*Wagonjwa watatu wathibitishwa kuwa na virusi vya H1N1
*Hali imethibitiwa,
*Hali imethibitiwa,
*Wataalamu wamepelekwa na dawa zimeshafikishwa eneo husika
*Karantini imewekwa bila kudhuru uzalishaji
Machi 3, 2010, Kahama, Shinyanga –
*Karantini imewekwa bila kudhuru uzalishaji
Machi 3, 2010, Kahama, Shinyanga –
Mgodi wa Buzwagi jana ulithibitisha kuwepo kwa wagonjwa watatu ambao ni wafanyakazi wa mgodi wenye virusi vya H1N1, au mafua ya nguruwe. Wafanyakazi hao ni wakazi wa mgodini na mpaka sasa hali zao ni nzuri na wanaendelea kupata nafuu.
Hapo awali mgodi ulikwishachukua hatua za dharura, ambazo ni pamoja na; kupima afya za wafanyakazi , kuwatenga walioathirika na kuwapatia dawa za Tamilflu ambazo ni maalum kwa kutibu virusi hivyo.
Mgodi huo ulituma vipimo vinne kwa ajili ya upambanuzi wa aina ya virusi, katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Maswala ya Utabibu (NIMRI), ilioko Dar es Salaam. Hapo Jumaatatu Machi 1, NIMRI ilirudisha majibu yaliothibitisha uwepo wa virusi vya H1N1 kwenye vipimo vitatu kati ya vinne vilivyowasilishwa.
Mgodi wa Buzwagi unafanya kazi kwa karibu na daktari wa wilaya ya Kahama pamoja na Wizara ya Afya kufuatilia hali ya walioathirika na kuthibiti kusambaa zaidi kwa ugonjwa. Vilevile timu ya wataalamu imetumwa kutoka Wizara ya Afya na bingwa wa maswala ya afya wa Barrick pia yupo mgodini kutoa ushauri na kusimamia matibabu.
Wafanyakazi wote wasio na majukumu ya lazima wamerudishwa majumbani na mienendo ya watu wanoingia na kutoka mgodini unathibitiwa ipasavyo.
Mpaka sasa watu 21 wako kwenye karantini na wanapatiwa matibabu kamili. Bado ni mapema mno kubaini chanzo cha virusi kwa vile uchunguzi bado unaendelea. Tutawahabarisha kadri tunayvopokea taarifa mpya.
About African Barrick Gold
African Barrick Gold Corporation is the fifth largest gold mining company in Africa. African Barrick Gold (ABG) is soon to be listed on the London Stock exchange and plans to seek future listing on the Dar es Salaam Stock Exchange.
African Barrick Gold operates four mines in Tanzania; Bulyanhulu, North Mara, Tulawaka and the Buzwagi mine.
Issued By;
Teweli Kyara Teweli
PR & Communications
African Barrick Gold,
Mgodi huo ulituma vipimo vinne kwa ajili ya upambanuzi wa aina ya virusi, katika Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Maswala ya Utabibu (NIMRI), ilioko Dar es Salaam. Hapo Jumaatatu Machi 1, NIMRI ilirudisha majibu yaliothibitisha uwepo wa virusi vya H1N1 kwenye vipimo vitatu kati ya vinne vilivyowasilishwa.
Mgodi wa Buzwagi unafanya kazi kwa karibu na daktari wa wilaya ya Kahama pamoja na Wizara ya Afya kufuatilia hali ya walioathirika na kuthibiti kusambaa zaidi kwa ugonjwa. Vilevile timu ya wataalamu imetumwa kutoka Wizara ya Afya na bingwa wa maswala ya afya wa Barrick pia yupo mgodini kutoa ushauri na kusimamia matibabu.
Wafanyakazi wote wasio na majukumu ya lazima wamerudishwa majumbani na mienendo ya watu wanoingia na kutoka mgodini unathibitiwa ipasavyo.
Mpaka sasa watu 21 wako kwenye karantini na wanapatiwa matibabu kamili. Bado ni mapema mno kubaini chanzo cha virusi kwa vile uchunguzi bado unaendelea. Tutawahabarisha kadri tunayvopokea taarifa mpya.
About African Barrick Gold
African Barrick Gold Corporation is the fifth largest gold mining company in Africa. African Barrick Gold (ABG) is soon to be listed on the London Stock exchange and plans to seek future listing on the Dar es Salaam Stock Exchange.
African Barrick Gold operates four mines in Tanzania; Bulyanhulu, North Mara, Tulawaka and the Buzwagi mine.
Issued By;
Teweli Kyara Teweli
PR & Communications
African Barrick Gold,
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...