hakuna madereva wakorofi, wajuaji na wababe kama wa dala dala jijini dar. huyu hapo yuko pande sio wake akaanza kuleta utemi katika njia panda ya magomeni makuti akitokea mwenge. mbabe mwenzie alishuka na kumkwida kabla ya kumpa vibao

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 10 mpaka sasa

  1. Haya mambo ya kupeana vibao, si tulisema hayafai? Angemu-Swetu ingekuwaje?

    Tatizo ni polisi/sheria kuto kuwa na utashi/vipengele vya kutokomeza tatizo la madereva wakorofi. Nyang'anya leseni na fungia kutoendesha kwa miaka miwili, toza faini 200, 000 tu kwa kosa, hakuna atakaye chezea sheria kiasi hicho!

    ReplyDelete
  2. Madereva wa dala dala ni wapuuzi tu.

    ReplyDelete
  3. Tatizo ni sheria zetu kutofanya kazi madereva wakorofi wako kila nchi ila sheria zao ni kali

    ReplyDelete
  4. Mithupu vibao pekee sii dawa inatakiwa unamfunga jela ama rumamnde mpaka jengo alimofungwa linabomoka vinginevyo afiye humu. unawapeleka mahali kama mtwara farm17 watapata habari yao. hapo dar mnawapaka mafuta tuuu

    ReplyDelete
  5. ADILI NA NDUGUZEFebruary 16, 2010

    Madereva daladala Tanzania wakorofi, Madereva wa Matatu Kenya wahuni, Taxidrivers in South AFrica very rough. Ukienda Zambia kuna Town buses driver hovyo hovyo. Yaounde Cameroon mabasi namtaxis zote ziko dented shauri ya udereva wa kihuni. Africa yote haswa South of the Sahara ni ubabe ubabe tu.

    ReplyDelete
  6. Nakubaliana nawe kabisa. Uzembe na ukorofi wa madereva hawa unasababishwa na ubutu wa adhabu au utekelezaji wa sheria za usalama barabarani. Kwa mfano nakumbuka niliwahi kukaa hostel moja ambayo mkataba wake ulisema, ukipoteza ufunguo na kusababisha kitasa kubadilishwa unatozwa faini/fidia ya shilingi 400,000 hivi (ilikuwa nje ya nchi nikimaanisha Euro 200). Hivyo, mtu yeyote atakuwa makini zaidi akijua kuna mzigo mzito ambao kuubeba ni ngumu endapo atazembea na kupoteza ufunguo. Nashangaa hata wamiliki wa mabasi walikuwa wanabishana na SUMATRA ilipopandisha faini, eti kwa kudai ni kubwa mno. Kwani kunaulazima wa kufanya kosa? Halafu SUMATRA nao eti wanakaa meza moja kujadili na watu kama hao wenye hoja dhaifu, hii kweli Tanzania.

    ReplyDelete
  7. They are driven by daily targets from their bosses, not crazy. How the driver takes it to road who cares.

    Actually, mimi nawapongeza. Hawa ni watu wa kupiga mzigo, kufukuzana na muda. That's how we chase the clean money siyo kukaa na kusuburi rushwa.

    Watz wote wanatakiwa waishi kama madereva wa daladala ili kuongeza uzalishaji kama kweli tunataka kuendelea.

    ReplyDelete
  8. jisifieni tu kupiga wenzenu vibao angetoka na sime akukate je?sio kazi yako usalama barabarani.by the way hata mimi watu wa daladala wananikera sana,to be honest madereva wengi wa dar vichwa maji, tukipigana vibao itakuwa ngumi kila kona

    ReplyDelete
  9. hii mivuta bangi iko stimu saa zote yani inapenda kuchomeka kila dakika sijui ikoje sawasawa kulambwa makofi yana yanakera haya manyangumi hadi basi kama unandesha gari dar utaungana na mimi hawa watu ovyo sana

    ReplyDelete
  10. Bongo bwana balau ya toba vurugu mechi mtindo mmoja, yaani madereva wa kibongo wanatumia mikono badala ya kutumia Indicator, vile vile sheria hamna hapa

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...