Baada ya mpambano mkali ulioshirikisha filamu kutoka sehemu mbali mbali duniani, hatimaye mshindi amepatikana, naye ni Frederico Teixeira de Sampayo kutoka Hispania.

Filamu yake "Wash, Rinse and Spin", imeibuka mshindi kati ya filamu 500 zilizoandaliwa na watu wa kila aina kutoka mabara yote duniani.
bofya hapa uone Filamu iliyoshinda
Kuanzia mwezi Februari, BBC World News, katika mfululizo wa vipindi maalum vya televisheni na radio, vile vile online, walifanya shindano la kuandaa makala fupi ya video - kwa digital camera au mobile phone camera, ruksa!
Kwa upande wa Afrika, filamu iliyowika ni "Somewhere in Northern Tanzania", iliyoandaliwa na Ibrahim Matukuta mkazi wa Zanzibar.
Zawadi
Video au filamu tano bora zaidi kutoka kila bara - Afrika, Amerika ya Kusini + Amerika ya Kaskazini, Ulaya, Asia na Oceania, ziliingia katika fainali ambayo inarushwa kupitia matangazo ya televisheni ya BBC World vile vile zitaonyeshwa kwenye tovuti ya BBC.

Mshindi wa jumla amepatikana na
atapewa zawadi ya semi-professional HD mini DV camcorder.
Kwa maelezo zaidi, tembelea wavuti ya

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...