"Babu Kaju" performed by Alex Kajumulo and Original Sound. Recorded live at Judkins Park on July 4, 2009.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 20 mpaka sasa

  1. Habari ya Kajumulo World Soccer imeishia wapi?

    ReplyDelete
  2. KUNA WATU YANI WANAISHI MAISHI YAO KIUTANI UTANI!! LINI HUYU JAMAA ATAKUWA SERIOUS!!

    ReplyDelete
  3. Kaju babu K wape vidonge vyao KAJU KAJU KAJU KAJU
    WASA WASA WASA hahahahaha nami nakuam,bia
    KWASIIIA LAKWA.

    ReplyDelete
  4. they are really having fun, that's the most important thing in life.

    what else do you people want?

    ReplyDelete
  5. Hehehehehehe Babu Kajuuuu namna gani tena? Band utadhani Buguruni Jazz Band . damn kulikoni tena naona mpaka vidonge unawapa wakitema shauri yao.ule mpango wako wa kujenga Uwanja wa Michezo wa Kimataifa bongo upo wapi ?.
    mdau UK.

    ReplyDelete
  6. najua kesho hapa maoni ya kumwaga.haya wabeba box kazi kwetu na anabahati sana hii ingekua ijumaa tumeshatoka kubeba box sasa tupo home kesho hakuna kazi wewe

    ReplyDelete
  7. Ingekuwa ni timu ya mpira wa miguu basi ingekuwa Lipuli ya Iringa yaani imeshuka daraja...kweli Babu kaju kadata!!

    ReplyDelete
  8. ha ha ha ha ha teh teh teh teh heheeeeeh! dah leo nimecheka sana hadi mbavu zinauma sasa. Huyu jamaa kweli Kamanda nimempenda sana afer this one here. Nakumbuka Mtaalam huyu aliwahi kuja Dar na Mavumba ya kufa mtu akainunua Sigara SC ikawa kama Chelsea ya bongo vile, Akamuajiri Julio na akaipeleka timu Camp Brazil Mwezi mzima, Jamaa alikuwa na mavumba si ya kitoto na Jina lake lilivuma kitaani si mchezo, pia kukawa kunaingizwa Jeans toka Hapa US zikiwa na nembo ya Kajumulo. Akaaihidi kujenga uwanja wa kimataifa. baadae akaiuza timu kwa merey balabuuu wa moro na ikaanza kuitwa moro united. Akala kona. kaibukia kwenye music industry, safi sana babu kaju wanaume ndo tunatakiwa hivyo, you fight till you can't fight no more, while tyrin' to have as much fun as this in the process.
    Duh Michuzi na wewe basi, manake juzikati tu hapa kuna mdau alipost kuulizia the where abouts of this Kamanda Kaju, and one commenter had it (correctly) that Kaju's now involved with one music band here in the states, lakini akaibuka mdau mwingine akapinga na kudai kaju hapigi musiki bali box tu la kivyakevyake, kaka michu umeona isiwe tabu umeamua kuweka hii hapa. naamini vyombo vya habari hasa udaku vitaidaka hii na kurusha magazetini mwao mana kamanda huyu alikuwa mtu baab kubwa, hakuwa pedesheee kama vipesheee uchwara vya bongo yeye alikuwa rich man of his time.
    mdau wa pajazzz

    ReplyDelete
  9. Michu, hebu wape watu utamu huu kutoka gerezani. Yaani wafungwa wapo siriasi kuliko dully na Ray C.
    http://www.youtube.com/watch?v=mKtdTJP_GUI&feature=player_embedded

    ReplyDelete
  10. babu kaju kadata,yaani full mizuka.
    Jamaa kamanda

    ReplyDelete
  11. NIMECHEKA HADI KARIBU NIFE, MAISHA JAMANI NI TABU, MUNGU ALITUPIGA KOFI WATU WA DUNIA YA TATU NDO MAANA TUNAANGAIKA SANA. NILISEMA HUMU KAJUMULO ANAJIBURUDISHAGA NA MUSIC WATU WAKABISHA. SI HUYO HAPO ANA WEBSITE YAKE PIANYI GOOGLE MTAPATA HISTORIA YAKE ALIVYOZUNGUKA DUNIA HADI AKAFIKA HAPO.

    ReplyDelete
  12. NAMKUBALI HUYU KAJUMULO.HUYU NI MWANAUME.UTAKIWI KUONA AIBU.HATA MIMI KAJUMULO NIPO MBIONI KUJIUNGA NA BENDI YA MUSIC HAPA USA.KAZI ZIMEKUWA NGUMU SI NIANGALIE UPANDE WA PILI TU.SONGA MBELE
    TUUUUUUUUUUUUUU.

    ReplyDelete
  13. he he heee wabongo nuksi kwa kusakunyua ishu za watu acha tu nimejichekea kweli mh sina hamu

    ReplyDelete
  14. Lakini anayejua ukweli atu habarishe kidogo kwani kimemtokea nini babu kaju? si huyu aliyekuwa akitembea na wapambe kulia na kushoto? au alipata matatizo ya kuibiwa kila kitu? au anapiga muziki kwa kujifurahisha? hata hivyo nampongeza kwa kipaji cha hari ya juu!

    ReplyDelete
  15. Du huyu kamanda si mchezo!

    ReplyDelete
  16. Kaju kiboko, na iwe lakini lazima maisha yaende, sasa hao wazungu wanaelewa wanachofanya au wanaendeshwa? Kaju wewe mwisho.
    Bongo wanakusubiri uje kuwadatisha na bendi yako

    ReplyDelete
  17. jamani Wadau wote naona hamjaelewa kuhusu Kajumulo hapo hiyo Bend kaianzisha fani tu haina maana kwamba amepigika kifedha hiyo ni kama alivyojaribu na timu ya sigara ilikuwa ni fan tu mambombo ya jamaa bado yako mswano sana tu ndio maana kawavalisha hao wazungu t shirt zenye jina lake yeye anachokitafuta sasa ni umaharufu tu na sio mshiko.

    ReplyDelete
  18. Hapa nimekumbuka hadithi ya babu yangu alokuwa akinisimulia ya kwamba ati"mungu aliwaita wanaewaende kwake mapeema sana asubuhi, mwafrika,mzungu, mwarabu na mhindi kila mmoja achukue urithi wake, mwafrika alichelewa kuamka, kaanza kujivuta wee, kushika nyeti na hiki na hiki hadi saa 6 mchana ndo akaenda kwa baba mungu!!!! alipofika akakuta wenzie weshachukua mali zote na ikiwa ni pamoja na akili alochagua mzungu, kilichobaki ni ngoma tu, basi akaichukua ndo maana hadi leo sisi ni wacheza ngoma tu" kama jamaa anvyoonekana hapo. Mhindi na mwarabu walichukua biashara.

    Kwa kweli ngoma tunajua kuzipiga.

    Mpg bx

    ReplyDelete
  19. Hovyoooo, kama mchuzi wa jogoo! Wee waibie wazungu Bongo usingepata wa kukusikiliza##1

    ReplyDelete
  20. Hao sijui wamekula hela ngapi , baada ya backup singer kusema kajumuloooo
    kuanzia dakika 1.27 check anavyotoa pozi za kupiga ngoma . yaani balaa tupu

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...