Unajua kuna kila sababu ya watukulalamikia serikali hapo kwetu bongo kwa mambo ambayo mara nyingiyanaweza kuepukwa ikiwa tu patakuwepo na uzalendo halisi kwa kusema hilini letu na siyo hili ni langu.
Ona, Tanzania ni nchi ambayo imekuwa mbelesana kwa mambo mengi ya kimaendeleo, lakini mara nyingi haya maendeleo huonekana kwa watu binafsi, Sina haja la kulisema sana hili maana linamifano lukuki na linaongelewa kial siku.
Tuyaache hayo na tuingie hapa kuona watani wa jadi walivyo mbele kwakuipamba nchi yao na sasa wanalenga 2010 ya SA! Ona walivyoingia ubia wa anga na Air Botswana na haya ndiyo matangazo.. (Business strategies kwa2010 .. hakuna zaidi ya hilo)
Sisi tuko wapi? ????
Tulishidana na SA Airways simply ya yale yale ya utajiribinafsi kwa hongo ndogo ndogo halafu mambo yanakwama.. Lini tutajikwamuahapa na u-mimi mimi huu!!!
Hivi vijembe vya watu kuongelea Ooh Mkuu wa nanihii anakwenda sana vekesheni... ooo nanihii ana duka la kuuzia vipodozi na mafuta ya kuongeza matiti na nanihii!!! si swala la kulivalia njuga mpaka Bungeni. Oooo John Mashaka na Dk. Shayo waandike kwa Kimatumbi.... (((Wapi na wapi)))
Hivi vijembe vya watu kuongelea Ooh Mkuu wa nanihii anakwenda sana vekesheni... ooo nanihii ana duka la kuuzia vipodozi na mafuta ya kuongeza matiti na nanihii!!! si swala la kulivalia njuga mpaka Bungeni. Oooo John Mashaka na Dk. Shayo waandike kwa Kimatumbi.... (((Wapi na wapi)))
Hivi kwa nini badala ya kujifanya wajuaji na wakosoaji wa kila jambo tusiongelee njia mbadala ya hizo unazioona hazifai, na pia tujenge utamaduni wa mashindano ya maendeleo kwa nchi nzima!!!!???????
Mdau dRU
Mdau dRU
yaani ukiwa huku UK utaona matangazo ya utalii ya nchi zote za africa likini Tanzania haionekani, naona kama wizara ta utalii ya tz haifanyi kazi hata kidogo, any kama kazi ipi? ningeona serikali iifutilie mbali kwani inakula tu pesa na hakuna la maana wanalolifanya! am glad am not a tanzanian anymore! holiday zangu ni mombasa nalipa pound 400 flight and 7 days accomodation kwa raha zake! with kenya airways. halafu nakuja TZ kusalimia ndugu and then narudi zangu mombasa I like it and its very cheap! tanzania very expensive! poleni
ReplyDeleteJamaa wanatupiga mabao kweli kweli angalia tangazo lao kwenye CNN na lile letu japokuwa tuna vitu vingi(TZ) lakini wenzetu na uchache wa vitu vyao, quality la tangazo letu ni aibu hii yote kwa sababu kama ulivyosema ubinafsi(10 %) na nchi itakuwa hivi hivi mpaka watu wabadilike kwenye akili na matumbo yao.
ReplyDeleteKwa kweli wewe Anon wa kwanza unanishangaza!! Huko UK unakaa sehemu gani? Umeshakwenda Victoria underground ukaona matangazo ya kuitangaza Tanzania, au huko barabarani hujakutana na taxi ambazo zina mabango yanayotangaza Tanzania? Wewe kama umeamua kuukana uraia wa Tanzania, huo ni uamuzi wako binafsi ulioufanya kwa hiari yako. Acha kukashfu nchi ambako ndiko ulikozaliwa. Unachotakiwa kufanya ni kutoa mawazo na mchango wako jinsi gani tunaweza kuitangaza nchi yetu hata kama umeshaukana uraia wa nchi hiyo! Usimtukane mkunga wakati uzazi bado ungalipo!!!!
ReplyDeleteNchi yetu, viongozi wake ni wepesi sana wa kuongea lakini kivitendo hakuna. Karibu kila kiongozi anawaza achote vipi kwa kipindi ambacho yuko madarakani. Haingii akilini nchi ina miaka karibu 50 tokea ijitawale na inachimba madini mbalimbali lakini wananchi wake karibu ni wa mwisho duniani kwa umaskini!!
ReplyDeleteDRU,
ReplyDeleteNimependa sana mtazamo wako nami nina mtazamo kama wako kuhusu jinsi watanzania na mpangilio wa mikakati yetu na mawazo yetu(mindset and priorities).Nchi inazidi kuwa ya madaraja hili linaonekana kwa viongozi pamoja na wananchi mojamoja hasa mijini, yaani mali na umimi vinaonekana kuwa ndiyo dili kuliko maendeleo ya dhati ya nchi na wananachi wake.Tusipozingatia hili tutakwama zaid katika dimbwi la umaskini. Tufike mahala katika blog ya jamii watu walio wengi wanachangia kuhusu namna tutakavyojikwamua sio mambo ya nani ana nina na anafanya nini(triviality).
Mungu ibariki Tanzania na wananchi wake.
OHL
Tutakaa kila siku kuwasema watani wetu wa Jadi, Ni kweli 2010 inakuja, World Cup hapa bondeni, tuna mipango gani????? Watani wetu wa Jadi wameishaanza kuadvertise na mipango unaiona. Kuna watu wengi wa nje watakaokuja kwa ajili ya World Cup, Wizara ya Utalii una mipango gani kuhakikisha tunatangaza rasilimali zetu za utalii kwa watu hao. Opportunity has come to us lakini hakuna hata knachoendelea. Kweli wabunge wetu jamani mnakaa Bungeni kuzungumzia dawa za kuongeza makalio, hips na mengineyo kweli?? Et sijui kuvaa mawigi, jamani give us a break, Yaani Bunge siku hizi limekuwa sehemu ya kupigia michapo. Amkeni wangunge, mawaziri, etc sisi wanachi wenu mnatukatisha tamaa. Kuna katuni moja ilichorwa na Kipanya anauliza hivi sisi Wanzania tumerogwa na nani???? It is very dissappointing!!
ReplyDeleteAnon July 31,11:26 am(wakwanza kutoa maoni hapo juu),bilashaka umechemsha kutoa maoni yakijinga kama hayo.Kwanza ndio nyie mliojiripua,pili huna uzalendo kabisa,Tatu,umekuwa mtumwa wa kisasa.Bilashaka huko ulipo unapiga boxi au unafanya kazi kwenye makampuni ya kuricycle au unakula benefit ya walipakodi bure,uoni aibu.Nakushangaa ulivyoukuwa mjinga na ideas zako.Hata ndugu zako watakuona unafikra finyu "eti mimi sio mtanzania tena" poleni,alaa.
ReplyDeletekwa taarifa yako,kulikuwa kunaeffort kutangaza Tanzania kwenye matube ingawa sio aggressive kama wengine.ni jitihada tuu,nenda chukua Hammersmith and city line tube utaona matangazo.umeniudhiiii!
Maongezi ya waliojilipua yani ni kupondea TZ kuanzia sunrise mpaka sunset, nipo UK najuta kuwafahamu waliojilipua waoneni tu na mitazamo yako kama anon wa kwanza ni shida tupu hapa natafuta nyumba nihame nikakae mbali hawana la maana kutwa kucha hodi wanavizia breakfast,lunch mpaka dinner. Mume wangu kawavumilia washkaji sasa na yeye amechoka tunahama soon
ReplyDeletewatu kibao tuko uk, nakubaliana na jamaa wa kwanza uk hamna matangazo ya TZ.
ReplyDeletenyinyi mnapewa hela mnaenda kuweka tangazo moja kwenye tube moja kwenye taxi moja kwenye bus halafu mnajipika picha wenyewe mkiwa mmesimama, alafu mnaweka kwenye internet na kusema tanzania inamatangazo kila kona
watanzania sio wajinga tena
Oh dear!! acheni kubishana sote ni ndugu hata yule aliyeukana uraia wake bado ni MTZ. uraia wa karatasi wala haiji. Tuungane tuzidi kuitangaza nchi yetu nami inaniuma sana.Huku UK wengi hawaijui Tanzania maana sio wote wanaoijua jiografia.Mpaka useme Tanzania ipo karibu na Kenya.Kimoja tu ninachojivunia ni amani. Mungu ibariki nchi yangu Tanzania.
ReplyDeleteDuuh kwakweli kila mmoja anazungumza kwa uchungu na nchi yake najua ni lazima upate uchungu kama unafuatilia kila tukio la maendeleo ya nchi yetu TANZANIA.naanza kuongea;
ReplyDelete1.Maendeleo ni nini?
-Hili ni tatizo kubwa sana kwa watanzania wengi kujua maendeleo tunayoyahitaji na kwa muda gani,nimefanikiwa kufika nchi mbalimbali wakiwa wanazungumzia maendeleo si leo na kesho tu hapana ni ya miaka kuanzia 5,10 na kuendelea na viongozi wanakuwa committed kiukweli si porojo kama tulizoziwea kwetu kama baba unapomuahidi mtoto ahadi hewa kila kukicha na hali akijua hutekelezi sasa hilo laja kwa viongozi wetu.
2.Watanzania tunapenda starehe,yap!hilo ni la kwanza kwetu na kuwajibika ndo kunafuata na hili linaanzia kwa viongozi maana ofisini humpati eti ana kazi za nje nyingi 'si lolote'ni starehe 10%follow up mnh unadhani utakuwa na maendeleo,NO.
3.Jamani tunahitaji maendeleo ya nchi kwa kiwango kikubwa na si 2010 pekee bali katika kila nyanja inayohusu maendeleo barabara,huduma za afya,maji,umeme,usafiri wa ndani ya nchi(ajali),jamani jamani tunaangamia na hii yote ni kwasababu nchi inanuka RUSHWA(WIZI) kila idara uuuuuwiiiiiii twafa.
Mwisho MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE.
Mdau Mac(US)
wadau
ReplyDeleteAkina shayo na Mashaka ni kajisehemu tu ya watanzania wenye kuwaeleza watanzania wenzao na hasa vijana hali na umuhimu wao katika kujenga taifa. Ukifuatilia sana makala zao ni za kuelimisha na kutoa fikra mpya.
Kuhusu kuitangaza tanzania UK ninafikiri hamjui undani wa kilichotokea kwa hiyo ningewaombeni mkae kimya.
Hela za serikali zililiwa na hata mpaka sasa swali lililoulizwa bungeni kuhusu hili sakata bado kupatiwa ufumbuzi.
matanango yalisemekana ni ya miezi tisa lakini mhuu... tunajua what happen
anzania iko kazi kweli kweli!
Dr Shayo na Mashaka nafikiri angalieni ni wapi umaweza kuuza akili zenu na siyo kurudi tanzania
100% Tanzania haiweze kuendelea endapo Mafisadi wapo kila kona ya nchi. Wanaotakiwa kuitangaza nchi ni viongozi ambao wako mstari wa mbele. Sasa viongozi wenyewe kama ndo kabati kuwa wa kuifadhi mafisadi unafikri hapa kweli Tanzania itasonga mbele? Juzi tu tumetoka kulalamika kuhusu FISADI INTERNATIONAL AIRPORT kuhusu wizi. Ili nchi iendelee inabidi wasafishe ufisadi kwanza. Tunajua kuwa watu tunaipenda sana nchi yetu, lakini ufisadi kwa viongozi too much.
ReplyDeleteMisaada inayotolewa kwa Tanzania kutoka nchi za nje, bila ufisadi kwa viongozi wenyewe wanaopokea misaada hii Tanzania tungekuwa mbali sana. Kiasi hata nyingine jirani wangelikuwa wanaona wivu fulani kimaendeleo. Lakini haya makabati ya mafisadi ndo chanzo cha nchi yetu kuendelea kudidimia kila siku iendayo kwa Mungu. Watu inabidi tujifunge buti tutembee hadi Ikulu. Hii misaada inayotolewa ni mingi sana kiasi kwamba hata Wanafunzi wanaoangaika na usafiri wa kwenda shuleni wangekuwa na SCHOOL BUS. Lakini ndo hivyo uongozi hakuna kabisa.
Mungu ibariki Tanzania na watu wake. Lakini Mafisadi wote tupilia mbali.
Mdau. USA
Kama huyo anon wa kwanza kaukana uraia wa TZ hayo ni maisha yake. Alichosema kuhusiana na mada hii ndio cha muhimu hayo mengine hayatuhusu kwani alivyotoka kwao sidhani kama alikuaga au hata utanufaika na lolote kutoka kwake kiuchumi.
ReplyDeleteCha msingi ni kwamba katika pita pita zako huko UK hajaona hayo matangazo yanayohusu TZ. Hii inawezekana kuwa matangazo yamewekwa sehemu chache sana au yeye hatembelei maeneo maarufu.
Kinachotakiwa ni kuongeza matangazo na sio kumsakama ooh kaukana uraia, kajilipua, mkae mkijua mwisho wa siku watu wengi sana wanaganga njaa na kama yeye anaona kama kujilipua itamsaidia katika kuganga njaa yake yote ni heri ilimradi hamuibii au amuombi mtu hela.
Mimi hivi karibuni nilikutana na mtu ambaye baada ya kujitambulia alinichangamkia sana kwa sababu natoka TZ. Alisema kuwa alikwenda TZ muda si mrefu lakini cha kushangaza aliingia TZ akitokea Kenya. Safari yake iliandaliwa kutokea Kenya wakati hajatumia hata robo ya muda wote aliokuwa safarini huko Kenya. Tukumbuke kuwa kunaubadhirifu sana wa mali ya serikali/Umma na mambo kama haya ya matangazo labda watu wamechukua nafasi kujenga nyumba nyingine kwani matangazo kama tujuavyo ghali sana. Waliopo UK wanaweza kutupa habari kama wanayaona haya matangazo katika maeneo tofauti tofauti.
Tutafakari mada iliyoletwa na sio vinginevyo.
habari za muda huu mjomba...!
ReplyDeletekwa kweli hii kitu kipo interested na mfano mzuri wa kuigwa lakini tatizo letu ni moja...
kusema kweli kwa sisi vijana ambao tupo nje ni miongoni mwa watu ambao tuna zorotesha taifa kwa mfano :
1.kijana wakitanzani ukifanya naye kazi kama humjui anajifanya sio mmbongo na atawatangazia watu kwamba hajui na wala hajai kusikia kuhusu tz
2 : hatuna utaratibu wa kutembelea sehemu za asili kama mbuga, milima ,na visiwa pamoja na sehemu muhimu za kitalii, kwa hiyo inakuwa tabu kuilezea au kumfahamisha mtu ni jinsi gani nchi yetu ilivyo., na hata mtu jiographia na hali joto ya nchi yake hajui sasa kaka hapo tupo pamoja kweli ?
3 : viongozi ndio namba moja hawatoi msaada wowote katika kuendeza secta hizo zaidi ya kuziteleza, mfano, amboni tanga,nyumba ya mungu,iringa, singida na hata bagamoyo, znz ndio kabisa hakuan lolote linalofanyika na hata hiyo garden ya uhuru ndio usiseme vimetupwa
Sisi ndio wazee wa Kalaghabaho wenyewe.
ReplyDeleteJuzi juzi shirika la ndege la Marekani liitwalo Delta lilikuwa na mpango wa kuanzisha safari za ndege kutoka US, kupitia Dakar na kwenda moja kwa moja Nairobi. Walifuta mpango huo kwa sababu ambazo sizikumbuki. Ile ilikuwa nafasi nzuri kwetu kuwaambia walete ndege zao Kilimanjaro International Airport. Tungeweza kuwavuta watalii zaidi kwa njia hiyo.
Tangazeni nchi yenu kwenye vyombo vya habari kadhaa siyo just kwenye ma Tube stations za UK.Kwanza UK imechacha ile mbaya ki uchumi. Halafu mkae mjue kwamba rushwa na usumbufu mwingi Kwenye point of entries zenu kunawakosesha abiria na watalii.Fungueni macho.
ReplyDeleteMbeba mabox kikongwe.
We anony wa kwanza yaaaani we acha tu,nisipate dhambi buree!eti sio Mtanzania tena?eti Vacation Mombasa?
ReplyDelete1.What r u doing in this blog?
2.Ndugu zako wameona hii post kweli?
3.Umefaidika nini na uraia wa Uingereza?
4.Wapi zamani tena?...ooh i thought so!
5.Kuna blog nyingi za akina aterere,jiunge huko....aha tena nimekumbuka,Naakaya naye yuko huko huko unakotua na ndege,you guys should hook up,since you are all foreigners now.chunga tu usivunje sheria za Bongo ukiwa huku,maana yake watakudepot Uingereza na waingereza watakunyanganya uraia,aafu sasa sijui watakudepot wapi?probably....mmmmm...NO IDEA!