Rais wa Msumbiji Armando Guebuza akiongea na waandishi wa habari ambao hawapo pichani wakati wa mkutano wa jukwaa la kujadili uchumi wa dunia kwa Afrika unaondelea Jijini Dar Rais Mstaafu wa Tanzania Benjamin Mkapa akitoa ufafanuzi wa hoja za waandishi wa habari kwenye mkutano wa kimataifa wa kujadili uchumi wa dunia kwa Bara la Afrika jijini Dar. Kulia kwake ni Waziri Mkuu wa Eithiopia Meresi Zenawi.
Makamu wa Rais Dk. Ali Mohamed Shein na Naibu Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Dk. Asha-Rose Migiro wakifatilia mada kwenye mkutano wa jukwaa la kujadili uchumi wa dunia kwa Afrika unaondelea Jijini Dar leo. Waziri Mkuu wa Kenya Raila Odinga wa kwanza kushoto akiongea na waandishi wa habari kwenye mkutano wa jukwaa la kujadili uchumi wa dunia kwa Afrika (World Economic Forum) unaondelea Jijini Dar-Es-Salaam. Katikati ni Waziri wa Biashara na Kilimo na usafirishaji na wa kwanza kulia ni Joe Nyagah ambaye ni Waziri wa maendeleo ya ushirika.
Naibu Waziri Mkuu wa Zimbabwe Profesa Arthur Mutambara akisisitiza jambo kwenye mkutano na waandishi wa habari kwenye mkutano wa jukwaa la kujadili uchumi wa dunia kwa Afrika unaoendelea katika ukumbi wa Mlimani City Jijini Dar Waziri wa nchi ofisi ya Makamu wa Rais (Mazingira) Dk. Batlida Burian akizungumza na Rais Mstaafu wa Msumbiji Joachim Chisano wakati wa mkutano wa jukwaa la kujadili uchumi wa dunia kwa afrika unaoendelea Jijini Dar leo. Pembeni kushoto kwa Rais Chisano ni maafisa wanaohudhuria mkutano huo.







Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 17 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 06, 2010

    wadau hebu maprofesa wa uchumi waluwaaliki ?

    ReplyDelete
  2. AnonymousMay 06, 2010

    A promising future for Africa, very encouraging indeeed. We should be doing this more often, strategizing. A breakthrough to our economies will soon be a reality.

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 06, 2010

    Honourable Mkapa, you are looking very smart indeed.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 06, 2010

    kwa kuitangaza nchi yetu na kuiwezesha kikwete amefanikiwa sana,now tz ni moja ya nchi inayoheshimika sana kwa africa.kwa viongozi wa africa na nje ya africa.katikati ya miaka 80 mpaka 2005 tz ilipoteza umaarufu wake na heshima kwa nchi za africa,lakini sasa naona inapewa nafasi nyingi sana.hii ni moja ya matunda ya safari za jk,japo kuna watu kila kitu kupinga tuwao,ukangalia kama olmpik china waliichagua tz peke yake kupitisha mnara wake,george bush alitumia siku 5 kati ya saba alizokaa africa,na kuja na mikataba ya nguvu ya millenium challenge,rais wa china pia alipita hapa na kuacha matunda ya kituo cha mikutano cha j.k.nyerere kinachojengwa.mambo ni mengi tukiyataja yote tutajaza blog ya misupu.sema jamaa wa mtaa wa pili hawataki kuona hayo,wanaangalia weakness tu za JK.msindwe na mlege.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 06, 2010

    tunaomba video ya Beni tumsikilize akitoa hoja..twataka jua km kaacha hasira pindi the guy face a tough question..michu please let us have such thrill...

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 07, 2010

    Jembe la mkno juu
    ufagiaji wa barabara kwa mkono juu
    uchumi bila sayansi na teknolojia ni kujidanganya!
    karne ya sasa tunahitaji vitendea kazi vya kishandani
    kama tunashindwa kushindana kusafisha barabara na kulima nyanya na vitunguu tutaweza wapi kushindana na watu wanaochapa kazi masaa 24 kwa kutumia mashine,akili, na mitaji mikubwa?
    benki zinafanya nini kama mtu anashindwa kukopa na kununua mashine za kufanya usafi wa barabara?
    Viongozi punguzeni siasa nyingi na angalineni zaidi hali halisi na matatizo ya mlala hoi, huyo ndiye anabeba taswira ya mambo yote.

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 07, 2010

    big ben not only smart but confident and good in upstair

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 07, 2010

    KUNA WASAFIRI NA WABEBA MABULI.......WENZETU WATAKUWA WASAFIRI NA WATANZANIA TUTAKUWA WABEBA MABULI.

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 07, 2010

    Tuwekeeni Ben Mkapa tumsikilize naye.

    Tumewasikia akina Mwinyi, Asharose, Shein, tumeshamwona Batilda. Inatosha

    ReplyDelete
  10. AnonymousMay 07, 2010

    mamaaa asha-rose migiro safi sana na karibu home!!i was asking myself have yu been invited?ooh yes there yu are my lady!!
    keep the good work n representation

    nkapa upo baba?

    tungepata clips za maongezi ya
    1.asha-rose kama aliongea
    2.mkapa
    3.odinga
    4.armando guebuza
    5.ivone chakachaka

    tafadhali michuzi

    ReplyDelete
  11. AnonymousMay 07, 2010

    WEWE THU. MAY 06, 11:55:00 NANI KAKUAMBIA KUZAA WATOTO NI MAFANIKIO? MAFANIKIO NI JINSI GANI UTAKAVYOWATUNZA NA KUWAENDELEZA WAFANIKIWE KATIKA MAISHA. HICHO KITUO CHA MIKUTANO CHA J.K. NYERERE KIMEBADILISHA NINI MAISHA YA MTANZANIA? BUSH AMEBADILISHA NINI MAISHA YA MTANZANIA ANGALAU JIMMY CARTER ALIWEZA KUBADILISHA MAISHA YA MTANZANIA KWA MRADI WAKE WA KILIMO WA GLOBAL 2000 AMBAO KAMA KAWAIDA YETU BAADAE TUKAUTELEKEZA. MIKATABA SI MAFANIKIO BALI MAFANIKIO NI JINSI GANI MIKATABA HIYO INTAKAVYOTEKELEZWA KWA UFANISI NA KUPUNGUZA UGUMU WA MAISHA KWA MWANANCHI. WEWE ULIVYOMFINYU WA MAWAZO KWAKO TISHETI NA KOFIA NDIO MAFANIKIO ULIYOYAPATA.

    ReplyDelete
  12. AnonymousMay 07, 2010

    Kazi kweli. Mimi nampongeza Kikwete kwa International interaction, GOOD! Lakini mambo humu ndani ya nchi sielewi anachofanya ni nini. Nafikiri nchi inaenda kwa acceleration ya mavuno ya brother wa taifa Ben. Mkapa maana alipokea nchi hii haina pesa kabisa! nakumbuka serikali (wizara na taasisi) ilikuwa jambo la kawaida kusema haina hela, ilifika wakati wafanyabiashara wakubwa wakawa wanaikopesha serikali. Lakini Mkapa alikusanya mapato vizuri akadhibiti mfumuko wa bei vizuri maisha yakawa ahueni, BAHATI mbaya akajisahau watu wakawa wanachota pesa na wakasema 'VIJISENTI' na yeye akacho kidogo. Lakini leo bei za kila kitu JUUUUUUUU!!! Watendaji wakuu kama mawaziri hawaelewi wanachokifanya. Pres. Kikwete angalia vizuri humu NDANI kaka!!!

    ReplyDelete
  13. AnonymousMay 07, 2010

    Honourable Meresi Zenawi you also look good.

    ReplyDelete
  14. kangoma k.May 07, 2010

    next time mikutano muhimu kama hii ni bora kuwahusisha vijana wengi ambao ni viongozi wa baadae wanaoweza kutekeleza hayo yanayoongelewa kuliko kujaza maraisi wa zamani na wazee ambao wengi hawana nafasi tena ya kuyatekeleza!!!!nilimuona raisi wa zamani wa msumbiji ndugu chisano akimwaga usingizi wa nguvu kwa vile kinachoongelewa yeye hana nafasi nacho tena!!ndo maana hata kenya hawakumleta Mzee MOI!!!!hapo kwetu niliona mawaziri wa zamani ambao wakati wao hawakuweza kubuni mbinu zozote za ku-unlock the so called African potential so is useless for them to be on the front seats in such a crucial discussion on Africa's economic and social destination. Is a colossal waste of opportunity for young leaders of Africa.

    ReplyDelete
  15. wewe Fri May 07, 10:28:00 AM: mfinyu wa mawazo ni wewe na si mwingine.Safari za JK zimeisaidia sana nchi yetu. Kwa mfano, umedai kwamba hamna kitu bush ametufanyia, nenda ukasome kuhusu millenium challenge account. Kwenye huo mkataba bush katupatia zaidi ya $600 milioni. Hizo pesa ndio zinajenga barabara ya tanga-horohoro, pia Kuna barabara nyingine tanzania bara itaanza kujengwa sema nimeisahau. Zanzibar nao wamepata barabara. Na bado kuna miradi mingine ambayo inafanywa na hizo pesa. Barabara zikijengwa watu wanaweza kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi zaidi na matokeo yake bei za vyakula n.k zitashuka, huoni kwamba mtanzania kashinda hapo? Haya, umesema ukumbi wa mikutano wa j.k nyerere hauna faida kwetu? Siku hizi kuna kitu kinaitwa utalii wa mikutano (conference tourism). Watu wakichagua kufanya mikutano yao tanzania, watanzania wengi watapata kazi mahotelini, kwenye ukulima maana mahitaji ya chakula yataongezeka, hazina yetu ya fedha za kigeni itaongezeka. Pia, kadri watu wanavyozidi kuja tanzania kwenye mikutano, tunazidi kuitangaza nchi yetu, wakimaliza mikutano wanaweza wakaenda kutalii mbugani, au wakaenda zanzibar. Kwa hivyo usije tu hapa kwenye blog na kutoa maoni bila kufikiria kwa kina. Na hayo ni matunda ya safari za china na USA pekee, bado hatujaongea safari zake zingine. THU. MAY 06, 11:55:00 yuko sahihi kabisa, ni kweli kwamba kuna sehemu zingine JK anateleza (mfano TUCTA), lakini kuna mazuri ambayo amefanya na inastahili tumpe pongezi.

    ReplyDelete
  16. AnonymousMay 07, 2010

    Kaka Michuzi,
    Kuna tetesi kuwa gharama za huu mkutano pamoja na washiriki zimefadhiliwa na walipa kodi wa Tanzania kama uleee wa wakati ule wa "Sullivan". Kama ni kweli sina wasiwasi kuwa nchi itakuwa imevuna hasara na madeni badala ya faida kama walivyo wenzetu ambao wamewahi kufadhili mikutano mingi ya WEF.
    ....Tanzania iko kwa usingizi mnono katika mambo haya. this kind of conference is supposed to be a big deal for Tanzania revenue collection and not irresponsible government expenditures and source of increasing public debt...popularity is not a big deal if we gained nothing......just my personal opinion.

    ReplyDelete
  17. AnonymousMay 07, 2010

    Kuna mdau hapo juu anataka kusikiliza clip ya Yvonne Chakachaka.

    Hahahaa duh hivi bado hujaichoka single ya Malaria?? ilishafanyiwa collable za kutosha i think inatosha.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...