shughuli katika mji wa unguja zilisimama kwa muda jana wakati wa swala ya kumuombea marehemu profesa haroub othman katka msikiti wa Masjid Salama eneo la Msufini na baadaye msafara wa kwenda mazikoni shambani kwake Chuini. Hakika alikuwa mtu wa watu kwani mazishi yake yameelezwa yalikuwa ni makubwa kupata kutokea visiwani kwa muda mrefu
mitaa yote ilifurika waombolezaji wakati jeneza lilipokuwa likipitishwa
mistari ya waombolezaji waliojipanga barabarani kusubiri jeneza ilitanda kila mahali
viongozi wa serikali walikuwepo kumsomea marehemu
viongozi wa vyama vya upinzani walikuwepo kuomboleza
masjid salama ulifurika ndani
nafasi ilikuwa haba masjid salama kiasi waombolezaji wengine walilazimika kuswalia nje. picha zote na mdau othman mapara.
-----------------------------------------------------------
Mpiganaji mwenzangu Michuzi,
naomba kwa kupitia blog ya jamii, nitume salam zangu za rambirambi kwa familia, ndugu, jamaa, jumuiya ya wasomi 'Mlimani' na duniani kote na kwa Watanzania wenzangu kwa kuondokewa na mwanazuoni tunu yetu na niliyemheshimu sana ndugu yetu Profesa Haroub Othman.
Pigo hili limenikumbusha lile la hivi karibuni lililowakuta wasomi wa dunia na sisi 'wapiganaji' pale alipotutoka Dk. Tajudeen kwa ajali ya gari kule Nairobi.
Pia nichukue nafasi hii kutuma rambirambi zangu kwa familia, ndugu, jamaa na Watanzania wote kwa kuondokewa na rafiki yangu na mzee wetu Sheikh Suleiman Gorogosi ambaye kwaye mawaidha yake yaliyojaa hekima yalikuwa hayamithiliki na niliyaheshimu mno.

Wote, naomba Allah azihifadhi roho zao mahali pa amani daima--AMINA.

Mdau Saidi Msonda,
Sudan.










Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 30, 2009

    Pumzika mahala pema Peponi baba inatia uchungu sana.Tutazidi kukumbuka na kukuombea zaidi maana hiyo ni njia ya kila mmoja wetu.
    Rest in peace.
    mdau

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 30, 2009

    mICHUZI HUU NI MFUMO DUME NINI? MBONA WAOMBOLEZAJI WANAWAKE HAWAPO KATIKA PICHA? AU TUELEWEJE?

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 30, 2009

    tutakukumbuka baba yetu, babu mpendwa, PROF. HAROUB.

    Mungu akulaze pema peponi na kila la heri likutangulie hko uendako.

    tutakuwa nawe kiroho kwani kimwili ndio haupo nasi tena.

    R.I.P

    ReplyDelete
  4. Al MusomaJune 30, 2009

    Walikuwa maelfu kwa hakika, si mamia...

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 30, 2009

    Anon wa pili unamaana gani ukisema mfumo dume? wanawake unawataka wa nini? wamekulalamikia kwamba hawakuwepo iliwauma? nadhani ni wakati tuheshimu taratibu za imani za wenzetu sio kila kitu lazima uchangie. Heshima kwa dini ya wenzako plz u r grown up now

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 30, 2009

    Rest in peace Uncle!
    Thanks for everything!

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 30, 2009

    Mzee kwa kweli amezikwa,yaani umati wote huo.Hiyo inaonyesha ni jinsi gani alivyokuwa mtu wa watu.Mungu akuangazie na akuweke mahala pema peponi.

    Mkulima-Kijijini Gezaulole

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 30, 2009

    sisi ni wa Allah na hakika kwake tutarejea, hakika ya mauti ni mawaidha kwa waumini. hakuna aliyetaraji kua prof angetutoka kwa wakati huu, lakini kazi yake allah haina makosa. mungu akusameh na akupe kauli thabit huko wendako.
    poleni wafiwa na wazanzibari wote.
    mdau coventry university.

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 30, 2009

    M/mungu anlaze mahali pema peponi Amini kwani sisi sote twaenda huko uko ila tu pia tuwape pole wale jamaa wote.
    kwani huyo jamaa hapo juu anataka kujua kuhusu wanawake kwani wewe ujui kuwa pale ni msikitini sio kanisa na pia wacha ujinga kua na heshima ya kueshimu dini za wezako.

    Ndambe uk

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 01, 2009

    He was a man of substance. May Almighty God rest his soul in eternal peace.

    R.I.P - Haroub

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...