Wadau wa globu ya jamii kunradhi na ashakhum si matus!
Nina swali langu hili ambalo niliwafuma wazee fulani leo (siwataji jina) wakizozana na kuulizana hivi nani aliyeanzisha tabia hizi za wanaume kuvaa chupi? Je utamaduni huu ni wa ki afrika au? Je ni haki kwa mwanamme kuvaa chupi?
Gumzo hili nililikuta katika bunge la faragha la wazee fulani wakiulizana na pengine wasipate jibu, na kwa kuvutiwa na hoja yao hii nikaona sitakuwa mtovu wa adabu kama swala hili nitaleta na kumkabidhi mstahiki mkuu wa wilaya ya naniino ili aliweke uwanjani.
Mpaka sasa jibu halijapatikana; kwa nini wanaume tuvae chupi? na kuna faida ipi ya kuvaa chupi wakati tayari tumevaa nguo ambayo haiwezi kupeperushwa na upepo?
Na kama utamaduni huu wa kuvaa chupi ni wa kigeni basi nani aliyeuleta?
WAZEE NAOMBA MNIWIE RADHI,ASHAKUM SI MATUSI WA MASWALI HAYA!(na maswali yenyewe si yangu bali nami kama nilivyojielezea nimewafuma wakubwa wenzenu yakiwaumiza kichwa) pia naomba majibu yasiwe na uchafuzi wa hali ya hewa.
Shukurani
Mdau MsemaKweli

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 29 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 12, 2009

    kwa kweli nimependa swali lako niuzuri kuilimishana kwa mamboz tafauti haswa tuko wengi mamboz mengi hatujuwi kwa nini yanatokea ghafla siku hizi hapo kale tunaambiwa yalikuwea hakuna.lakini kama sija kosea kuna siku nilikuwa nikitizama tv hapa niishipo mara habari za america wakawa wana leta mamboz tafauti ya kiafia moja wapo wakawa wanazungumzia kuhusu mwanamume kuvaa chupi wachunguzi wanasema niuzuri kuvaa chupi eti haileti saratini.lakini siamini hili jamboz nilazima tuliende juu chini mpaka tulijue hapo zamani kweli kulikuwa hakuna vombo vya uchunguzi utasikia mtu kama kwa homa au kichwa kumbe ilikuwa kensa.kuna siku pia oprah kwenye tv kamleta dr moja akizungumzia kuhusu wanawake wasivae chupi kila mara ili kupate upepo ilikujikinga na maradhi kama kensa nikacheka sana.ambapo tangu tuko wadogo tunafundishwa kuvaaga chupi siku hizi kume kuwa na wachunguzaji wengi shukrani mdau toronto.

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 12, 2009

    Chuni ni aina ya nguo ambao inaweka maumbile yako ya kiume sehemu moja. Ukivaa suruali yenyewe bila chupi, uume wako utakuwa unaning'ina chini na kuonyesha uume wako ulivyo. Na pia unapofanya tendo la ndoa, baada ya kumaliza, kuna maji maji huwa bado yanatoka katika uume, kwa hiyo chupi husaidia kuzuia maji yale yasichafue suruali yako uliyo ivaa.


    Na kwa Mwanamke, chupi humsaidia kila wakati. Wakati wa hedhi, akikojoa, au akifanya tendo la ndoa, chupi humsaidia sana ili asichafue gauni au kanga zake alizo vaa.

    Kuvaa chupi ni asili ya watu wote duniani na si utamaduni. Unakumbuka ile hadithi ya Adamu na Eva walipojigundua kuwa walikuwa uchi, cha kwanza walijifunika utupu wao. Na wanamke alijifunika uchi na maziwa yake. Tokea siku hiyo ikabidi wajitengenezee, chupi zao wenyewe, tena zilikuwa za kamba, inamaana chupi hiyo ilikuwa ikifunika mbele na nyuma ilikuwa kamba.

    Kaka Michuzi nakuomba radhi kama nitakuwa nimekujibu vibaya, na pia nafikiria maelezo yangu yatasaidia maada hii uliyoiweka hapa. Hii ni kutoka Michigan. Inshaallaah!

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 12, 2009

    Ninahakika uliyeuliza hili swali ni mwanaume, basi jibu ni rahisi jaribu kutembea bila chupi halafu jijibu kama unahaki ya kuvaa ama kutembeza kengele na filimbi yako kama bembea!!

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 12, 2009

    Kwa mtazamo wangu, sifaham hao wazee walisimamia hoja gani walipokuwa wanajadili suala hili, lakini mchango wangu kwa wanajamii ni kuwa Je chupi gani ni bora kwa wanaume? mifuko ya kubebea mbegu za kiume imeumbwa ining'inie nje ya mwili wa binadam na sio ndani kama viongo vingine(figo,kibofu nk) ili kwamba iepuke kiasi kile cha joto cha ndani ya mwili wa binadam. Ndio kusema hali ya joto kama lile la ndani ya mwili wa binadam sio mazingira bora kwa mbegu za kiume. Kwa sababu hiyo chupi iliyobora kwa wanaume hasa wanaotaka kupata watoto ni ile ambayo haiibani mifuko hiyo miwil karib kabisa na mwili.Kwa wale walionashida kupata watoto, swali la awali kabisa kujiuliza ni kama unavaa chupi ambayo inaruhus mifuko ya mbegu kuning'inia vizuri na kutobanwa mwilini. Sijui kama hao wazee pia walifikiria hilo kuwa kwa hali ya hewa ya joto kama baadhi ya sehem za Tz, kwa nini wanaume tuvae chupi ambazo zinaathiri uwezo wa uzazi na kama endapo tumeiga tu wenzetu ambao wanaish kweny nchi za baridi.Kwa Ubora wa uhai wa mbegu za kiume, kuvaa bucta au chupi isiyobana ni vizuri zaidi.
    Mdau: Chaimaharage,Songea.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 12, 2009

    Mdau kwa mimi ninavyoelewa wanaume hatuvai chupi, tunavaa boxer sasa tafuta kiswahili chake. Wanawake pekee ndo wanavaa chupi, kwa mwanaume kuvaa chupi hapo tutajiuliza maswali mengi kwamba labda wewe ni dada poa!!! Chupi ina umbile tofauti na boxer, boxer inatundu kwa mbele kuwezesha kuchomoa sehemu yako nyeti na kujisaidia haja ndogo. Nafikiri tutafute kiswahili cha boxer tusiite chupi kwa mwanaume. Chupi ni kwa wanawake. Natumaini utakuwa umenielewa mdau?
    Kwa nchi zilizoendelea mwanaume huwezi ukasema " I am wearing an underwear" they will be shocked and think that you are a gay" Instead you may say I am wearing a boxer" Tafuta tafsiri ya kiswahili kwa neno "boxer"

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 12, 2009

    kwanza jiulize kwani wanawake chupi huwasaidia nini?umuhimu wa chupi kwa mwanamke ndiomumuhimu wamchupimkwa mwananume

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 12, 2009

    Kama unaweza kwenda commando we nenda commando. Kuvaa chupi hakusaidii kitu chochote kile. siku hizi hakuna noma wala nini. Kama mwanaume asipovaa chupi na ukakumbwa na mfadhaiko basi hilo litakuwa noma babu kubwa maana kutakuwa na ramani ya africa katika suruali yako. na kama uko ngangari, basi haijalishi nenda commando. Hakuna research inayoonesha kuwa kutovaa chupi kunaweza sababisha saratani au gusha!
    Cha kufikiria tu ni kwamba ukiiacha ikaning'inia kwa muda fulani labda yaweza kurefuka maana kuna gravity inayoivuta kwenda chini. Unaweza jaribu hiyo inaweza kuwa ni theory yangu! badala ya kula mkuyati kurefusha, usivae chupi!!! That's it!!!
    Mdau

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 12, 2009

    tena bra mwanamke anaweza asivae chupi kama nguo ya juu haikuwa transparent basi kwa mwanamke hamna noma. lakini kwa mwanaume duh!!!! sasa vyombo vyote viwili vikining'inia mwanawane si inakuwa dhahama??!!!!!! mwanamke ana chombo kimoja tena kiko intact lakini mwanaume vyombo vina-hang hembu piga picha ukicheza mpira na vyombo mning'inio duh!!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJune 12, 2009

    kufuri kwa mwanuume huiepusha dunia hii na maovu mengi!!! ngoma zikining'inia basi ujue ubakaji njenje!!!! halafu ukiwa katika mazingira shawishi inakuwa balaa zaidi sababu kama zipu haiko imara basi hukawii kuonekana kituko cha siku. jamaa atatoka nje live ha'fu inakuwa howcome sio!!!

    ReplyDelete
  10. ngoko ya jomoJune 12, 2009

    majibu ya maswali mengine ni kufanya majaribio ya jambo husika.Vaa suruli bila chupi, suruali yenyewe isiwe na mifuko ya mbele usije ukajihami kwa kuweka mikono mfukoni,panda daladala za mbagala au dongolamboto ,harafu mdada asimame mbele yako akubandikie tako sehemusehemu.Utajijibu mwenyewe kama chupi inafaa au la.Utanijibu pitia blog hii,kabla hujafanya nijulishe niandae hati za kujakukuwekea dhamana polisi.

    ReplyDelete
  11. AnonymousJune 12, 2009

    uko juu annons wawili...ni kwamba hamjui kiswahili au???mboni hamueleweki?

    chupi sio lazima sana kwa mwanaume,kwanza kwa joto la bongo khaaaa ndo mwazo kuleta uvundo,utakuta mtu anavaa bukta na chupi khaaaaaaaaaaaa

    mara moja moja si haba ata wamama wakiwa wamevaa trouserz msivae chupi au vaeni G-string...hewa ni muhimu saaaana

    asante

    ReplyDelete
  12. AnonymousJune 12, 2009

    annon #4 toka juu...

    asante sana kwa jibu

    ReplyDelete
  13. AnonymousJune 12, 2009

    Anko michu nami naomba nichangie,kwanza Mdau wa uni 12 ,7:58 anataka kutuchanganya chupi ni neno zuri tu la kiswahili, umagharibi usitufanye tuige kila kitu.sisi tuna chupi za kike na za kiume hiyo unayoita boxer nia aina tu ya kaptula ya ndani.
    Pili niseme kwamba chupi hizi za sikuhizi zinabana sana na hii husababisa wanaume wengi kuwa na bunduki fupi, huku kwetu visiwani watoto wa kiume huwa hawavalishwi chupi mpaka wapevuke (baleghe) hii husaidia kijana kuwa na "bunduki" ndefu kidogo hivyo kumridhisha mwenza pale anapooa.
    Chupi kwa akina mama wengi huwaletea joto, na maradhi mbalimbali ya ukeni,wanawake wa ulaya na amerika huvaa chupi zaidi kwa kuwa huvaa nguo mbili tu za chini aidha sketi fupi tena yenye kuruhusu uoni(tranparent) na chupi.lakini huku kwetu akina mama huvaa nguo nyingi na kujifunika vizuri ni vema wasivae chupi ili kupitisha hewa nzuri.
    Kwa hiyo chupi si vibaya kwa wanaume kuvaa,lakini kama huna pilikapilika za mizunguko piga tu bukta au msuli vitu vining'nie.
    Asante

    ReplyDelete
  14. AnonymousJune 12, 2009

    Kwa mwanaume asipovaa chupi au boxer uume unakuwa huru kujigongagonga kwenye suruali au hata msuli aliovaa. Hii inasaidia kuufanya uume kupata sugu, na katika hali ya kupata sugu inasaidia kumuepusha mwanaume asipate kirahisi maambukizi ya magonjwa ya zinaa ikiwamo ukimwi.

    Pia uume unapokuwa huru bila kubanwabanwa na vijinguonguo unapata nafasi ya kurefuka ipasavyo na hivyo kuweza kutoa dozi ya uhakika kwa mpenzi wa kike.

    ReplyDelete
  15. AnonymousJune 12, 2009

    Chupi hazina manufaa yoyote kwa wanaume. Tena zina madhara kibao. Mtu akivaa chupi iliyobana kwa mfano uume wake haupumui inavyopaswa,joto zaidi lina madhara kwa mbegu za kiume tena wengine wanaamini kuwa kuubanabana uume wako unaupunguzia urefu wake yaani haukui. MIMI SIVAI MACHUPI NG'O. naachia mzee mzima anilindie viatu he hee

    KILI
    BG

    ReplyDelete
  16. AnonymousJune 12, 2009

    Kuna mjadala mwingine nilishawahi kusikia eti kuvaa chupi kunafanya mashine ipinde, sasa sijui kama kuna ukweli katika hili?

    ReplyDelete
  17. AnonymousJune 12, 2009

    Chupi kwa wanawake pia sio kitu cha maana. Chupi kwa mfano hizi wazoziita "thong" epuka zaweza kuharibu hata ubikra wa binti, ule ukamba waharibu shepu ya nanihii badala ya kufunga mdomo basi inacheka tuu. Kama wajifuta vizuri baada ya haja mambo yatakuwa sawa. Ile kitu imeundwa ili ipumue hii kuzibaziba wala haisaidii. MIMI MAMA WATOTO WANGU NIMEMKATAZA KABIA KUVAAVAA HAYA MACHUPI. freedoooom!

    KILI
    BG

    ReplyDelete
  18. AnonymousJune 12, 2009

    Dah,Chai maharage toka Songea umemaliza kiaina. Ni kweli twahitaji hewa, vyombo vinhitaji kupigwa upepo ili viwe na afya njema ndio maana hata wabunifu wa mavazi hayo ya kiume wameamua kutengeneza bukta pensi mzee, hata wadau wa Pwani utakuta wametinga msuli au kanzu ndani amekandamiza pensi yake "small" ya livapul, au arsenal kiaina lengo ni kuweka ventilations za kutosha ili kutoathili ukuaji wa vyombo.
    Nakubaliana na wote wanaosema kwamba chupi si nzuri sana kwa wanaume na kinababa
    Gatutso!

    ReplyDelete
  19. AnonymousJune 12, 2009

    Ukitaka kuhakikisha kuwa kwanini wanaume tusivae chupi za kubana kuna tatizo la watoto ambalo wanazaliwa na Undescended Testicle or Cryptorchidism: hii ni pale mtoto anapozaliwa na mifuko ya mbegu imebaki ndani na haining’inii nje kama watoto wengine. Tatizo hilo lazima litatuliwe mapema kwa kuzitoa na kuzining’inisha testi hizo nje la sivyo mtoto huyo atakapokuwa atakuwa na tatizo la uzazi na pia katika nafasi nyingine kuepusha uwezekano wa kansa. Hivyo hali ya joto sio mazingira bora kwa mbegu za kiume na hivyo tunapovaa chupi/bucta ni bora kuzingatia kuepuka kuzibana karib kabisa na mwili ili kutoathiri uhai na ubora wa mbegu.
    Mdau:chaimaharage, Songea

    ReplyDelete
  20. AnonymousJune 12, 2009

    bro michuzi wambie wasomaji wako. kitaalamu. chupi ilitokana na tatizo liitwalo TESTICULAR TORSION. hutokea kwa vijana walio katika umri wa kwanza wa kubarehe, maumbile yao hukua na hasa kende, ambapo kutokana na kuongezeka kwa mizunguko na utafutaji katika umri huu,kuna uwezekano mkubwa wa kende kujiviringisha katika mhimiri wake na hapo hutokea maumivu makali sana, ambapo hupelekea kupoteza kende moja kwa matibabu ya haraka au zote mbili kama atacheleweshwa zaidi ya masaa 24. zaidi search google kwa heading juu.
    kila kitu kina sababu ,sio urembo tu.

    ReplyDelete
  21. AnonymousJune 12, 2009

    Wanaume si haki kuvaa chupi,kwani akishavaa suali basi chupi ya nini?tena kujilundika minguo mingi na nchi zenyewe ni za joto.
    Kwa kweli mwanaume haipaswi kabisa kuvaa chupi,chupi ni vazi la kinamama kwa hajili ya kuwastili.

    ReplyDelete
  22. AnonymousJune 12, 2009

    SHUPI AU TUNAITAA KUFULI HUWA NI MLINZI WA UUME KWANI BILA CHUPI WAWEZA AIBIKA YAGHE UKIONA UPENDAVO NA MJOMBA AKIAMKA SURUALI YAKO ITAONYESHA NI HERI UKIWA NA KUFULI ITASADIA KIDOGO ALAFU NIMEFANYA UCHUNGUZI KWA SEHEMU ZA JOTO KAMA BONGO WANAUME WENGI WANAVAA G-STRING NA NIMUURUA SANA KWA WANAUME SASA KWA USHAURI WANGU NYIE MLIO BONGO JARIBUNI KUVAA G-STRING MTAIPENDA KULIKO KUACHA KUVAA CHUPI NA BUKTA AU KIPENSI CHA ZAMANI HAHAHA

    ReplyDelete
  23. AnonymousJune 12, 2009

    Globu ya jamii imenena. Kuanzia sasa wanaume tuache kuvaa chupi ili kuruhusu kende zifanyekazi vizuri.

    ReplyDelete
  24. AnonymousJune 12, 2009

    wazee walikuwa hawazungumzii chupi ambayo mtoa swali anazungumzia. chupi ilikuwa ni lugha ya fasihi tu ili wewe usijue wanazungumzia nini. kijana mdogo ukome kutega masikio wazee wakizungumza.

    ReplyDelete
  25. AnonymousJune 12, 2009

    chupi kwa wanaume zilikuwa zikivaliwa enzi ya nyerere sikuhizi wanaume wanavaa boxer unless otherwise we si ridhiki, na hao wanaosema eti usipovaa chupi utakuwa unapiga kengele na filimbi ni kweli kwa siku za mwanzo utajisikia tofauti lakini ukisha zoea hakuna cha kengele wala filimbi. huku tulipo sisi wanawake huwa wanava chupi wakiwa wamesafiri kwenda mwezini, siku ambazo wapo hapa duniani akivaliwi kitu kwani inasadikiwa kuwa duniani kuna joto kuliko mwenzini kwa hiyo upepo ni basic need na ole wako ubake,kwani wanasema ukiona na ukitamani sema kwani uondoki nacho

    Mbega mweupe

    ReplyDelete
  26. AnonymousJune 12, 2009

    kuvaa chupi ni uamuzi wa mtu.unaweza kuvaa au usivae hakuna atakayekuuliza.

    ReplyDelete
  27. AnonymousJune 13, 2009

    ZOTE HIZI NI MBWEMBWE TU KUNOGESHA UTAMU,UKIAMUA KUVAA WEWE VAA CHUPI TU SWALA LA ILITOKEA WAPI SIORAHISI KUJUA ITAKUWA UNABUNI TU ZAIDI YA ADAMU NA EVA. MIMI SIVAI CHUPI NA WALA HIYO MIFADHAIKO SIIPATI WALA NINI WALA HAKUNA CHA RAMANI KTK SURUALI. NILIVAA CHUPI NIKAONA MIYEYUSHO TU SO MIE NA CHUPI MBALIMBALI KABISA NA HAKIHARIBIKI KITU.WALA KUVAACHUPI HAKUIFANYI NANINHII(MZEE JONGO OO!)KUWA MFUPI WALA KUTOVAA HAKUREFUSHI KITU YOTE NI MBWEMBWE TU!

    ReplyDelete
  28. AnonymousJune 13, 2009

    SWALI LA KIZUSHI JUU YA SWALI:
    JAMANI MIE NAULIZA HILI ILA NAOMBA WALE WENYE UHAKIKA 100% NDIO WANIJIBU HILI KAMA HUNA UHAKIKA BASI BORA TU UCHUNIE!
    hivi nikweli kuna dawa ya kienyeshi inayo refusha mpini au ni wizi na utapeli wa waganga wa kienyeji? na kama ipo je inamadhara yeyote kwa nyie mlioshuhudia hilo?
    asanteni.

    ReplyDelete
  29. AnonymousJune 15, 2009

    Wewe Ann wa Tarehe June 13, 2009 12:22 AM,
    Dawa ya Kuongeza uerfu wa mpini ipo... leta kiganja cha albino nikupeleke kwa mganga akurefushi huo mpini wako, na hakuna madhara wa nini.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...