Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Bw. Martins Ovberedjo akimkabidhi ufunguo wa gari Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii Dkt Aisha Kigoda leo jijini Dar es salaam. WHO imetoa magari 25 kusaidia mpango wa kuboresha afya ya mama na mtoto na pia kupunguza vifo vya wanawake na watoto walio chini ya umri wa miaka mitano nchini.
Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii Prof. David Mwakyusa akiongea na waandishi wa Habari (hawapo pichani) leo jijini Dar es salaam wakati wa hafla fupi ya Shirika la Afya Duniani (WHO) kukabidhi magari 25 yaliyogharimu fedha za kitanzania zaidi ya shilingi milioni 986 kusaidia mpango wa Afya ya mama na mtoto nchini.

Mwakilishi wa Shirika la Afya Duniani (WHO) nchini Bw. Martins Ovberedjo akimkabidhi nyaraka mbalimbali za magari yaliyotolewa leo na Shirika la Afya Duniani kusaidia mpango wa Afya ya mama na mtoto na pia juhudi za kupunguza vifo vya watoto walio chini ya umri wa miaka 5 nchini. Picha na Aaron Msigwa - Maelezo



Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. I hope hayo magari yatafikia tageted people...wamama na watoto....mhhhh kesho utayaona yapo mitaani tu yamepark kwenye mabaa na hotel majira ya jioni...

    Ndio kama haiti watu wanauliza hela zinazokwenda kwa misaada kila siku zinaishia wapi?????? Raisi wao kajificha kimya anaona aibu nchi imeanguka vijumba vilijengwa cjui na cement ya udongo wa mfinyanzi....

    Mafisadi wana siku yao

    ReplyDelete
  2. mgosi wa kayaJanuary 15, 2010

    Naungana na mdau wa kwanza hapo juu kwamba ni matumaini yetu huo msaada utawafikia walengwa na magari yatatunzwa vizuri siokama tulichokiona miaka ya nyuma ambapo Nissan Patrol za jeshi karibia 250 ziliyeyuka na wala hazijulikani huko ziliko.Kwa hiyo wakati tukielekea uchaguzi mkuu nafikiri hayatatumika kwenye kampeni maana hao mawaziri wanaweza kusema wao ndio wameyatoa msaada

    ReplyDelete
  3. Wewe Anon wa Jan 15, 10:36:00 PM. Hebu acha hizo. Kwani hata wakiyatumia kugawia masanduku ya kupigia kura tatizo ni nini. Au hata yakitumika kama official cars za Waziri, Katibu Mkuu au Regional Medical Officer shida yako ni nini? Hujui uongozi unatakiwa kuwa wabunifu. Unamsema Rais kajificha? Ulitaka afanye nini ili umuone. Aah hebu acha hizo.

    ReplyDelete
  4. Nomba kuuliza haya magari yamenunuliwa na pesa za Tanzania zaidi ya shilingi milioni 986 au yametolewa kama msaada na WHO???

    anyway.. magari ndio haya yamepatikana, sasa ndugu zangu yatatumika kweli kusaidia mipango ya afya ya wakinamama na watoto???? yatakwenda mikoani na vijijini?? yatakwenda kuwasaidia wakinamama waliojifungua ili waweza kwenda kwenye vituo vya afya? yatatumika kuwapelekea misaada ya afya hawa wakina mama na watoto wao huko mikoani na vijijini? yatawasaidia wahuguzi iliwaweze kutoa hizi huduma?

    je na huyu Naibu Waziri wa Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii aliyekabindiwa ufunguo wa gari lake, kwani na yeye yuko kwenye FRONT LINE katika kutoa huduma za afya zinazohitajika huko mitaani? au Hilo gari ni lakwenda ofisini tu? kama ni lakwenda ofisini tu, kwani inamaana alikuwa hana gari kabla ya hapo? kwani magari yenyewe ni 25 tu, na nchi ni kuuuubwaaaa.
    Haya michuzi kaka, mie nauliza tu haya maswali kwa uchungu mkubwa kwani nina wasiwasi na jinsi gani hayo magari yatatumika......

    ReplyDelete
  5. Huyu waziri sio fisadi na ni mchapa kazi mzuri. I believe hayo magari are in good hands.

    ReplyDelete
  6. WADAU
    magari haya ni vitendea kazi ambavyo vinatumika katika uboreshaji wa huduma za afya.....si kwa ajili ya kupeki kwenye mabaa.....yametolewa na WHO

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...