Mbunge wa Urambo Mashariki na Spika wa Bunge Mhe. Samuel Sitta akijaribu moja ya treka za mkono alizokabidhi leo Jimboni kwake kwa ajiri ya maendeleo. ya jimbo lake. Mhe. Sitta amekabidhi jumla ya trekta 12 zenye, thamani ya Million Mia moja ikiwa ni ufadhili toka Denmark ambapo kila kata inayounda jimbo la Urambo Mashariki imepata treka moja. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge
Matreka ya Mkono yakiwa katika msururu baada ya Mbunge wa Urambo Mashariki na Spika wa Urambo kukabidhi trekta hizo 12 kwa vikundi vya wajasiriamali jimboni kwake kwa kila kata ya Urambo Masahariki wanaojishughulishja na kilimoikiwa ni mkakati wa kutekeleza kauli ya Kilimo kwanza jimboni Kwake. Matreka hayo yanajumla ya thamani ya shillingi Million Miamoja ikiwa ni ufadhili toka Denmark. Picha na Owen Mwandumbya wa Bunge


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. wajomba wameanza kuandaa gia ya kuomba kura

    ReplyDelete
  2. Akumbuke na umeme pia. Maana hiyo wilaya haina gridi ya taifa. Umeme ni wa genereta na linawashwa kwa masaa jioni na kuzimwa kabla ya alfajiri.

    ReplyDelete
  3. Washa umeme kwanza

    ReplyDelete
  4. Mheshimiwa sixx, yohanna mashaka alikushauri kwamba, Kama kweli unaipenda Tanzania, basi wakamate mafisadi kwanza Kisha uwashe umeme hapo tutajua kweli unaipenda Tanzania. Vinginevyo hivi ni viini macho vya kampeni vya 2010

    ReplyDelete
  5. Hizo hela za kuyanunua hayo matrekta katoa wapi? Wizi mtupu!!!!!

    ReplyDelete
  6. Maoni mengine tuliyoyaandika umeyaweka kapuni sio kwani yanagusa ukweli, huo sio uzalendo Bro Mithupu ni ubaguzi wa demokrasia, nimekumind kwa kutotoa maoni yangu ya awali, kama unaona yana ukweli zaidi edit basi na uandike utakavyowapendeza na kuwafurahisha viongozi wetu!

    ReplyDelete
  7. Wabongo wenzangu:Kabla ya kufungua kinywa kutema uchafu, angalau soma kilichoandikwa. We anony wa 12;42 huoni kuwa imeandikwa kuwa huo ni "UFADHILI TOKA DENMARK"? au kimatumbi hujui?
    Swala langu ni kwamba, unatumiaje ujiko wako wa kitaifa kuomba misaada nje na halafu kuigawa jimboni kwako ili kujipatia kura? Not fair kwa sie wenye wabunge waliolala.
    Blackmpingo

    ReplyDelete
  8. nachukia sana hii tabia asa kipindi iki

    ila jehanamu ni kiukweli kabisaa na watu watadondokea uko

    &&**":@#A:"|\< zao sana basi tu apa michu angeipiga teke ujumbe huu ningemwaga upupu umu leo kwa hii tabia

    ok

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...