Kaka Michuzi nashukuru kwa kufanikisha mawasiliano ya watanzania kutokea sehemu mbali mbali duniani.

Kaka naomba kama inawezekana unirushie kwenye blog yako mswada wangu. Nilikuwa napenda kujua gharama za usafirishaji kwasasa kutoka mikoa ifuatayo kwenda DSM: Iringa, Mbeya, Rukwa, Ruvuma, Shinyanga, Tanga, Kilimanjaro, Arusha na Manyara. Gharama inaweza kuwa kwa kilogram kwa kilometer au tani kwa kilometer. Gharama hizi hasa ziwe za usafirishaji wa mazao kama mahindi na maharagwe.

Natanguliza shukurani zangu kwako na kwa wale wadai watakaokuwa na muda wa kunisaidia.

-- 
Mdau FJM

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 06, 2009

    Aisee yaani we unashangaza sana kwani huku bongo huna jamaa wa karibu ambaye ataweza kukufanyia hiyo kazi yako kwa ukaribu Au una cha kuuliza? acha kujitenga na ndugu zako

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 06, 2009

    Ama kweli hii ni blog ya jamii, kila mwenye goma lake hulicheza!

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 06, 2009

    Mdau FJM,

    Fanya hivi:

    1. Fungua tovuti ya Google.co.tz2. Search "Tanzania Freight Forwarders" (with or without the quotes)
    3. Utaona tovuti za makampuni ya usafirishaji wa mizigo (freight forwarders)
    4. Wasiliana nao watakupa bei zao.

    ReplyDelete
  4. AFANDE MIDAKOMay 06, 2009

    NENDA KAULIZE STENDI YA FUSO JANGWANI

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...