Miss temeke katika mazoezi ya mwisho mwisho.
Picha na habari na Jane John

Mwandaaji wa miss TEMEKE BEN KISAKA wa BMP COMPANY ametangaza zawadi za washindi katika shindano hilo. Amesema mrembo atakayetwaa taji la miss temeke atajinyakulia shilingi milioni moja na nusu, mshindi wa pili shilingi milioni moja ,mshindi wa tatu laki nane na mshindi wa nne na tano watapata laki tatu wakati waliobaki wote watapata laki moja na nusu kwa kila mtu.

Shindano hilo imnafanyika leo katika ukumbi wa TTC CHANG'OMBE na litapambwa na burudani kutoka bendi ya TWANGA PEPETA na B BENDI ya BANANA ZORRO.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 4 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 09, 2010

    Sasa huyu msela hapo anajiita nani..mwanaume au..kwa nn kama watanzania mnapenda sana umiss msitafute watahini wakike basi...disgusting

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 09, 2010

    ukitaka kujua nchi fulani inaelekea kuanguka/defalt ni tanzania...sijawahi kuona nchi yeyote inayokuwa na ma miss kila sehemu,kila siku utasikia miss ilala,ubungo,etc kesho miss ikulu sijui?
    hivi watanzania tunamatatizo gani?
    hivi tulishakoswa kazi kabisa na tumebakiza tu mambo ya umiss?
    Nionavyo taifa hili linaelekea kuanguka kabisa.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 09, 2010

    michuzi ushauri wa bure anzisha blog nyingine spesho kwa ajili ya mamiss maana vimezidi umezipa kipaumbele sana hizi habari za mamiss utadhani nchi yetu haina mambo mengine ya msingi kwanza haya mashindano sijui yana faida gani ya jumla kwa nchi

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 10, 2010

    jamani chukueni hizi sheree za umiss kama ajira. kwa hivi sasa watu wengi hawana ajira so akuna ubaya kutengeneza pesa kwa kutumia umiss. vingine pia huu umiss ni entertainment. tafadhali michuzi endelea kutuonyesha hizi picha za mamiss. picha zao zinapamba globu yako.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...