Mgeni rasmi katika shughuli hii alikuwa Mheshimiwa Naibu Waziri wa ushirikiano Afrika mashariki,MOHAMED ABOUD.Ambae aliwakabidhi washindi zawadi zao,namba moja alipewa fedha taslim sh. laki sita, huku aliechukua nafasi ya pili akiondoka na kitita cha laki nne, na mshindi wa tatu sh, laki tatu, namba nne na tano walipewa sh laki moja na nusu.
warembo wote walipewa zawadi zao isipokuwa mrembo namba tano Emakulata Alphonce kutoka kagera alipatwa na mshtuko na kupoteza faham aliposomwa na jaji mkuu kwamba ameshika namba tano,hivyo hakuweza kufika mbele kwani alikuwa amepelekwa hosipitali ya rufaa bugando,tunamshukuru mungu kwani kwa sasa anaendelea vizuri.
Kwa picha zaidi naomba waingie
florasalon.blogspot.com.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...