DJ RICHIE WA BONGO DJs

TAARIFA KWAMBA NDUGU YETU MPENDWA ALMAARUFU KAMA DJ RICHIE WA BONGO DJ'S AMETUTOKA USIKU WA TAREHE 23 JANUARI 2010 KWA PRESSURE YA GHAFLA SI ZA KWELI, GLOBU YA JAMII IMETHIBITISHA.

HABARI HIZO, AMBAZO ZIMESAMBAZWA KILA MAHALI KWA NJIA YA SIMU NA MITANDAO, ZIMEKANUSHWA VIKALI SASA HIVI NA DJ RICHIE MWENYEWE BAADA YA GLOBU YA JAMII KUFANYA UTAFITI WA KINA KABLA YA KUZICHAPISHA.

"DAH! KAKA WALA SI KWELI KUWA MIMI NIMEKUFA, NA SIJUI NI NANI AMESAMBAZA HABARI HIZO ZA UZUSHI NA KWA SABABU IPI.
IMENISIKITISHA SANA KWANI NIMEPOKEA ZAIDI YA SIMU 200 TOKA KILA KONA YA DUNIA KUULIZIWA."NINACHOWEZA KUSEMA NI KWAMBA MIMI NAMWACHIA MUNGU ILA NASHUKURU KWAMBA NIKO SALAMA NA NINA AFYA NJEMA KABISA. PIA NAWATAKIA POLE NDUGU, JAMAA NA MARAFIKI WALIOPATWA NA USUMBUFU BAADA YA KUSIKIA HABARI HIZI ZA UWONGO.


"NINA WASIWASI KUNA MTU AMA WATU WANAOTAKA KUHUJUMU ONESHO LETU BONGO DJs WIKIENDI IJAYO AMPABO MIPANGO YOTE IKO SAWA NA ALI KIBA AMEKWISHATUA UK TAYARI KWA ONESHO HILO", ALISEMA DJ RICHIE KWA MASIKITIKO MAKUBWA ALIPOONGEA NASI KWA NJIA YA SIMU.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Gachucha,Dallas TexasJanuary 24, 2010

    Kama sijakosea ndugu zangu haya ndio mambo yanayovuka mipaka kama vile binadamu.Kifo ni hitimisho ya maisha yetu katika ulimwengu wa kimwili na mwanzo wa kimaisha ya kiroho.Kifo ni taarifa ambazo kila mmoja wetu zitamgusa kwa namna moja au nyingine kulingana na mahusiano ridhawa na mlengwa.Kwa kweli inavunja moyo saaana kuona jinsi tulivyokosa maadili ya kijamii na kuvuka mipaka inayokiuka haki ya mtu kuishi.Kumzushia mtu kifo kwa sababu binafsi(labda chuki au wivu hasa wa kimaendeleo)ni upungufu wa kutumia busara za kibinadamu.Binadamu saa nyingine huombeana mabaya lakini siyo kifo asilani!.Ukiona mwenzako anafanikwa kimaisha usimchukie ila mvute karibu akupe siri ya mafaniko!!.

    ReplyDelete
  2. damn haters get something to do with your life loosers
    pole Richie,we got ya back
    pamoja kaka
    mdau Slough

    ReplyDelete
  3. DJ Richie utaishi maisha marefu. Pole sana lakini. Nadhani umekosa usingizi baada ya kusikia habari hizi!

    ReplyDelete
  4. Ndugu yetu Richie mungu akujaalie maisha marefu! Hao wazushi ni wivu tu. Tupo pamoja siku zote...BF BOYS FOREVER!!!!!

    ReplyDelete
  5. Mzee pole sana, wabongo nuksi. Isaac Mgwassa

    ReplyDelete
  6. Babu Richie watu wa Flats nini wamekuzushia.....au akina Shulwa nini?

    ReplyDelete
  7. duh wabongo noma, yani mnamzushia mwenzenu kufa kisa wivu wa show ya ali kiba?

    ReplyDelete
  8. Brother Richie pole sana .... Mungu atakujalia kuwa na maisha marefu zaidi ..inasikitisha kuwa watu wana wivu wa kijinga just for the Ali KIBA's Show . Hawajui kuwa u DJ hukuanzia hapo UK nakumbuka tangu miaka ile ya early 90's ulikuwa unachakarika kinoma i.e BF Boys parties chini ya kina Libe , Kaburu na Michael Jackson wetu bob Zeno. Keep it up bro .
    NB ... inasikitisha mdau aliyemusisha Shulwa na habari hizi ... kijana wa watu hana hili wala lile ..chakula tu ni shida sasa hizi propaganda ataanzia wapi ..

    Musa
    Osaka ,Japan

    ReplyDelete
  9. DJ Richie, pole sana.

    Ukifanya kazi ya jamii kwa moyo wako wote, ifanye kwa nguvu zako zote...haya maneno maneno ni ya "marafiki" wanayoihusudu kazi yako nzuri na hawawezi kubuni wala kuboresha za kwao.

    Vita ya maisha hupiganwa mpaka pumzi ya mwisho.Hakuna kilio cha upendeleo ktk mapinduzi ya kweli.

    Adui wako akikusifia basi tafakari kwa makini kazi hiyo unayoifanya.

    Matusi, Uongo,Fitina,Husuda na Uzembe ni Ufisadi vile vile. Endeleza 'MAKAMUZI', Usiogope MALIMWENGU kaka, lazima tuishi nayo ili tuboreshe WAJIBU wetu.

    J'mosi kwa ALI KIBA mie tiketi yangu namba 1. Kamua sauti za kizalendo.

    Maina A Owino.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...