HABARI TOKA ZENJI ZINASEMA AJALI YA GARI IMETOKEA LEO MAJIRA YA SAA 11 JIONI HII MAENEO YA BUNGI, MIEMBE MINGI, WILAYA YA KATI MKOA WA KASKAZI UNGUJA AMBAPO WATU WAWILI WAMEPOTEZA MAISHA.
KWA MUJIBU WA KAMANDA WA POLISI MKOA WA KASKAZINI UNGUJA, AFANDE RASHID SEIF, GARI HILO LA ABIRIA LILIACHA NJIA BAADA YA TAIRI MOJA LA MBELE KUPASUKA NA GARI KUGONGA MWEMBE
KAMANDA RASHID SEIF AMESEMA MMOJA WA MAREHEMU AMETAMBULIWA KWA JINA LA MUSTAPHA MTAMBO (50) NA MWINGINE AMBAYE NI MWANAMKE BADO HAJATAMBULIWA.
AMESEMA JUMLA YA MAJERUHI 13 WAMELAZWA KWENYE HOSPITALI YA MNAZI MMOJA WAKIPATIWA MATIBABU, NA KWAMBA GARI HILO ILIKUWA NA ABIRIA WENGI WAKITOKEA HARUSINI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 09, 2009

    mwenyezi mungu awalaze mahala pema waliopoteza maisha na walioko hospital mwenyezimungu awape uhauweni.
    mdau coventry

    ReplyDelete
  2. Mwakitosi, TemekeJuly 10, 2009

    Huyu Kamanda Rashid Seif ni yule ajulikanaye kama "Saddam" ambaye aliwahi kuwa pale polisi Chang'mbe na baadae akahamishiwa Iringa kama OCD. Ni mchapa kazi hodari na hana chembechembe za ufisadi.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 10, 2009

    Inna lillaahi wainna ilayhi raajiun, mungu awalaze pema peponi marehemu na awape subira wafiwa.
    Jengine anko nanihii kwa marekebisho ya taarifa zijazo wilaya ya kati iko mkoa wa kusini na sio kaskazini unguja

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...