Msaada wa materials
Habari za kazi kaka michuzi.Mimi naitwa zamda ni mwanafunzi, nilikuwa naomba nitumie blog yako kuomba msaada wa material au doccuments za biofuels hasa guideline ya biofuel investment maana nimejaribu kuitafuta lakini sijabahatika kuipata,nimepiga simu wizara ya kilimo na wizara ya nishati lakini sikuweza kupata draft yoyote.
Nimeomba draft kwa kuwa Tanzania bado hakuna policy yoyote inayohusika na uwekezaji wa biofuel zaidi ya hiyo guideline hadi hapo watakapokuwa na policy. Ninaomba kwa yoyote ambae anaweza kuwa na hiyo guideline anisaidie ili niweze kukamilisha report yangu ya mwisho.
Nitashuluru sana kwa msaada wenu.Naomba anaependa kunisaidia awasiliane nami kwa email yangu:
zamdamandari@gmx.com
Asanteni sana.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 9 mpaka sasa

  1. AnonymousMay 20, 2010

    Zamda kwanza pole sana kwa shule.
    Mimi naitwa Abdul Ali. Hayo material ninayo. Issue ni jinsi ya kunipata. Anyway mimi ninapatikana Kijitonyama, ukifika pale Break point-Sayansi uliza kwa mzee Ali Mkubwa watakuelekeza kwangu nitakupa hayo material tu aunt.

    ReplyDelete
  2. Tembelea blog yangu na utajifunza kuhusu jatropha (mbono) kama una swali tuwasiliane kupitia mail yangu

    ReplyDelete
  3. AnonymousMay 20, 2010

    Kaka Abdul mbona unambania dada Zamda...email amekupa sasa si umtumie kwa email mpaka tena aje breakpont..hata kama ni paper work scan utume..utabarikiwa.

    ReplyDelete
  4. AnonymousMay 20, 2010

    MMH, WEWE ZAMDA UKIENDA HAPO KIJITONYAMA KWA HUYO ABDALA USIENDE PEKE YAKO, SHAURI YAKO.

    ReplyDelete
  5. AnonymousMay 20, 2010

    Mmh, misaada mingine inaonyesha dalili za masharti humu. Mhusika katoa anuani pepe kama unataka kumsaidia, wewe unataka akufuate nyumbani sijui Break Point sijui Komakoma.

    ReplyDelete
  6. AnonymousMay 21, 2010

    Mwalimu Nyerere aliwahi kuwaambia wahisani kuwa tunakubali misaada lakini "with no strings attached", yaani bila masharti. Mimi pia ni Abdul (lakini si huyo wa breakpoint kijitonyama).

    ReplyDelete
  7. AnonymousMay 21, 2010

    Mwalimu Nyerere aliwahi kuwaambia wahisani kuwa tunakubali misaada lakini "with no strings attached", yaani bila masharti. Mimi pia ni Abdul (lakini si huyo wa breakpoint kijitonyama).

    ReplyDelete
  8. AnonymousMay 21, 2010

    wee 12:53:00pm nani kasema waislamu hapa??

    acha jazba wewe!!tumia ubongo

    matope

    ReplyDelete
  9. AnonymousMay 21, 2010

    Matope, nadhani hukunielewa kabisa. Nilipomnukuu Mwalimu nilikuwa na maana ya kuwa ukitaka kumsaidia mtu usimpe mahsrti. Huyo dada katoa e-mail yake lakini mdau (ambae ni mwajina wangu, yaani wote tunaitwa Abdu) akaanza kumwelekeza nyumbani kwake. Nina maana mimi pia ni Abdul lakini siye huyo wa kijitonyama, umenielewa sasa??? Sikutaja suala la dini. soma na uelewe kabla ya kukurupuka kwa jazba. Mimi Abdul lakini siye wa break point.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...