ankal akiwa na Jane John wa TBC-1 (shoto) na Shamim Zeze wa Darhotwire katika mnuso fulani hivi. Kinadada hawa ni wana libeneke mahiri na Globu ya Jamii inachukua nafasi hii kuwapongeza kwa kuendeleza libeneke na kuwahamasisha kinadada wengine waige mfano kwani wigo wa libeneke bado ni mpana sana na hauna mwenyewe. Watembeleeni.
kwa Shamim Zeze
kwa Jane John

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. Salaam Waleikum Ankal, asante sana kwa kututambulisha BLOG NYINGINE pia kwa mwangazo wa aina nyingine. NAOMBA KAMA KUNA MWENYE KUFAHAMU BLOG NYINGINE ATUWEKEE HAPA ILI TUZISOME NA KUBURUDIKA.BLOG ZA WATANZANIA, KAMA HIZI ZA KINADADA HAPA. SHUKRANI ANKAL.

    ReplyDelete
  2. Anko Michuzi, nina swali la kizushi. Unakumbuka wapi au unakumbuka nini ukiona picha kama hiyo ya mtu ameshika chupa ya soda, bia au juice? Mimi mwenzio nakumbuka enzi zetu nikiwa LY kule kijijini kwetu siku ya graduation. Hapo nimemnunulia nanihino wangu chupa moja ya soda ajidai nayo.Wakati huo soda yenyewe unakunywa kwa mwaka mara moja hasa kwenye graduation.Yaaaani hiyo lazima ionekane kwenye picha.Raha kwelikweli.....

    Mdau
    Mbezi Luis

    ReplyDelete
  3. JE ZEZE HUSAHAULIWA AU KUNA SABABU

    Da Shamim Zeze hajapata bahati ya kutunukiwa zawadi kama kumbukumbu.
    Mchango wake katika fani ya urembo,sherehe na mavazi mbali mbali katika jamii yetu yastahiri kupongezwa na tunu ya zawadi ya kukumbukwa na kizazi kijacho.
    Mashirika mengi ambayo yanafanya vizuri katika uchangiaji na utoaji wa zawadi mbalimbali lakini DaZeze hajabahatika kupata zawadi ya kumbukumbu kwa kizazi kijacho. Sizungumzii "IPHONE au "IPAD" DaZeze anastahiri tunuko la zaidi ya hapo.
    Namtakia kila la kheri katika maendeleo ya libeneke kwa warembo,sherehe na mavai bila ya kusahau ukurasa wa "maisha" katika Darhotwire.

    Mickey Jones
    Denmark

    ReplyDelete
  4. Dada Shamimu Zeze, nimefurahi kukuona, nilikuwa najua kuwa Darhotwire haina msimamizi maana ilikuwa imejaa matusi na watu kuchafuliana majina. Naomba lifanyie kazi hili.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...