Nimekuwa nikijiuliza ni kwa nini ajali za kutisha haziishi nchini kwetu. Je ni Barabara mbovu, Uongozi mbovu au Madereva wetu ndio wabovu? Je kama ni wabovu, leseni zao wanazipatapaje? Katika kuzunguka nchini, nilifanikiwa kuzipiga hizi picha ambazo ningewaomba wadau mzichambue na kuamua wenyewe chanzo cha ajali mbaya katika nchi yetu. Lori ina ovateki juu ya mlima !!!!! Basi la Abiria nao wamo
John Mashaka
mashaka.john@yahoo.com
Dar es Salaam, Tanzania
hapa madereva wanatanua kwenye alama zinazokataza kuovateki


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 68 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 18, 2010

    Kwa kifupi ni kwamba, system nzima Tanzania ni haifanyi kazi. Tunaishi kwa kudra za mwenyezi Mungu tu. Hamna mwenye uadilifu na kuheshimu chochote akifanyacho, awe ni dereva, polisi, mhasibu, kiongozi wa kisiasa, .................you name it. Completely broken system!

    ReplyDelete
  2. Hata wewe John Mashaka unachochea ajali unapiga picha wakati unaendesha gari?

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 18, 2010

    Moja ya sababu si umekwisha itaja mwenyewe na ushahidi umeouonesha? Kama unaleseni wewe uliipataje? Au muulize mtu yeyote mwenye leseni hasa ya magari ya abiria (Class C) aliipataje?

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 18, 2010

    Naafikiana na maoni ya Anon May 18, 09:24:00. Aidha kiongozi akianzisha jambo katika taasisi yoyote akiondoka tu basi lile suala linakosa sustainance. So sad indeed. Kiasi kwamba the psychological make up ya kila mtu ndani ya taasisi ni kuchukua chako (as long as it is supposed to be yours) kuchukua chako mapema. Sijui tufanyeje.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 18, 2010

    BARABARA NI MBAYA,HAZIKUJENGWA KWA KIWANGO KISASA ILA CHA KIZAMANI,KWENYE MILIMA BARABARA ZA WENZETU ZINAKUWA PANA ZA KURUHUSU MAGARI MATATU KUPISHANA LAKINI SISI BARABARA NI FINYU TANZANIA MAGARI YAMEONGEZEKA KWA HARAKA NI MENGI MNO,TUSILAUMU MADEREVA TULAUMU UJENZI WETU NA MIPANGO YETU MIBAYA KATIKA UJENZI WA BARABARA

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 18, 2010

    Your very very right.SOME drivers I think are tired of their life and want die on the roads and kill innocent people in their quest.broken brains and morals as well.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 18, 2010

    Mkuu hapo nakupa tano yaani umelenga kwelikweli. According to picture inaonyesha madereva ndio wabovu
    Hiyp picha ya kwanza dereva wa upnde huu haruhusiwi ku overtake lakini wanaovertake.
    hii nyingine both side hawaruhusiwi ku overtake
    Swali la kujiuliza jee walipataje leseni ?

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 18, 2010

    Kaka MISUPU hiyo barabara yenyewe ni SINGLE FILE halafu mtu bado anataka kuovertake kibishibishi dah kweli Bongo hatari tupu.
    Mdau Ukerewe!!!

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 18, 2010

    ANON WA KWANZA AMESEMA KWELI SYSTEM NZIMA MBOVU.DEREVA WA BASI LA ABIRIA KWENDA MIKOANI AKIPAKI BASI KWENYE HOTELI KWA AJILI YA ABIRIA KUPATA MLO ANAPEWA HONGO YA KULA BURE NA ANASTUA NA BIA AU KONYAGI AKITOKA PALE MWENDO MDUNDO,HAPA KWA WENZETU UK KARIBU NA MBINGUNI,KUWA DEREVA LAZIMA USOME THEORY UFANYE TEST UPASS,KISHA UFANYE PRACTICAL TEST MPAKA UPATE LESENI WE NI DEREVA KWELI NA UKIKAMATWA UNAENDESHA BILA LESENI ADHABU YAKE NI KWENDA JELA NA SIO FAINI ACHILIA MBALI ULALIWE UNAENDESHA UMELEWA.SASA KWETU RUSHWA KILA IDARA,NI MUNGU TU ANAJUA TUNAISHIJE BONGO.QUALIFICATION YA KUWA DEREVA UANZIE UTINGO,TATIZO NI KUBWA NA SERIKALI ZETU HIZI ZA SIKUIZI VYEO KWA KUJUANA SI UTENDAJI TUMEKWISHA.

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 18, 2010

    Jicho la kamera linaonesha kuwa wewe mwenyewe Mashaka katika kupiga picha hizi ulikuwa unaingia upande sio wako na hivyo kuchochea uwezekano wa AJALI

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 18, 2010

    Nakubaliana na mdau wa 7. Tatizo Tanzania (na sehemu nyingi za mashariki na kusini mwa Afrika), mtazamo wa WATU ndio wenye kasoro na SI mabarabara wala system. NIJIELEZE: (1) Madereva wengi hawataki kufunga mikanda ya viti mpaka wamuone askari "traffic". (2) Ukisafiri na basi, kama dereva anakwenda mbio ukilalamika abiria wengine wanakujia juu na kukuambia viyu kama "kama huna haraka bora ushuke , sisi tunataka kuwahi...etc."; Na hili haliishii barabarani tu: (3) Hata watu wenye kujua kuwa kuna ukimwi, hawakubali kupima kabla ya kuoa/kuolewa na wakishakunywa bia moja hawataki kutumia condom; (4) Hata wasomi wenye kujua madhara ya ulevi wa kupindukia ("alcoholism") utakuta wanakunywa mpaka watapike, waanguke, wajikojolee au waishiwe na pesa. Hapa Dar, 2002, nilimtukana Mzungu mmoja sana aliposema kuwa WA-TZ ni watu "suicidal" wasiothamini maisha kutokana na uendeshali wao, ulevi wa kupindukia na kutojikinga kwa ujumla ili kustiri maisha yao. Lakini kila kukicha nazidi kukubaliana naye. Lazima tubadili mtazamo ("mentality" yetu)wetu na kuthamini maisha yetu, ya watu wengine na hata viumbe vingine. Vinginevyo tutabaki watu wa kulalamika daima na kungojea tufanyiwe kila kitu na kuwa "monitored" kama watoto. Mabadiliko yaanze katika nafsi zetu, familia zetu, mitaa yetu, vijiji vyetu, miji yetu na kwenda juu, na SIYO kutoka juu kuja chini. SOmeni historia za wenzetu jinsi walivyoendelea. They always worked hard and progress came from grassroot community VALUES!

    ReplyDelete
  12. KalikaliMay 18, 2010

    Hili ni tatizo kubwa Tanzania. Na ni hatari si kwa wavunja sheria wenyewe tu, bali kwa watumiaji wengine hasa wanaofuata sheria za barabarani. Wewe utakuwa unaendesha kwamba sheria inakuruhusu uko upande wako, lakini mara mjinga mmoja anakufuata huko huko na kukuua! Pamoja na kwamba alama ziko wazi kuwa usi-overtake hapa, bado watu wanaamua ku-overtake! Imekuwa nchi ya law of the jungle - serikalini, wizarani, shuleni, benki, siasa, barabarani nk nk. Na mimi nauliza: sijui tufanyeje. Nadhani kwa kuanzia tunahitaji serikali ya dikteta.

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 18, 2010

    Kuna mdau hapo juu amesema kwamba tunaishi kwa kudra za mungu nami nakubaliana naye kwa 100%. Kimsingi watanzania karibu wote hatuna utamaduni wa kujali taratibu, kwa mfano leo asubuhi wakati niko katika daladala watu walikuwa wanalalamika kwa sababu dereva alikuwa hatanui wakati wenzake wanatanua na kuwawahisha abiria wao. Sasa nikawa najiuliza mwenye matatizo hapa ni nani, huyu ambaye hatanui au wale wenye kuvunja taratibu na kutanua ili wawahi.

    ReplyDelete
  14. Nabii TitoMay 18, 2010

    MTUME NABII YOHANNA MASHAKA, MBONA UMETUACHA KAMA VILE MAYATIMA BWANA? SISI NI FANI ZAKO AMBAO KILA SIKU TUKO TAYALI KUZIPIGA KWA AAJILI YAKO, KWA HIYO UNAPOTEA KWA MUDA MREFU NA SISI TUNABAKI UPWEKE. ATIKO ZAKO MKUU TUMEZIMISI SANA ILA NAONA UMELUDI NA STAILI YA TASWIRA. SASA MKUU TUNAOMBA U BIEVU KAMA MSOMI WA UCHUMI TOKA MUZUMBE CHUO KIKUU CHA UNIVESITI CHAKO WEWE MICHUZI NA PETER NALITOLEA. LETA ATIKO BWANA JAMVINI KUCHANGAMKE, ALAFU UJE KWENYE MAHUBIRI YANGU YA KULE NANIHII, ILA ANGALIA USIPOTEZE NETIWAKI WAKATI UNAENDESHA GARI BWANA TUNAKUHITAJI SANA, MTUME NABII

    ReplyDelete
  15. AnonymousMay 18, 2010

    miimi nilidhani john mashaka hajui kiswahili, sasa yeye anafanya nini kwenye hizi barabara? bwana kuendesha bongo mkuu kunahitaji ungangari, hawa siyo watu wa kushindana nao. wengine tayari wameshakunywa, au wengine wako high na ile ninihiii ya asili, yaani ile mmea kijani ya ninihiii

    ReplyDelete
  16. US BloggerMay 18, 2010

    Dr. Us Blogger)

    Watu wanapoishiwa na mada ndo wanabakia hivi. Nabii ameniogopa debeti kwenye redio na luninga. Tayari nimemmpa ofa ya DOLA MILLIONI MOJA lakini bado ananikimbia kimbia kwenda kupiga picha za kizushi

    Nabii hacha kunikwepa bwana grow up and be a man

    Dr. US Blogger
    Alumni OXFORD University
    Economics Department

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 18, 2010

    John Mashaka, kumekucha Ukonga!!!! vipi umekuja kugombea? Mnyika Ubungo na NNuaye, Ukonga John Mashaka na Makongoro Mahanga, Kinodnoni Zitto Kabwe na Hildebrand Shayo. Temeke January makamba na ShyRose Banji, mwaka huu kuna shuguli... ilala Stevini Kanumba na Wema Sepetu. tuone sasa nani zaidi,

    ReplyDelete
  18. AnonymousMay 18, 2010

    JOHN MASHAKA ATIKO ZIKO WAPI?
    kama hauna atiko basi kula kona

    ReplyDelete
  19. AnonymousMay 18, 2010

    ankal, hivi jonh mashaka ni wazili wa nini? na anafanya kazi gani huko marekani,
    kwa maana nasikiaga tu jonh mashaka lakini sielewi mie

    ReplyDelete
  20. AnonymousMay 18, 2010

    NGOMA DROO SI MPIGA PICHA WALA DEREVA MZEMBE WOTE NI WALE WALE TU, NI KAMA HUKUMU YA FISADI WAKATI HAKIMU NAYE FISADI, YAANI NI SAWA NA KUAJIRI MWIZI ALINDE NYUMBA YAKO...

    ReplyDelete
  21. Jabilo Wuod KakseruMay 18, 2010

    Bw. Mashaka Mimi siwezi kukupigia kura hadi hospitali yetu ya shirati ipate vitanda vipya. Watanzania siku hizi tumekuwa wajanja. In idwaro telo to Jo thuru ok ikony waneni mana e TiVi ichalo rais mar piny ngima? Omera ji oheri ndi nikech in kod chuny maber, Koro kel maendeleo dala koro ekawana miyi ombulu jatelo ondiek marach

    ReplyDelete
  22. AnonymousMay 18, 2010

    mashaka siye wabongo hii ni kwaida. Kwanza dereva anapoendesha hivyo ndo anaonekana mjanja. Wewe si unakuja tu mara moja na kula taswira, njoo upande dadadala uone mambo Yao ya rash hawa

    ReplyDelete
  23. AnonymousMay 18, 2010

    jani!! madereve hawajui sheria za barabarani hlf njia zenyewe mbovu na madereve walevi sana karibia asilimia 80%!!!

    ReplyDelete
  24. AnonymousMay 18, 2010

    i think Tz is the only country whr u can drink and drive..
    Sam

    ReplyDelete
  25. AnonymousMay 18, 2010

    Mr president bring articles on economy tuisheni vinywa

    ReplyDelete
  26. AnonymousMay 18, 2010

    hivi huyu mashaka anatoa wapi hela za kuja Tanzania kila baada ya miezi miwili , na hata muda wa likizo anapate kwa maana mfanyakqzi wablawaida marekani anapata siku 14 tu kwa mwaka. Isije ikawa hela za mama yangu za kodi ndo zinazolipa zile hizi nauli za kuzurura kwenye first class na kupiga picha

    ReplyDelete
  27. Wadhi KanyeMay 18, 2010

    ankal Nina hasira kweli, wiki nzima sijafanya kazi, masaa yangu kazini yamepunguzwa sijui nitalipaje renti mwisho wa mwezi huu. Matusi yananiwasha Tena ya nguoni, hebu tundika picha za nabii au atiko tumumwagie matusi. Hawezi kuwa rais bila ya kula matusi ya mashabiki. Haki ya nani, Nina hasira za kufa mtu, ntarukwa na akili hii boxi ya marekani balaa

    ReplyDelete
  28. AnonymousMay 18, 2010

    ata mie uwa nakunywa na vitafunwa na uku naendesha espeshali nikiwa nawai asubuhi kazini na sina muda wa kukaa dining...
    ukikijidai kufata sheria utatukanwa njia nzima na madereva adi stimu ikutoke na usiwe na raha cku nzima,sasa ya nini?na ww unabidi uwe mwehu tu

    Mola tunusuru

    ReplyDelete
  29. AnonymousMay 18, 2010

    Kwenda Tanzania kwa watu wa kujitusha Kama hawa ni Kama $12,000 matumizi mara 4 kwa mwaka ni Kama $48,000 kwa Mshara wa Jon mashaka wa $5 kwa saa nashindwa hizi hela anatoa wapi. Wanajamvini kuna kitu hapa nakosa hembu mnisaidieni

    ReplyDelete
  30. AnonymousMay 18, 2010

    Sasa ikiwa mashaka alikuwa abiria kwenye hiyo gari je?

    ReplyDelete
  31. Walioonewa mbweniMay 18, 2010

    wanadamu ndo tulivyo. Ajabu kumuona mtoto mdogo miaka 32 kuhamisha familia14 kwa sababu wana vijisenti. Hebu fikiria ulipolelewa panauzwa kwa sababu mtu ana uwezo wake wa kifedha heti renchi ya billioni moja????. Sasa sisi tuliolelewa kwenye maeneo hayo tunakuwa hatuna pa kuishi tena, jamani haki iko wapi, ranchi ya heka Mia moja itakusaidia nini? Wakati maisha ndo haya mafupi? Haya wenye nguvu wapisheni

    masikini waliohamishwa kwenye eneo Lao na mashaka
    mbweni beach dar isalama

    ReplyDelete
  32. AnonymousMay 18, 2010

    System! Yes our system is dead. Big up kwa mdau wa kwanza kabisa hapo juu. System (kwa barabara) inahusisha vitu vingi kama watumiaji,wasimamizi na watengenezaji. Hapo picha zinaonesha watumiaji wasivyo makini. Vitu kama kutoa leseni feki,matairi yasiyo na viwango,vifaa au spea feki au used zisizo na ubora,magari mabovu kutembea barabarani n.k ni makosa ya wasimamizi. Barabara nyembamba,mbovu nk ni watengenezaji . So our system is dead and buried. Tuanze kuchanganua namna ya kuitengeneza upya ili ifanye kazi. Itachukua muda,na gharama kubwa kuiweka ifanye kazi ila mwisho itapunguza ajali kwa kiwango kikubwa kuliko njia zote za sasa

    ReplyDelete
  33. AnonymousMay 18, 2010

    Kwa kweli mie sielewi ni kwa nini John mashaka is such a polarising figure in Tanzania, jina lake linapotokea sehemu mijadala inakuwa mikali kuliko kawaida
    rais wa nchi, vingozi wa juu na wakimataifa wanapachikwa humu lakini sionahi comments za kishabiki au za chuki Kama za John mashaka,
    niseme wanaomkaribia ni hasheem thabeet na stivini kanumba, kilichoniacha hoi ni video yake mwaka Jana iliyovutia watu karibia 50,000 chini ya mwezi
    mie naona siyo vyema kuwa contreverial hivyo. Naona wameanza kumsujudi na kuanza kumuota rais basi kesho tu atapewa urais kweli kwa kuwa amerokea marekani. Hii ndo sababu kubwa wazungu wanaiba Mali asili zetu

    ReplyDelete
  34. AnonymousMay 18, 2010

    Kuna utafiti umefanya wa wanasayansi wa pyschologia huku scandinavia ninapoishi, wamegundua kuwa watu wenye wivu, haters, wafitini na wenye roho mbaya huwa wanapunguza kinga yao ya mwili yaani energy-carolies kubwa muno sawa na zaidi ya ile nguvu mwanamme anapoteza wakati wa kupiga bao-ejaculation. Sasa nimefuatilia watu wanao mpinga Bwana Mashaka maoni yao ni wivu, chuki na haters, wewe unaoji kwa nini mashaka anapenda kusafiri US via Bongo mara kwa mara, hili jambo linawezekana inategemea wewe kazi yako ni ipi, Ushauri wa bure, nyie wenye chuki mnajiua wenyewe, you will never stop someone who is destined to win.
    mdau regards-Finland

    ReplyDelete
  35. AnonymousMay 18, 2010

    ankal sina chuki wala wivu na nabii Ila ningefurahi kweli kuona huyu jamaa anapewa kolamu kwenye globu ya jamii kwani abakunwa vichwa kisawasawa hadi anapewa urais wa nchi 2015. Tusche utani jamaa anajuwa sans kuanzisha mijadala chanya

    ReplyDelete
  36. AnonymousMay 18, 2010

    @ mdau wa FINLAND
    unikome na ukomae, sina wivu wala nini nyinyi ndo wale wanaomsujudu nabii wenu mashaka. Mm sijipendekezi kwa mtu, na mtu mzima atishwi nyau

    ww mtoto mdogo anatoa wapi hela $50,000 kila mwaka kuzunguka nchi, Mtu mwenyewe analipwa $5.75 kwa saa. Hizo hela zinatoka wapi? Hadi kununua ranchi ya 1billion???? Wizi mtupu mnaotetea, hawa ndio watakao iuza hii nchi mkiwaendekeza

    ReplyDelete
  37. AnonymousMay 18, 2010

    Anayemponda mtume nabii ni demu wake wa zamani wa Kule Houston, kwa sababu mengi ya chuki yanayoandikwa humu ndo Yale Yale anayoongeaga kwa watu. Nadhani Ana uchungu wa kutemwa,, kudadadeki atajiju. Wanawake tunashida kweli, sasa kaa mtu mliachana naye kazi gani Au faida gani kupondana

    ReplyDelete
  38. AnonymousMay 18, 2010

    Jamani utulivu, hii blog siyo ya John mashaka, hii blog ni ya ankal, puuhhhh wabongo yani sijui tukoje!!!!!

    ReplyDelete
  39. Hasheem ThabeetMay 18, 2010

    brother mashaka, good job, keep on representing Tanzania economic, karibu sana Memphis

    ReplyDelete
  40. AnonymousMay 18, 2010

    Hii blogu inatumbuiza kweli. sina mbavu yaani mashaka jina lake likitolea tu watu wanakuwa weu
    mashaka juu juu juuzaidi
    sisiemu juu juu juu zaidi
    teteeeeee

    ReplyDelete
  41. AnonymousMay 18, 2010

    wallstreet imekufa, safari za mashaka za kila siku ni kutafuta kazi serikalini, kazi ipo!

    ReplyDelete
  42. AnonymousMay 18, 2010

    John na hasheem wote mashauzi tu, sijui kwa sababu ya nafasi zao au kwa sababu wanaishi marekani
    bwana hela ipo bongo, kwa jinsi wanavyochezea hela hawafiki mbali

    ReplyDelete
  43. AnonymousMay 18, 2010

    ankal kidumu globu ya jamii, hii ni kiburudisho tosha. Sasa mada ya ajali imegeuka kuwa madavya mtu mwingine? Au kwa sababu wameona jina la John mashaka, kesho muweke kanumba ze Greti

    ReplyDelete
  44. AnonymousMay 18, 2010

    john wa Mashaka inabidi akamatwe tena afungwe mikono nyuma hapo angesababisha ajali au wadau mnaonaje

    ReplyDelete
  45. AnonymousMay 18, 2010

    INAMAANA NYIE WOTE MNASHINDWA KUJUA KWAMBA HIZO BARABARA KAMA ZINGEKUWA NA 2 LANES KWENDA NA 2 LANES KURUDI AJALI ZINGEPUNGUA SANA? UKIWA NA 2 LANES KWENDA MTU ANAPO OVERTAKE GARI YA MBELE KAMA INAENDA MWENDO MDOGO HATOWEZA KUKUTANA NA GARI NYINGINE INAYO RUDI KWANI INATAKUWA KWENYE 2 LANES ZA UPA MWINGINE.

    by akili ni nywele kila mtu ana zake.

    ReplyDelete
  46. AnonymousMay 18, 2010

    Anony Tue May 18, 09:54:00 AM you have problems; macho yako ni mabovu kabisa, chunguza mistari mieupe mbele na nyuma ya nissan/patrol ukubali kuna kona going to the right back side of yourself. Kubali bwana mashaka alikuwa nje ya barabara au abiria wakati anapiga hiyo picha.

    ReplyDelete
  47. AnonymousMay 18, 2010

    Kuna watu akili zimetulia na mada zao sio Kama hizi, hapa hakuna mjadala wowote basi kwa sababu watu wameona jina la John mashaka. Mashaka kaungane na nabii mwenzio nabii tito mpromoti kinywaji cha kili

    ReplyDelete
  48. AnonymousMay 18, 2010

    wenye wivu na wajinyonge rais mashaka namfagilia hadi keshokutwa. Hawa ndio watanzania walio nje wanaotuwakilisha watanzania kwenye anga za kimataifa. Huyu ni mchumi mahira Tena msomi makini sana, kwa hiyo kaka endeleza libeneke, kwani mpo wachache
    united nations --- rose migiro
    NBA ----- hasheem rhabiti
    walstrit--- Jonh mashaka
    filamu---- stivini kanumba
    NASA ----dr. Peter kalegele
    Tanzania oyeeeeeeee

    ReplyDelete
  49. AnonymousMay 18, 2010

    Hii nchi imekwisha hakuna cha mtihani wala nini. Toa kesho unapata leseni yako, kwa nini ajali zisiishe? Alichofanya mashaka ni kuleta mada ili tujadili Ila sielewi imeuka vipi kuanza kumjadili yeye mleta mada? Huo ndo ujinga wetu watanzania hatuko serius kabisa. Heri tusherekee bethidei ya mboni kuliko kujadili vitu muhimu
    mdau
    Manchester

    ReplyDelete
  50. AnonymousMay 18, 2010

    Kwa watu wenyebusara, kumponda mashaka siyo dawa dawa ni kujibu hoja zake kwa hoja,
    vinginevyo mnazidi kumjenga na kumpa umaarufu Mkubwa mnaompa sasa hivi
    pengine hoja kwa hoja siyo personal attack
    heti analipwa $5 kwa saa, watu wengine bwana watakufa
    wanatembea kwa wivu.

    ReplyDelete
  51. AnonymousMay 18, 2010

    Hanitishii mtu bwana. Kama ni hela tunazo.mtoto wa mkulima hawezi kunibabaisha
    mtu hawezi kwenda popote humu mchini
    bila kupitia familia zetu, hawezi mtu kuwa kiongozi
    bila kuwa mtoto wa mkubwa
    mashaka ni ndoto za mchana tu
    hawezi kuwa hata tarishi wa nyumba kumi
    huyu mashaka wenu mbona hata kununua Vogue inamshinda??
    Siye vogu ndo baikeli zetu na benzi ndo zetu za kansani
    mtajiju
    toto la kigogo

    ReplyDelete
  52. AnonymousMay 18, 2010

    nadhani hawa mashaka worshippers hawajui kwamba mashaka siyo mtanzania. Kwa taarifa yenu mashaka ni mtu wa msumbiji

    ReplyDelete
  53. AnonymousMay 18, 2010

    WEWE UNAESEMA MASHAKA ANALIPWA $5.75 KWA SAA EITHER UTAKUWA UMELEWA GONGO AU WANZUKI,KAMA SIVYO BASI NI MBUMBUMBU,MAREKANI HAKUNA MSHAHARA WA $5.75/HR.NAISHI CALIFORNIA NA MINIMUM WAGE NI $8.25/HR NA HIYO NI KWA NON-PROFESSIONALS KAMA KWENYE RESTAURANTS.MSHAHARA WA MTU KAMA MASHAKA MASTER'S DEGREE ITAKUWA SI CHINI YA $80,000 A YR.KAMA HUJUI KITU ACHA KUROPOKA MJOMBA.

    MDAU,CA-USA

    ReplyDelete
  54. AnonymousMay 18, 2010

    Wtanzania tuna matatizo makubwa kweli, tuna Imani potofu mno.

    Mtu hawezi kutushinda akiweza basi majungu ndo haya. Sasa ubishi na kipato chake vinaingilianaje?

    mwenzenu anazungumIa ajali nyie sijui ranch, sijui hela anatoa wapi. Katafuteni zenu na nyinyi Kisha mtaona raha ya kusemwa

    ReplyDelete
  55. AnonymousMay 18, 2010

    Sam, you are wrong! In all Eastern, southern and central African countries people DRINK and DRIVE, especially in Kenya, Malawi, Zambia and Zimbabwe. Like one Mdau said above, it seems that in these countries people glorify alcohol and don't value life. I agree with one of the people who said that it's a problem of MENTALITY. No one wants to take responsiblity for our rashness, recklessness, drunkeness, lateness, laziness, envy; instead Ohh it's the roads or system or the government or some bloody excuse!!!. The hell no!!! it's our mentality. Ngowi7.

    ReplyDelete
  56. AnonymousMay 19, 2010

    WATU BWANA, HAMNA MAHALA POPOTE PALE AMBAPO AMESEMA ALIPIGA HIZO PICHA AKIWA ANAENDESHA GARI WACHENI KULALAMA KITU AMBACHO HUNA UHAKIKA NACHO

    ReplyDelete
  57. AnonymousMay 19, 2010

    wanawake ni nuksi, yupo demu mmoja ameniambia yeye alimtaka mashaka, jamaa katoa nje sasa kazi yake imebaki kuandika message za uongo na matusi, mimi nakubaliana na Mdau wa Finland kuhusu utafiti wa kisayansi, mwanamke utakufa bure, wewe na wenzako ni wivu, haters, chuki, wazandiki, wafitini na wenye roho chafu.

    Mr. Mashaka ni msomi na mchumi yupo wall street-Mtanzanian peke kule, wewe unabepa mabox , shule hakuna, hoja zenye mantiki huna, sasa unafikiri wewe na mashaka ni sawa. Kafie mbali muache Mashaka mtu wa watu. Hata Jesus alichukiwa lakini alipendwa na wengi, hata Obma, Hata mandela alipata kura asilimia 70% alipogombea hakuna binadamu anaweza kupendwa na wote, hivyo siyo ajabu kwa mashaka, lakini ukweli ni kwamba watu wengi wanamkubali mashaka kwa hoja zake zenye mashiko na mantiki-kiingereza chake kama Obama vile, wewe umekaa ulaya hata kuandika article moja huwezi.
    mimi ni mdau wa Sweden, mashaka anijui na wala sijawahi toa comments kumsifia lakini napenda hoja zake. Bwana Mashaka ebu toa article nyingine sisi wadau tufaidi, vipi wall street na uchumi wa dunia vikoje? najua haya mambo anayaweza mashaka haters kazi zao ni box tu.

    ReplyDelete
  58. AnonymousMay 19, 2010

    Nyie karibia wote mmetoka nje ya mada. "Mashaka, Mashaka"! Utasema hiyo ndio mada yenyewe!

    Jibu ni moja tu!

    Ma-Civil Engineers waliotumika kijenga daraja la umoja kati ya Tanzania na Msumbiji! Baaas!

    Maana mtakubaliana nami kuwa lile daraja ni maridadi haswaaaaa! Na kwa jinsi lilivyojengwa kwa umahiri na jinsi lilivyo pana na imara, nadhani hata uwezekano wa ajali kutokea ni mdogo sana (Ee Mungu tuepushie, maana kuna haters najua wanaweza enda fanya ushirikina, ili tuu ajali zitokee pale, kwa madhumuni ya kuni-prove wrong).

    ReplyDelete
  59. AnonymousMay 19, 2010

    @ anynony Tarehe Wed May 19, 12:42:00 AM, YOU HAVE MADE MY DAY

    jamani mdada aliyetemwa anakaa houston, yeye ndo anayesambaza uongo dhidi ya mashaka. alidhia kapata shimola dhaabu, na sasa hivi haamini katemwa mwee,,,,. huyu demu nuksi na hasira zinampanda kusikia mashaka kaopoa mali mpya tena kali, msomi. mashaka kaa mbali naye anakutafuta na hasira kali kweli kwa sababu watu wanamcheka.hawezi kuamini kwamba angeachwa. Habari ndo hiyo, najua hapa siyo u-turn lakini mipasho muda mwingine muhimu. wewe nani ataoa mwanamke anayeshinda kwenye ma klabu na mabaa?? kachafua jina la kijana wa watu kwenye ma facebook, blogs, yaani basi tu. yeye angejuwa kwamba clock inatiki tu. mashaka juu, juu juu zaidi. napenda atiko zake bwana, kwani jamaa amaetulia, wivu utakuua mwanamke weye, hata mie mdemu si alinambia kwamba mashaka kaanzisha blogu kumutukana kumbe ni yeye ndo kaanzisha blgou yenye tena kutumia jina la rafiki yake, jamani wanawake tunashida aisee,,. Misupu ilove you,,,, I love this BLOGGGGGGGGGGGG
    imemaliza stress zangu kwa leo

    ReplyDelete
  60. AnonymousMay 19, 2010

    ANKAL, NANI MAARUFU TANZANIA KAMA JOHN MASHAKA KUSEMA KWELI???
    NACHEKA NAKUFA DUHHHH HII, KALI, EMBU PELEKNI HII MADA U-TURN

    ReplyDelete
  61. PETER NALITOLELAMay 19, 2010

    MIMI KUANZIA LEO NIMEAMINI YA KWAMBA MTUME NABII YOHHANA MASHAKA NI GENIUS KWELI KAMA WADAU WENGINE WANAVYOSEMAGA.ALICHOFANYA MASHAKA NI KULETA PICHA NA SENTENSI NDOGO, KWANI KILA SIKU HIZI PICHA ZA AJALI ZINAWEKWA HUMU, LAKINI HATUNA REAKSHENI KAMA HII. MTUME YOHANNA AMEWEZA KUCHOKONOA FIKRA. MATOKEO YAKE MBUZI, SWALA PUNDAMILIA, NGURUWE NA NGIRI WA KUTOKA TANZANIA WAKAANZA HOO MASHAKA HILI MASHAKA LILE WAKATOKA NJE YA MADA. KAMA NINGEKUWA MHADHIRI KULE MUZUMBE, NINGEWAPA FELI MTIHANI. HAWA WATU VICHWA VYAO VIMEJAA MAKAMASI SANA NDO MAANA HAWAFIKIRI. SASA IKIWA HAMUWEZI KUELEWA MASWALA MADOGO KAMA HAYA, NONDOZZ ZA NABII ZA KIUCHUMI ALIZOMA CHUO CHETU CHA MUZUMBE CHA KULE MOLOGOLO MTAELEWAJE? BWANA MUZUMBE IMETOA JINIAS WENGI SANA, MR. JK, ANKAL NA MZEE KANUMBA NA MTUME YOHANNA WA WOLSTRITI AMBAYE NDIYE RAIS WA TANZANIA 2015

    ReplyDelete
  62. AnonymousMay 19, 2010

    kwanza asante sana ankal kwa kutupa nafasi hii nzuri kujadili maswala muhimu. naomba nikosoe wachangiaji kadhaa humu hasa nikianza na
    @ anony Tue May 18, 05:49:00 PM
    sidhani kwamba mashaka john analipwa $5.75 kwa saa, kwa sababu gani, mwaka 2008 nikiwa naongea narafiki yangu mmoja hapa marekani ambaye alikuwa akifanya kazi kwenye kampuni inayotwa Goldman Sachs. Huyu kijana ana umri wa miaka 29 na alikuwa analipwa USD 350,000 kwa mwaka nje ya marupurupu. Kwa maana hiyo namaanisha ya kwamba Investment Bankers ndio watu wanaolipwa sana zaidi ya profeshonal players. Mishaara ya hawa jamaa inaanzia USD $250,000 hadi USD $475,000 pia inategemea cheo chako.Kwa hiyo wanapoongezea bonus, inaweza kuwa hata mara mbili au mara tatu ya mshaara wa mtu, ila kodi wanayolipa ni kubwa sana kulinganisha na mtu wa kawaida, kuna baadhi yao hao vijana wadogo wanaoopoa mamilioni. ukiangalia NY, wanaoendesha magari mazuri sana ni hao bankers. Wanakatwa kodi ya mapato 37% na Bonues 45% ila hiyo hela bado ni nyingi sana. Mabenki makubwa kama GoldMan Sach, JP Morgan, Bank of America, Wachovia na CITI wanatoa mishaara mikubwa sana. Hawa jamaa hela zao siyo kwamba wanaziokota, hapana wanafanya kazi kweli. Kwa wastani wanafanya kazi masaaa karibia 13 kwa siku. Hawakai nyumbani, mara nyingi ni watu wanaozunguka ndani na nje ya nchi na hata hizo hela nyingi wanazolipwa hawaoni faida zake kwa maana ni watu ambao wako kwenye stress muda wote na ni walevi mno kutokana na kazi hasa kushugulika na dili kubwa zenye thamani ya mamimillioni, ila kama unataka kula hela zake. Kwa maana hiyo sioni shida mashaka kwenda tanzania kila mara, mfuko unamruhusu. Hata kama hana Range-rover Vogue, sidhani kwamba anashindwa, nadhani hataki tu. Swla la ranchi la billioni hilo silijui na sidhani anaweza kushindwa au ni hela za wizi, hizo ni hela zake na jasho lake. eniwei, kwa kifupi sidhani analipwa Dola $5.75 kwa saa unless nimednganyika, ila kama ni hio hela, asingeweza hata kwenda na kurudi kwa sababu nauli ni kubwa na maisha ya marekani kwa hela hiyo hauwezi kutunza hata $100 kwa mwezi

    Mdau
    NEW-YORK, NY

    ReplyDelete
  63. AnonymousMay 19, 2010

    mdada anayesemwa hata mie namjua, na ninajua nikiandika jina lake michuzi atabania.hizo habari hata na mie nimezisikia, mtu hakutaki kwa nini umng'anga'ie na kumchafua jina??? huyu dada ni mwongo sana alafu mzushi kweli, u need 2 grow up tabia mbovu kueneza ujinga kwa mtu asiye na taimu na wewe. sasa yeye ana ubavu gani kujilinganisha na mashaka? watu wengine bwana. mtu mzima kazi ni ugomvi na watu, wewe mtu mwenye akili timamu kwa nini hata wanaume wanaotoka naye hawataki waonekane naye? hata kama ningekuwa mashaka ningemtosa,, heti hasira, hasira makalio yangu mjinga tu na wivu wa kitoto, si ni mrembo mbona anakznia mtu ambaye hamtaki,kwenda zako ukachambe wazee, kudadadeki habari ndo hiyo

    ReplyDelete
  64. AnonymousMay 19, 2010

    jamani, jamani jamani, sasa ajali za barabarani zinaingilianje na kuanza kujadili maisha binafsi ya mtu, peopple?
    sentnsi za mashaka hazizidi mbili lakini maisha yake binafsi imezidi kila kitu, mwacheni kijana wa watu
    mashaka baba wala usikate tamaa. huma wa kitanzania upo nyuma yako, wanaokupenda ni wengi kuliko hii mifisadi ya kiitikadi

    ReplyDelete
  65. AnonymousMay 19, 2010

    SASA MASHAKA KWA VILE UNAKUJA TZ KILA MARA INABIDI UWE MWANGALIFU SANA. WALIOMFANYIA HASHEEM YANAWEZA KUKUTOKEA NA HASHEEM ASIPOCHUNGA T. I. D ATAMLOGA
    AU WATAKUFUATA HUKO BARABARANI NA KAMERA YAKO WAKUHACHIE LORI KUTOKA MLIMANI UFE USIPOTEGEMEA AU HATA KABLA HAUJAWONA WANAO

    AU T. I .D ATAKULOGA NA WEWE
    xoxo

    ReplyDelete
  66. MchunguziMay 19, 2010

    Huyo Joni Mashaka mwenyewe kachapia.

    Hiyo p[icha ya chini hapo haikatazi kuovateki bali inaruhusu kuovateki pande zote.

    Angalieni vizuri ni vipande vipande hiyo haijaunganika ila ndo viko dabo dabo.

    ReplyDelete
  67. AnonymousMay 19, 2010

    kwani huyu mashaka ni Issa Michizi ama labda mnieleweshe

    ReplyDelete
  68. AnonymousMay 19, 2010

    1. BARABARA NI NDOGO: TUTAKIWA TUWE NA BARABARA MBILI ZA KWENDA NA MBILI ZA KURUDI KAMA TUNAUWEZA KWA BARABARA ZA KWENDA MIKOANI ZIWE SITA(TATU KWENDA NA TATU KURUDI) NA PIA KATIKATI YA BARABARA MBILI KUWE NA UKUTA KIDOGO ILI KUZUIA MAGARI KAMA YANAOVATEKU YASIENDA UPANDE WA BILI NA WATU WANAOFUKA BARABARA WASIFUKE KILA MAHALI.
    2 LESENI: ZINATOKA BILA MPANGILIO MAANA UKITOA KITU KIGODO UNALETEWA LESENI YAKO NYUMBANI BILA YA KUFANYIA TEST.
    3.DEREVA: WENGI HAWANA LESENI NA PIA HAWAJUA SHERIA ZA BARABARA NA HII NDIO MAANA UNAONA WANAKIMBIZA MAGARI BILA AU KUOVATEKI BILA SABABU.
    POLISI BARABARA (TRAFIKI) WANAPOKEA HONGO KUPITA KISASI MAGARI MENGI YAMEJAZA ABIRIA, HAYANA INSURANCE, KWA JUMLA MABOVU NA HAYATAKIWI KUWA BARABARA ILA YANARUSKIWA KWA SABABU KITU KIDOGO MAANA MZARAU MUIBA....
    SERAKARI: SERAKARI PIA HAIJALI MPAKA SASA HIVI AJALI ZOTE HIZI HAKUNA HATA KIONGOZI MMOJA ALISEMA KITU HATA VYAMA VYA UPINZANI WAPO KIMYA JE VIONGOZI MNAPOKWENDA MIKOANI NA TUMIA NINI ? MAANA BARABARA NDIO HIZI NA MABUSI NA MAGARI MENGINE MNAYAONA KILA SIKU HATUA GANI MMECHUKUA KWA JAMII YETU.
    NINA MENGI ILA NAONA NIWACHE HAPA
    MUNGU IBARIKI TANZANIA NA WATU WAKE...AMEN.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...