inabidi aende TSJ kusomea uandishi wa khabari!

    kwani haina vionjo vya mwandishi mahiri

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 24, 2009

    Yaani Richard Mawenya (refa) ndo amekuwa JayZ these days? people please, he ain't close to Jay Z. huyo aliyeweka hizo comments lazima is one of his baby mamas

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 24, 2009

    Where the haters at all the hatin cats
    Yeah Look in the mirror nigga hate on dat...HAHAHAHAH!


    WABONGO BWANA, KAZI YENU KUSENGENYA 2 ....Yeah let em c me
    Hi hater
    Pull of easy. Bye Hater
    U dont like me? Why hater
    Won't U tell em how mad I make ya
    I ain't caught up in all da hot talk.....

    ReplyDelete
  14. AnonymousMay 24, 2009

    KAKA MICHU NAOMBA UMPE Hİ NDUGUYANGU AMRANI HAPO MWAMBIE KIPARANG'ANDA ANKUPA Hİ FROM turkey

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 26, 2009

    kwi kwi kwi

    refa bila jezi,mmechacha sana

    iyo migoli

    aya wabeba box

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 27, 2009

    timu ilovaa jezi ya njano namjuwa dedi ruba peke yake wa madison ya zenji.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 28, 2009

    Peter Bategeki kikapu vipi? Mbona tunakuona kwenye soka tu.

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 29, 2009

    WABONGO WA DC MMECHOKA NA MEMORIAL WEEKEND ILIKUWA MBOVU SANA..MMETANGAZA HUMU FOR A LONG TYME WATU TUMESAFIRI HADI HUKO NYAMA ZENYEWE KAGRILL KADOGO WATU 100....HEBU MJE MASS MUONE TUNAVYOFANYA SHUGHULI ZETU..

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...