Naibu Meya wa Ilala Mstahiki Jerry Silaa ( wa tatu shoto) akiwa Washington DC, Marekani, leo anakohudhuria mkutano wa "Innovative cities;global dialogue" wenye mada ya "Cities as engines of economic growth;enhancing sub-national investment climate" (BOFYA HAPA) ulioandaliwa na benki ya dunia. Pamoja na mambo mengine Mh. Silaa ameomba Benki ya Dunia kuendelea kutoa fedha kuboresha makazi duni kwa miradi ya miji na majiji.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. AnonymousJune 23, 2010

    Tokea ukonga shule ya msingi,pugu secondary o level,jitegemee secondary a level,University of Dar es salaam na mpaka sasa hivi umeukwaa UMEYA safi sana jerry ila chonde ndugu yangu usitusahau sisi wananchi yako wa Gongolamboto mwisho wa lami.maana tokea umepata udiwani na huku ukahama kabisa dahh.
    Mdau-Ukerewe!!!

    ReplyDelete
  2. AnonymousJune 23, 2010

    Ok
    Mdau Mbije,A

    ReplyDelete
  3. AnonymousJune 23, 2010

    we mdau-ukerewe acha kutuzingua humu.
    Ktk madiwani wanaojitahid bongo Dogo Jerry anaongoza sanaaa tu.si huku kwetu uswazi ndio tunamfahamu sana achana na hizo historia zako za kila siku oooh..kasoma hapa kasom hapa,,so what?? umeulizwa?? mbona hizo kila mtu anajua, hata akitaka kujua zaidi atazipataa mtandaoni. Kwanza unadai upo ukerewe..so ya Goms ya nini..tuachie wenyewe.

    Jerry keep it UP!! mtu wetu ,ila chochonde usitangaze NIA kwenda mjengoni bado tuna kuhitaji sana G'mboto.

    Mdau-Gogolamboto

    ReplyDelete
  4. AnonymousJune 24, 2010

    we mdau wa gongolamboto 02:38:00pm.mpumbavu kabisa wewe na hujui chochote sasa mimi kuongerea wasifu wa jerry kinakuuma nini.sasa kwa taarifa yako huyo jerry unajifanya wamfahamu kumbe ziro kabisa.na mimi kuishi kwangu UKerewe wewe kunakuwashia nini mijitu mingine bwana ovyooo na wewe kama unakinyongo tafuta safari ya ukerewe basi sio kubwabwaja tuu.halafu kaka MICHUZI micoments mingine ya wapumbavu kama hawa usiwe unaiweka mtandaoni alahaaaa.Kazi njema kaka MICHUZI.
    Mdau-Ukerewe!!!

    ReplyDelete
  5. AnonymousJune 24, 2010

    pamoja na yote Jerry, chonde chonde barabara karibu tunazama!

    ReplyDelete
  6. AnonymousJune 24, 2010

    Kwanza nimpongeze Bw. Jerry kwa hatua aliyofikia, kwani sasa yupo juu kama vijana wenzie wanavyosema. Ningependa nimkumbushe kuwa hapo alipofika ni kwa juhudi zake binafsi na hasa wananchi wa Kata ya Ukonga waliompa ridhaa ya kuwa Diwani wao. Inasikitisha pale unapofika Ukonga-Mombasa unapata KICHEFU CHEFU barabara za kwenda pembezoni zilivyombovu!! Sijawahi kusikia akilizungumzia kwa dhati, zaidi ya yeye binafsi kujipalilia kwa kwenda mbele na kusahau waliomvusha. NI HAYO TU, SIDHANI KAMA UTAKUWA NA SULUHISHO NA HILI UMESHACHELEWA UCHAGUZI NI KESHO TUNAANGALIA MBADALA.

    ReplyDelete
  7. AnonymousJune 24, 2010

    Mdau-Ukwere mshamba sana,

    Simply, i can say u'dont know wat ur talkin abt...better kip quety!

    Jerry WS, don't be dispointed with empty minds like this guy. we appreciate wat ur doing..just kaza buti kaka.

    Mdau-Pugu

    ReplyDelete
  8. AnonymousJune 24, 2010

    wewe mdau wa Pugu ndo mshamba kabisa wewe na hujui chochote.its you who got mind empted,,,rubbish kabisa wewe ubabaishaji mwingi tu huna lolote.Angalia maisha yako wewe usitie watu kichefuchefu.hapa tuko katika blogu ya ya jamii kutoa MAONI na sio malumbano.Asante sana kaka MICHUZI.kazi njema!!!
    Mdau-Ukerewe!!!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...