Juan Antonio Samaranch (1920 - 2010)
Dunia na hasa ulimwenguwa michezo umempoteza mtu mashuhuri sana, aliyekuwa raisi wa Kamati ya Olimpiki duniani (I.O.C) bwana Juan Antonio Samaranch, ambaye amefariki dunia kwa ugonjwa wa moyo akiwa na umri wa miaka 89.

Bwana Samaranch anakumbukwa kwa kuchukua uongozi wa IOC kutoka kwenye kipindi kigumu cha migomo toka nchi mbalimbali na matatizo ya kifedha kiasi cha kutishia kufilisikakwa shirikisho hilo.

Alipoingia madarakani mwaka 1980, bwana Samaranch alibuni na kufanikisha miradi kadhaa ya kuliingizia fedha katika Shirikisho hilo, kiasi cha kulianya kuwa shirika lenye utajiri wa kibilionea. Alitengeneza faida ya dola za Kimarekani milioni mia mbili na hamsini ($250,000,000) kutoka dola laki mbili tu ($200,000) alizozikuta alipoingia madarakani.
Habari kamili

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...