JK akilihutubia taifa wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya wanawake duniani zilizofanyika kitaifa katika uwanja wa michezo wa Ali Hassan Mwinyi mjini Tabora leo mchana.
JK akiangalia baadhi ya bidhaa zinazozalishwa na vikundi mbalimbali vya wanawake wa mkoa wa Tabora wakati alipotembelea mabanda ya maonesho katika viwanja vya Chipukizi mkoani Tabora leo
Wanafunzi wa vyuo na shule za sekondari mkoani Tabora wakipita na mabango mbele ya JK na vioingozi wengine wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Wanawake iloiyofanyika kitaifa mkoani Tabora
Wanafunzi wa vyuo na shule za sekondari mkoani Tabora wakipita na mabango mbele ya Rais Jakaya Kikwete na vioingozi wengine wakati wa kilele cha maadhimisho ya siku ya Wanawake iloiyofanyika kitaifa mkoani Tabora
Kinamama wakiwa katika maadhimisho hayo
Msanii Vicky Kamata akiwaongoza wanafunzi wa shule ya Sekoindari ya Wasichana Tabora kuimba wimbo maalumu wa Siku ya Wanawake Duniani wakati wa maadhimisho ya siku hiyo yaliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Ali Hassan Mwinyi Tabora leo mchana.
Sehemu ya wakazi wa mji wa Tabora na mikoa mingine ya jirani waliohudhuria kilele cha sherehe ya siku ya Wanawake duniani iliyofanyika katika uwanja wa michezo wa Ali Hassan Mwinyi, Tabora leo mchana. Picha na mdau Freddy Maro wa Ikulu







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 6 mpaka sasa

  1. Siamini kwamba wanawake wanaweza wakipewa nafasi. HAWAHITAJI KUPEWA NAFASI.

    Bali najuwa wanaweza kubomoa vipingamizi na kupata nafasi wenyewe bila upendeleo wala hongo, KISHA KUONYESHA UWEZO WAO.

    Upendeleo na hongo ndo vinafanya chipukizi wafikiri muda WAO ukifika watahonga au kupendelewa, HIVYO HAMNA HAJA YA KUPIGANA.

    MWANAUME.

    ReplyDelete
  2. Ninakubaliana na mdau Mwanaume kuwa alipewa tenda ya kubuni kaulimbiu "WANAWAKE WAPEWE amewarubuni akina mama, na ninafikiri ni mwanaume - ushahidi kwamba wanawake hawajiamini. Kama angekuwa mwanamke asingetunga kaulimbiu hiyo ambayo ni sumu. KUPEWA ni sumu na malipo yake ni makubwa, lakini KUJITAFUTIA ni ushindi mkubwa na hakuna anayeweza kukunyanganya au kukunyanyasa ulichojitafutia. Kwa hiyo tunahitaji miaka mingine 15 ambapo akina mama wataweza kutamka wenyewe kuwa TUJITAFUTIE/TUPAMBANE.

    ReplyDelete
  3. Nakubaliana na Anonymous Mon Mar 08, 08:22:00 PM. Hakuna haja ya kuomba nafasi wakati nafasi itakuja tu pindi wale wenye uwezo wataonyesha kuanzia chini. Kila aliye juu, katika utawala wowote ule unaofuata misingi ya utawala bora lazima alipewa nafasi kwa kuonyesha uwezo wake wa kuongoza akiwa chini. Wasione Akina Angela Milkel, mama Chancelor wa Bundescouncil nchini Ujerumani, uwezowake ndiyo uliomfikisha hapo. Dr. Rose Migiro hakupendelewa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa bali alionyesha uwezo wake katika nafasi alizokuwa amepewa huko chini. Bila kujua kuwa kwa kuwa makini katika kazi hizo za chini alijituma na hatimaye hadi Ban Ki Moon akamuona kipindi akiwa Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa.

    Hivyo, mantiki ya wanawake kujiombea nafasi wala si dalili nzuri kwao. Inaonyesha ni jinsi gani ambavyo bado hawajiamini na kuona tu njia mbadala ya kupata nafasi za juu ni Kujiombea. Mfano, Waziri katika Ofisi ya Rais-Utawala Bora ana uwezogani kama si kupendelewa tu. Hoja hapa ni kwamba; wanawake wenye uwezo watazipata nafasi zao na umma utawapongoze kwa sababu kweli walionyesha wanaweza. Siyo tu kubebwa eti kwa nafasi ni mwanamke halafu unapewa kuongoza kundi wakati uwezo huo haunao, tutapigana muda si mrefu japo tumekuwa na amani tangu Uhuru wetu. Watu kama akina Sofia Simba si wataipeleka nchi kuzimu tu kama watapewa nafasi za juu wengi kuliko kawaida.

    Binafsi natambua uwezo wa wanawake kama ambavyo wanaume walivyo, wapo wenye uwezo na wasio na uwezo katika kila nyanja. Usawa uwezo kwa kuzingatia uwezo wa mtu na si mwanamke abebwe wakati hana huo uwezo.

    ReplyDelete
  4. Tuwekee basi huo wimbo kwenye Utube tufaidike...

    Mwanamke halisi

    ReplyDelete
  5. Hivi na leo ni siku ya transvestites too?

    ReplyDelete
  6. jana ndio siku ya wanawake! mmmh kati ya siku 365 na robo eti siku moja ndio ya wananwake maanake zinazobaki za wanaume? haaaaaaaya safari bado ndefu.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...