Selamawit Zerabruck Ghebreslassie
Date of Birth 19-08-1991
Height 172
Hobbes reading, Traveling, movies
Sefora Messele Ghebreezgabiheir
Date of Birth 19-09-1991
Height 180
Hobbes swimming, reading

Eritrea imekuwa nchi ya kwanza kutangaza warembo wake katika mashindano ya kimataifa ya urwembo ya Miss East Africa mwaka huu yatayofanyika December 18, 2009 jijini Dar. Warembo hao walipatikana katika mashindano ya kuvutia ya urembo yaliyofanyika jijini Asmara Nchini humo hivi karibuni.

Warembo watakaoiwakilisha Eritrea katika mashindano ya mwaka huu ni
Selamawit Zerabruck Ghebreslassie na Mesele Ghebreezgabiheir.

Mwaka jana Nchi ya Eritrea pia ilikuwa ya kwanza kutangaza wawakilishi wake katika mashindano ya Miss East Africa 2008 yaliyofanyika jijini Bujumbura, Burundi ambapo iliwakilishwa na warembo Rahwa Ghebrehiwet pamoja ya Menal Hussien ambapo Rahwa Ghebrehiwet alifanikiwa kuibuka mshindi wa tatu.
Mashindano ya kimataifa ya urembo ya Miss East Africa huandaliwa na kampuni ya Rena Events Ltd ya jijini Dar.

Nchi 14 za ukanda wa Afrika mashariki tayari zimeshathibitisha kushiriki katika mashindano ya mwaka huu ambazo ni wenyeji Tanzania, Kenya, Uganda, Rwanda na Burundi, zingine ni Ethiopia, Eritrea, Djibouti, Somalia, visiwa vya Seychelles, Re union, Madagascar, Comoros na Mauritius.

Wakati huohuo ile bahati nasibu ya Miss East Africa ya kuchangia yatima ambapo mshindi wa kwanza atajishindia gari jipya aina ya Range Rover sport inaendelea na watu wote wameombwa kushiriki bahati nasibu hiyo.

“Tunawaomba watu wote washiriki kwa kuandika neno SHINDA kwa kutumia simu zao za mkononi na kutuma kwa sms kwenda namba 15567 ili waweze kujishindia zawadi mbalimbali na wakati huohuo wakichangia yatima wa Tanzania na Afrika mashariki kwa ujumla”
Imeandaliwa na kusainiwa na

Rena Callist,
CHAIRMAN,
MISS EAST AFRICA BEAUTY PAGEANT.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 23 mpaka sasa

  1. Kwa hali hiyo tunayoiona Tanzania nafasi yake ni ndogo hizo toto zinakila kitu naturali sasa kina dada zetu wanakazi pevu la si hivyo mkatafute warembo watakaoweza kukompiti na wasichana kama hao kwani uzuri wao ni wakuzaliwa ukweli unauma lakini hiyo ndiyo hali halisi

    ReplyDelete
  2. Jamani Hao Warembo aminia.

    Sina la zaidi.

    ReplyDelete
  3. Du! Mzee mzima mi naona hapo tusha pigwa bao la kisigino tayari, manake hapo kuna 8/10 na 10/10 sasa sisi sijui tuta score point ngapi, kwa ushauri wangu hiyo tabia ya warembo wa nyumbani kunyoa vipara wasitumie kama vigezo kwani nywele za mwanamke huongezea urembo kwa kiasi kikubwa. Nawasilisha!!!

    ReplyDelete
  4. Kwa mwendo huo sie twende tukashiriki tu, hakuna kushindana hapo!

    ReplyDelete
  5. Duh totoz kali sana,halafu bado mbichi sana,18yrs,warembo wa TZ wengi wa bongo wazee,bt uzoefu unaonyesha madem wazuri sana kwa sura -kichwani zero,division zero nyingi ni mademu wakali-coz wanadatishwa na men,may warembo wetu watashinda kwa brain(Q&A session)

    ReplyDelete
  6. Wabongo acheni unyonge na kujiweka nyuma. Kwani mnadhani ni urembo wa sura na maumbile tu ndivyo vinavyomfanya mtu ashinde?

    Kama ingekuwa hivyo, basi ni wachahche wangekuwa wanashinda. Kuna mambo mengi yanayoagaliwa kwenye mashindano, hosusani IQ ya washiriki.
    IQ ni moja ya vigezo muhimu sana kwenye haya mashindano.
    Endeeleeni kujiweka nyuma mtaona matokeo yake, Jumuiya ndio hiyo inakuja.
    Msipoweza kushikama, mtashika mkia.

    ReplyDelete
  7. watoto waha mi sisemi maana da wako juu mpaka mtu unapata presha. yaani utasema wanaoga na maziwa du.bongo tulietu. hamna mkorogo wala ma weaving ya ajabu ajabu jameni.ila hawa wanashindwaga kwenye kujieleza tu.ila kwa appearance wako juu

    ReplyDelete
  8. Duh! Watoto wazuri sana, utafikiri hawaendi chooni!!

    ReplyDelete
  9. bhagosha! hizi picha za ukweli ama 'zimefisadiwa' kidogo?. bhajama!

    ReplyDelete
  10. HAKUNA LOLOTE MNATISHIKA TU, HAWA TUNAO WENGI TU HAPA A-TAUN, NIPATIE UWAKALA NITAKUSHUSHIA WENGI KWA RAHA ZAKO KAKA

    ReplyDelete
  11. Anony 8;32 Kama IQ ni muhimu sana peleka kitu kama LADY JAY DEE AU LWIZA MBUTU halafu tuone kama watashinda kubali matokeo watoto hao watamu.

    ReplyDelete
  12. Duh! Kaka!
    Huyo kwenye picha ya kwanza huyo! Duh!

    Jamani mi mwenzenu humu ndio nitakamokufia humu.

    We Massaiboi nikupe e mail yangu unipe jinsi ya kuwapata hao huko Arusha?

    ReplyDelete
  13. Huko kwao kuna kwenda shule kweli? Watoto hata hawajaturn 18 wanaingizwa kwenye mashindano jamani? POVETY

    Huyo moja ndo ameingia tu 18 huyo mwingine ndio bado lakini kesha ingizwa kwenye haya mamiss du ...LIFE

    ReplyDelete
  14. Hapo tumepigwa bao 3-0! kama TMK vilee!!!

    ReplyDelete
  15. totozi utafikiri zimeshushwa Kina dada Tafadhalini msije mkaweka makatani ya kichwani mtakuja kuadhirika ni vyema mkasuka misuko ya kienyeji kuvutia majaji lakini ikiwa mtajidai kuwaiga wazungu mlala pakavu kwani hizo toto zina nyele za kuzaliwa nazo rangi si za kubuni nakuombeeni ushindi lakini nahisi upo mbali sana

    ReplyDelete
  16. Wanaume wa kibongo tatizo hawajielewi wakati mwingine. Wanasifia hao watoto sawa ni wazuri natural lakini wakumbuke hao wanamchanganyiko wa damu nyeupe. Hao ni Chotara kwa hapa kwetu tunaita hivyo. Angalia kama huyo wa kwanza yupo kama anaasili yakisomali. Mkumbuke kuwa Chotara mara nyingi wanakuwa wazuri.

    Sasa nyinyi mnapowaponda Warembo wenu wakitanzania ni kuwa mnaziponda asili zenu. Kama ndio hivyo basi wanaume woote wakibongo oeni machotara ili mpate watoto wa namna hiyo.

    Asili ya Mtanzania asilia ambaye hajachanganya lazima nywele zinakuwa ngumuu na nyusi pia sio laini, kope sio ndefu. Nyie hamuoni hao jinsi walivyo wana damu nyeupe Nywele zao, nyusi, kope?

    Jipendeni wenyewe, kubalini asili yenu, kwanza wewe mwenyewe mwanaume unaewasifia hao na kuwaponda wenzenu utakuta nywele hizo zako ni ngumuu umeweka pengine dawa ndio zikaonekana laini huna uzuri wa asilia.

    Na katika watanzania ni kuwa akishiriki Chotara akishinda mnalalamika mnadai kuwa sio Mtanzania mfano Miss aliyepita mlichonga hadi basi. Kama ni chotara wazuri bongo wapo kibao hawashiriki tuu sababu ya kuogopa kupondwa lakini wangeshiriki mngeona walivyo bomba.

    Watanzania Tuelimike. Tujipende wenyewe, Tujiamini, Mtu ajiamini alivyo kuwa ni mzuri, Tusijirudishe nyuma, Tupende uasili wetu. Kama nywele ngumu ni asili yetu jamani na wao wana asili yao.

    ReplyDelete
  17. Babuee mujue mtanzania ana uzuri wake na hao wanauzuri wao. Kisa nywele, pua, rangi ndio mtuponde? Hiyo ndiyo asili yetu, ukitaka kutuponda jinsi tulivyo kwanza jiangalie wewe, kisha umuangalia dada yako kama wewe ni mtanzania, au muangalie mdogo wako ndipo uponde wengine kuwa wanamanywele kama makatani. Sababu siamini kama mtanzania asilia, yani yule mbantu asilia ananywele nzuri, zooote zinakuwa kipilipili, pua inakuwa flat pia wakati mwingine.

    Sisi tuna uzuri wetu unaovutia na wao wanauzuri wao. Pengine wao maumbo kama wamepigwa na mwiko nyuma. Kiuno hakuna. Kisa sura ndio imekuchanganya? Angalia kila mahali.

    Hivyo wewe anon Tarehe Thu Sep 03, 12:45:00 AM,. Usirudie tena usirudie kabisa. Au wewe sio mbantu asilia????

    ReplyDelete
  18. Eti IQ umesikia haya ni mashindano ya kutafuta msichana intelligent ama..watu wengine vipi???of course inabidi kichwani mtu awe nazo lakini kigezi nambari one ni sura na uportable bau .usilete za kuleta.watoto wako juu hawa.rangi asilia sio za dukani.nywele ndo usiseme yaani I'm speechless

    ReplyDelete
  19. Wewe Mzalendo usilete POLITICS kwenye urembo, kwa ufupi hao mademu ni wakali mno!!

    ReplyDelete
  20. uuwii we anon 11:13 mbavu zangu zinauma mifano hai mingine kiboko lol!! hao mabinti ni wazuri saana hata msemeje ni wakali kuna machotara wangapi wako kawaida kabisaa tena ugly flani ni mambo ya bone structure ndo yanachangia kwa asilimia kubwa mtu aonekane bomba watu wanajikorogaaa wanakuwa weupe na bado sura zao nzito kama kawa kama we sio beautiful hata ulie ndo uko hivyo labda upige surgery ya nguvu uchonge mifupa ikae vyema na kuhusu majaliwa wo wo wo hayo ni majaaliwa sura mama sura ndo inaanza kwani makalio ndo uzuri? mtajiju kama una sura nzito mnalo kama si lako la jirani yako
    miss michuzi

    ReplyDelete
  21. annoy hapo juu umenichekesha.you made ma day...watu wabishi hawa watoto ni bomba haswa.and nyie mnaoleta ubishi hakuna aliyesema kuwa watanzania sio wazuri ila kwa wale tunaowekewaga eti wanawania beauty peagant hawakaribii hawa watoto hata kwa dawa.
    nasema kama mdau hapo juu wewe mzalendo usilete politics kwa kifupi hao mademu ni wakali mno

    ReplyDelete
  22. annoy sept 3 9:42 hawa watoto hata wawe wamepigwa pasi na miguu kama skoku za baiskel bwana msema kweli mpenzi wa Mungu hawa mademu wako bomba. hata aje demu mwenye shepu ya namna gani hizi hawezi shindana na hizi reception.zina mvuto wa pekee.
    shepu..shepu kitu gani?siku hivi jeans zinasaidia sana.
    no ubishi vibinti virembo sana tena sana

    ReplyDelete
  23. hahahahaaaa oyoyoyyyyooo hahahaaa

    miss michuzi vp?unataka tulazwe mapema mapema hahaaaa

    jeans zinasaidieje mdau?hahahaaaa

    ama kweli izi box zitawehusha watu umu bloguni/globuni

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...