FAMILIA YA ASHURA KASHEBA WA LONDON, TUNAPENDA KUMKUMBUKA MPENDWA WETU BABA YETU KIPENZI NDALA KASHEBA TOKA AIAGE DUNIA 22 OCT 2004 LEO HII AMETIMIZA MIAKA 5 KAMILI.


UCHESHI, UPENDO NA UKARIMU WAKO KATU HAUTASAULIKA ,MAWAZO NA USHAURI WAKO UTABAKI MIOYONI MWETU. UKO KWENYE MAOMBI YETU KILA SIKU NA TUNAKUMBUKA YOTE ULIYOYAFANYA KATIKA MAISH
UMEBAKI KUWA KUMBUKUMBU KUBWA SANA KWETU JAPOKUWA SIKU ULIPOTUTOKA ILIKUWA SIKU YA MAJONZI MAKUBWA SANA KWETU.

TUNAMSHUKURU MUNGU KWA KUTUPA UJASIRI MKUBWA WA KUELEWA KUWA KIPENZI CHETU UMETUTOKA.

SISI TULIKUPENDA LAKINI MWENYEZI MUNGU ALIKUPENDA ZAIDI,UKAE KATIKA AMANI MPAKA HAPO MWENYEZI MUNGU ATAKAPOTUKUTANISHA TENA INSHALLAH.

FAMILIA YOTE,WATOTO WAKO WOTE, NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI TUNAKUOMBEA MAPUMZIKO MEMA. MWENYEZI MUNGU AIWEKE MAHALA PEMA PEPONI ROHO YAKE PAMOJA NA NDUGU WOTE WALIOKWISHA TUTANGULIA MBELE ZA HAKI.

AMIN.

WAKO MPENDWA MKEO
ASHURA KASHEBA
LONDON
KWA KUMBUKUMBU ZILIZPITA ZA KASHEBA
BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Mama Ashura Kasheba pamoja na familia yako nipo pamoja nanyi katika kumkumbuka gwiji huyo wa muziki hapa nchini, mafundisho mengi ametuachia kupitia katika kazi zake nyingi na nzuri za muziki alizozinakshi barabara kutumia 'kombora' lake la nyuzi dozen!! RIP Supreme Freddy Ndala Kasheba - Ben

    ReplyDelete
  2. RIP shemeji yangu!

    Muddy

    ReplyDelete
  3. Ah muyoomba RIP

    ReplyDelete
  4. RIP Maestro, tunakukumbuka. Kweli ulikuwa umebarikiwa na kipaji cha hali ya juu

    ReplyDelete
  5. NAKUMBUKA SIKU YANGU YA MWISHO KUMUONA GWIJI LA MUZIKI NI PALE LION CLUB SINZA.SIKUJUA KAMA GWIJI AMEFARIKA HADI LEO NASOMA HII HABARI pumziko la milele gwiji,POLE SANA ASHULA,NA TUKO WOTE.SEMA NAPENDA PIA KUTUMIA NAFASI HII KUKUULIZA MDOGO WAKO WASTARA YUPO WAPI..?Pls mpe mail yangu...pachino8569@yahoo.com
    mdau uk.

    ReplyDelete
  6. Uendelee kupumzika kwa amani. Utuombee nasi tuliobaki huku duniani. RIP Ndala!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...