SERIKALI ya Japan imelikubali ombi la Serikali ya Tanzania la kutaka
igharimie ujenzi wa nyongeza wa barabara mbili muhimu Kusini na Kaskazini
mwa nchi na hivyo kupanua mtandao wa barabara za zinazounganisha mikoa yote nchini.
Makubaliano hayo yalifikiwa katika mazungumzo rasmi ya kiserikali baina ya
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri Mkuu Yukio Hatoyama wa Japan mjini Tokyo jana (Ijumaa Machi 26, 2010) katika siku ya tatu ya ziara ya siku nne ya
Mhe. Pinda nchini humo.
Baada ya mazungumzo hayo, Waziri Mkuu Pinda alisema kuwa aliwasilisha ombi kwa Waziri Mkuu wa Japan, Mhe. Yukio Hatoyama, kutaka msaada zaidi wa nchi hiyo kugharimia ujenzi wa Barabara kati ya Mangaka hadi Tunduru na kati ya Dodoma na Babati na Waziri Mkuu wa Japan akakubali.
Barabara ya Mangaka -Tunduru ni kilomita 146 na ya Dodoma Babati ni
kilomita 188. Barabara hizo ni nyongeza katika barabara Tunduru
-Tandahimba (k.m. 186) na Iringa – Dodoma (k.m. 250) ambazo tayari Japan
ilikubali kuchangia ujenzi wake kwa lami pia.
Katika mazungumzo hayo Serikali ya Japan pia imekubali kuisaidia Serikali ya Tanzania katika utekelezaji wa mradi wa Kilimo Kwanza, hasa kwa
kuwafundisha wahandisi wa kilimo cha umwagiliaji maji ambao ni wachache mno nchini.
Waziri Mkuu Pinda aliwaambia Waandishi wa Habari katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Japan (NHK) kuwa kwa jumla ziara yake ya Japan, kwa mwaliko wa Serikali ya nchi hiyo, imekuwa ya mafanikio.
“Naona tumefanikiwa sana. Hii ilikuwa ni ziara ya kuendeleza uhusiano na
ushirikiano baina ya nchi zetu na kuja kuwashukuru wenzetu kwa kutuunga
mkono kwa dhati katika jitihada za kujiletea maendeleo na kufuta umasikini,”
Mhe. Pinda alisema.
Mhe. Pinda alisema amemwalika Waziri Mkuu wa Japan kutembelea Tanzania
katika tarehe itakayopangwa baadaye na kwamba Mhe. Hatoyama ameukubali mwaliko huo.
Katika ziara yake hii ya Japan, Waziri Mkuu alitembelea shughuli za ushirika
wa wakulima na taasisi za utafiti wa kilimo na kuwa na mazungumzo na
viongozi wa Japan kuhusu kuendeleza uhusiano na ushirikiao wa maendeleo.
Jana (Ijumaa Machi 26, 2010) usiku, Mhe. Pinda alikutana na Watanzania
wanaoishi kwa kusoma na kufanyakazi Japan katika Hoteli ya Otani mjini Tokyo na kuwaambia kuwa wasikusahau nyumbani pindi wanapomaliza masomo yao au kupata nafasi ya kutoa misaada au kuwekeza.
Umoja wa Watanzania hao ulimkabidhi Waziri Mkuu Dola 2,000 (karibu Sh.
Milioni 3) zikiwa ni msaada kwa waliopatwa na maafa ya mafuriko katika
Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.
Mtanzania mmoja anayeishi Japan, Willy Ngoya pia alimkabidhi Waziri Mkuu
msaada wa vifaa 10 vya kupimia kilevi kwa madereva ili kusaidia jitihada za
Jeshi la Polisi nchini kukabiliana na madareva walevi wanaosababisha ajali
nyingi za barabarani.
.
igharimie ujenzi wa nyongeza wa barabara mbili muhimu Kusini na Kaskazini
mwa nchi na hivyo kupanua mtandao wa barabara za zinazounganisha mikoa yote nchini.
Makubaliano hayo yalifikiwa katika mazungumzo rasmi ya kiserikali baina ya
Waziri Mkuu Mizengo Pinda na Waziri Mkuu Yukio Hatoyama wa Japan mjini Tokyo jana (Ijumaa Machi 26, 2010) katika siku ya tatu ya ziara ya siku nne ya
Mhe. Pinda nchini humo.
Baada ya mazungumzo hayo, Waziri Mkuu Pinda alisema kuwa aliwasilisha ombi kwa Waziri Mkuu wa Japan, Mhe. Yukio Hatoyama, kutaka msaada zaidi wa nchi hiyo kugharimia ujenzi wa Barabara kati ya Mangaka hadi Tunduru na kati ya Dodoma na Babati na Waziri Mkuu wa Japan akakubali.
Barabara ya Mangaka -Tunduru ni kilomita 146 na ya Dodoma Babati ni
kilomita 188. Barabara hizo ni nyongeza katika barabara Tunduru
-Tandahimba (k.m. 186) na Iringa – Dodoma (k.m. 250) ambazo tayari Japan
ilikubali kuchangia ujenzi wake kwa lami pia.
Katika mazungumzo hayo Serikali ya Japan pia imekubali kuisaidia Serikali ya Tanzania katika utekelezaji wa mradi wa Kilimo Kwanza, hasa kwa
kuwafundisha wahandisi wa kilimo cha umwagiliaji maji ambao ni wachache mno nchini.
Waziri Mkuu Pinda aliwaambia Waandishi wa Habari katika mahojiano na Shirika la Utangazaji la Japan (NHK) kuwa kwa jumla ziara yake ya Japan, kwa mwaliko wa Serikali ya nchi hiyo, imekuwa ya mafanikio.
“Naona tumefanikiwa sana. Hii ilikuwa ni ziara ya kuendeleza uhusiano na
ushirikiano baina ya nchi zetu na kuja kuwashukuru wenzetu kwa kutuunga
mkono kwa dhati katika jitihada za kujiletea maendeleo na kufuta umasikini,”
Mhe. Pinda alisema.
Mhe. Pinda alisema amemwalika Waziri Mkuu wa Japan kutembelea Tanzania
katika tarehe itakayopangwa baadaye na kwamba Mhe. Hatoyama ameukubali mwaliko huo.
Katika ziara yake hii ya Japan, Waziri Mkuu alitembelea shughuli za ushirika
wa wakulima na taasisi za utafiti wa kilimo na kuwa na mazungumzo na
viongozi wa Japan kuhusu kuendeleza uhusiano na ushirikiao wa maendeleo.
Jana (Ijumaa Machi 26, 2010) usiku, Mhe. Pinda alikutana na Watanzania
wanaoishi kwa kusoma na kufanyakazi Japan katika Hoteli ya Otani mjini Tokyo na kuwaambia kuwa wasikusahau nyumbani pindi wanapomaliza masomo yao au kupata nafasi ya kutoa misaada au kuwekeza.
Umoja wa Watanzania hao ulimkabidhi Waziri Mkuu Dola 2,000 (karibu Sh.
Milioni 3) zikiwa ni msaada kwa waliopatwa na maafa ya mafuriko katika
Wilaya ya Kilosa, mkoani Morogoro.
Mtanzania mmoja anayeishi Japan, Willy Ngoya pia alimkabidhi Waziri Mkuu
msaada wa vifaa 10 vya kupimia kilevi kwa madereva ili kusaidia jitihada za
Jeshi la Polisi nchini kukabiliana na madareva walevi wanaosababisha ajali
nyingi za barabarani.
.


Hongereni wana umoja wa Japan kwa kukumbuka nyumbani. Na huyu aliezaa na mjapan m-kid wake atakuwa raia wa tanzania jina tu.Kwa uzoefu inaonyesha mtu akipata mtoto na wajepu, basi mtoto lazima abobee na kuwa mjapan 100% ukubwani.
ReplyDeleteMichu--what you forgot to report is what are the Japanese getting back from hiyo misaada. Is it a loan? if yes, is it concessional or? How are they going to guarantee oversight of these miradi? Are this projects strictly for Japanese construction firms au hata mbongo wa kawaida anaweza kubid for a mchongo?
ReplyDeleteI love your blog maan, but tuwekee a balanced report/
Mdau-
now...thats how you use public money on foreign trips by acquiring good deals for the Tanzanians...5 trips, 3 positive 1 leisure 1 failure
ReplyDeletekeep up good work pinda and who knows..u can become a savior of the poor(90%)
Anco Michusi mimi nina swali dogo tu kwenye picha ya pili na tatu kutoka chini huyo mdau alivaa scarf ya rangi ya damu ya mzee na koti jeusi je amevaa Helmet kichwani ama ndo kichwa chake real?
ReplyDeleteMdau Maswa Shinyanga
Lete hivyo vipima kilevi ili viwatajirishe 'Trafiki Polisi'. Ajali zitaendelea kama kawa. Mmomonyoko wa fikra za watanzania uliosababishwa na kukata tamaa na maisha iliyosababishwa na serikali ya sisieemmm ndiyo imetuleta hapa tulipo.
ReplyDeleteHata kila polisi akipewa pikipiki mbilimbili hakuna chenjeez zozote pozitiiv tutakazoziona. Itakuwa ni kuwaneemesha polisi tu, na sio kuleta mabadiliko yaliyokusudiwa. Hivyo vifaa vitatumiwa na polisi katika kuwatisha waendeshaji magari ili watoe elufu mbili (Shs. 200/=) fasta fasta tu.
Pole inji yangu ya Tanzania inayoangamia.
Tanzania x 2
Nakupenda kwa moyo yoteeee
Inji yangu Tanzania
Ardhi yako tajiri sanaa!
Nilalapo nakuota weweee
Niamkapo Dhahabuuu kwishlinaaaa
Inji yangu Tanzaniaaa
Inaporwa kwa kasi sanaaaa
....
Nabata ushungu .... heri niishie sasa. Naingia mitini
Dayasipora
Mdau Anonym 10:19,
ReplyDeleteNafurahi sana kwa kugundua hilo lakini siyo Michu mwenye hilo tatizo. Mimi ni mzawa wa bongo na kama nikijaribu kuvuta fikra siku za nyuma sana...miaka ya 1970 kuja hadi 2000...sikumbuki wakati wowote Tanzania inakopeshwa. Tanzania inasaidiwa tu haikopeshwi lakini katika taarifa mbalimbali za kiserekali tunaona kuwa tuna madeni...Hilarious...Inafurahisha sana...misaada,misaada, misaada..lakini mwisho inageuka kuwa madeni lakini inakuwa madeni wakati waliokuwa viongozi waliosaidiwa wamestaafu au wametoka madarakani...hakuna wa kumuuliza kuwa hili deni ni lipi na pesa iliokopwa ilifanyia nini....Jamani jamani...tuamke! na tuwe wakweli na tuwe na uwazi! Tumekopeswha kiasi hiki, na tunatarajia kufanyia hili, natunatarajia kurudisha kwa namna hii, kwa kipindi hiki...kwisha...blablablablabla tumesaidiwa...weweeeeeeee....
Wadau wa japan mnaonekana mnamshikamano sana ina reta moyo ila sijuwi na nyinyi mna mpango wa kufungua tawi la ccm ? ila nisinge kushaulini mlete ujinga wa siasa ughaibuni nyinyi fanyeni kazi kama wajepu wenyewe hawa jamaa walio leta siasa EU naona vichwa vyao sio vizuli. mdau wa kabur afughan
ReplyDelete