Agnes Aaron Sabiti akishukuru Mungu kwa bahati ya kujinyakulia milioni 40 za Vodacom
Meneja Mauzo wa Vodacom Kanda ya Kaskazini, Bw. Henry Tzamburakis akimkabidhi mshindi hundi yake leo
Vodacom Tanzania kupitia programu yake ya Uaminifu ya Tuzo Droo Loyalty leo imekabidhi zawadi yake ya kwanza ya mwezi ya promosheni inayoendelea ya Tuzo Droo kwa 2009/10.

Mshindi wa Julai 2009, Bi. Agnes Aaron Sabiti anayetokea KIA –Kilimanjaro -, alikabidhiwa kitita chake cha Tsh 40m/- pale Vodashop Moshi.
Meneja Mauzo wa Vodacom Kanda ya Kaskazini, Bw. Henry Tzamburakis aliiwakilisha kampuni ya Vodacom kwenye sherehe hiyo ya kukabidhi zawadi.

Bi. Sabiti, alisindikizwa na familia yake pamoja na wanachama wa kanisani kwake, aliisifu Vodacom Tanzania kwa moyo wao wa kujali na kurudisha kile kidogo wanachokipata kutoka kwa wateja wao.

Aliwaomba wananchi kujiunga na kutumia mtandao wa Vodacom na aliwahakikishia watanzania kwamba Tuzo Droo hii ni huru nay a haki kwa wateja wote wa Vodacom.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 3 mpaka sasa

  1. JAMANI HUYU SI MDOGO WAKE KINJE AU?

    HILO JINA LAKE LA PILI LINAONEKANA KAMA SIO LA KIRAIA AU NDIO UZUNGU WENYEWE!!

    HIVI TANZANIA NANI RAIA HALISI!!

    ReplyDelete
  2. ndiyo huyo ni mdogo wake kinje

    ReplyDelete
  3. huyo siyo mdogo wake kinje huyo anaitwa henry george hilo jina la mbele sijui kalitoa wapi ila huyo jamaa ana undugu na kinje nadhani kwa upande wa mama huko ,jamaa mbabe sana huyu sijui kama siku hizi amepunguza utoto maana ngumi mkononi huyo anyway umri umeshaenda na majukumu pia naona sasa ametulia ,safi sana mkuu henry piga kazi mwana tusonge mbele

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...