pindingu
chali...
maskini...
lori la mashudu

Na Ripota wetu, Dar
Hapa barabara ya Ali Hassan Mwinyi rodi, karibu kabisa na AAR kuna ajali ya gari imetokea muda mfupi uliopita.
Kuna hilo lori limebeba mapumba/ mashudu yale machicha ya kutengenezea nadhani bia. Sasa lori hilo likawa limefunguka mlango wa nyuma so mashudu yanamwagika tu, hivyo limepaki pembeni.
Basi kuna hii gari ndogo imekuja ikitokea mjini kuelekea Mwenge. Kumbe yale mashudu yamemwagika tokea kama mita mia hivi toka roli liliposimama na mashudu yenyewe yanateleza basi hiyo gari ndogo ile kuyakanyaga mashudu tu ikalewa ikaanza kuyumba yumba na hatimaye kuangukia mtaroni.
Kwenye gari hiyo ndugu kulikuwa na watu wawili, dereva hajaumia ila abiria (mdada) ndo ameumia na bahati nzuri madaktari wa AAR wakaja haraka na kutoa msaada na gari la wagonjwa (ambulance) likaja likambeba abiria aliyeumia.
Kusema ule ukweli kama mwenye hilo roli angeweka alama kwamba kuna tatizo (reflectors) nadhani hii ajali isingetokea.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. Mashudu yanateleza sana. Si mchezo. Niwewahi kuona magari yanateleza vibaya sana maeneo ya nyerere road pale quality plaza. kibaya gari lenyewe lilikuwa limeshayeya. Inatakiwa kuwe na utaratibu maalum wa kuyabeba hayo maulevi yenu

    ReplyDelete
  2. Pia barabara sio salama kwa maana hakuna kizingiti cha kukuzuia usiingie kwenye mtaro kama gari ina loose control. Barabara inapoishia tu kuna mitaro pembeni na ukiyumba tu kidogo ndo hivyo unadumbukia mtaroni.
    Hivyo ingesaidia sana kama wajenzi wangeweka vizingiti kuzuia magari kuingia kwenye mitaro au kwenye kona kali

    ReplyDelete
  3. Mitaro ni very Hazard. Wizara ya Usafiri inatakiwa kutafuta alternatives ya hii mitaro mfano iwekewe vizibo juu.Hii itapunguza ajali za namna hii.Sijawahi kuona nchi nyingine duniani yenye mitaro.

    ReplyDelete
  4. Mitaro inasadia sana. Magari mengi huishia mitaroni na kuepusha madhara kwa waenda kwa miguu na kusababisha ajali nyingine. Hebu fikiria lori lililo kata breki pale kibo kuteremkia Ubungo! Dereva akiliingiza mtaroni, mambo shwari kwa abiria wengine. Fikiria hata hiyo gari ndogo. Huenda dereva kaliwahisha mtaroni makusudi ili kuepusha madhara zaidi, mfano kugongana na gari linalokuja kutokea upande mwingine.

    ReplyDelete
  5. Ikikutokea tena hali kama hii usikanyage breki. Attention iwe kwenye usukani, nyoosha gari.

    ReplyDelete
  6. Pamoja na melezo mazuri na lawama kwa dereva wa kilo lori, bado ni jukumu la kila dereva kuwa makini anapoendesha gari na hasa annapoona barabara haiko kama kawaida. Hii ni sehemu ya mafunzo ya udereva "defensive driving". Nawashauri madereva wote wawe makini zaidi wanapoendesha.

    ReplyDelete
  7. ni kweli madereva wengi wa bongo hawana mafunzo yoyote ya udereva. kwa vile magari ni automatic basi kila mtu ni dereva. ndio maana ajali zinakua nyingi TZ. serikali iamke na iangalie upya utoaji wa leseni vinginevyo kila siku magari yatatumbukia kwenye mitaro..

    ReplyDelete
  8. Hii ndiyo raha ya Bongo bwana. ukiona gari lako limepata pancha au kioo cha pembeni kimekaa vibaya n.k wewe huna haja ya kuhangaika, paki hata katikati ya barabara kwa raha zako rekebisha. Hakuna haja ya kuweka alama yoyote ya tahadhali kwa wengine. Ukimaliza ingia ndani ya gari lako, mwendo mdundo.

    Mdau Mbezi kijijini

    ReplyDelete
  9. mdau mbezi umenichekesha acha tu,
    weee ndo unajua moviez za barabarani maana unakuwa kichaa tu kwakweli,,,,bado kwenye mataa ndo kasheshe jamani

    poleni mliopata ajali na mdada apone mapema tu aisee!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...