

Katika kuhakikisha burudani, ubunifu , sanaa na utamaduni kitanzania unawakilishwa ipasavyo katika shindano la urembo,; Miss Tanzania EU 2009 litakalo fanyika mjini Essen Germany, wasanii mbali mbali kutoka bongo wamealikwa...
Akielezea Blog ya jamii kwa njia ya simu mratibu wa mashindano hayo Nashe Mvungi amesema wasanii wa muziki wa kizazi kipya MB Dogg na Bushoke watapanda jukwaani kutumbuiza, mbali na hao kutakua na makundi mengine ya burudani kutoka sehemu mbalimbali za Ulaya.
Katika kinyangányiro hicho mgeni wa heshima ni Balozi wa Tanzania nchini Ujerumani Mheshimiwa A.Ngemera.
Akizungumzia washiriki wa mashindano hayo Nashe alisema nafasi bado ziko wazi kwa watakaotaka kushiriki, form za kushiriki zipatikana katika:
www.misstanzania.eu
au
email info@misstanzania.eu
Vile vile mratibu huyo alisisitiza kuwa washindi wa 3 wa mwanzo watapata nafasi ya kwenda United Kingdom kwenye mpambano wa Miss Tanzania mjini London.


Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...