Ofisi za Global publishers zikiwa nyang'anyang'a

Usiku wa kuamkia jana ofisi za Global Publishers zilivamiwa! Mara baada ya uvamizi huo walimteka mlinzi na kumfunga kamba kisha kuondoka naye na kwenda kumtupa maeneo ya kurasini Temeke jijini Dar es Salaam hata hivyo askari huyo yuko chini ya ulinzi anaisaidia polisi.
Inasemekana kulikuwa na makundi mawili ya majambazi waliokadiriwa kufika ishirini, ambapo kundi la kwanza liliondoka na mlinzi huyo ambaye alifungwa plasta mdomoni na kamba mikononi na miguuni, kisha kundi la pili lilivunja mlango na kuingia ndani ya news
room.


Habari zinasema walipoingia ndani ya news room walipekua na kuvunja droo kadhaa na kutupatupa vitu vingi ikionesha kulikuwa kuna kitu au nyaraka fulani waliyokuwa wakitafuta, kwani hakuna hata kompyuta moja iliyoibwa wala kuguswa! Zaidi walichukua TV moja ndogo ya flat screen, iliyokuwa reception kwa sababu wanazozijua wenyewe na kuondoka nayo.

"Ni jambo la kushangaza kwa kweli na kumshukuru Mungu kwa kutuepusha na usumbufu na hasara ambayo tungeipata kama wangebeba kompyuta", afisa wa chombo hicho cha habari anasema.
"Tumeona ni bora tuwafahamishe wasomaji wetu wapendwa juu ya jambo hili ili muweze kujua kilichotokea siku ya leo ambayo imetufungua macho na masikio na kutufanya tuamue kuchukua hatua madhubuti ya kuimarisha ulinzi na usalama wa kampuni yetu", aliongezea.
Kwa picha na habari zaidi

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 15 mpaka sasa

  1. AnonymousJuly 07, 2010

    huyo mtaalam wa fingerprints mbona hajavaa gloves?

    ReplyDelete
  2. AnonymousJuly 07, 2010

    Pole sana mithupu,hawana lolote km bao umeshawapiga wakati wewe unatembea wao walikuwa wanatambaa na kujitia siku zinaganda sasa wewe unakimbia wanataka utembee km wao.Kaza buti achana nao na wasipoamka muda huu wataendelea kulala mpk siku ya kiama.

    ReplyDelete
  3. AnonymousJuly 07, 2010

    mh!!hapa ndo uwa najua kuna mafia hii nchi

    poleni global publisherz

    ReplyDelete
  4. AnonymousJuly 07, 2010

    ..Duh hao majambazi kiboko... hii habari imenikumbusha sana wale jamaa walioiba mifano ya Kombe la dunia kule Kwa madiba....

    of coz kupunguza hasira za kukosa hiz nyaraka nadhani wakaamua kuchukua tv.

    ReplyDelete
  5. AnonymousJuly 07, 2010

    Hata wana-sisiemu mnavamiwa, safari hii Global lazima mlikuwa na news za kutikisa jamii.

    Mdau
    Nairobi.

    ReplyDelete
  6. AnonymousJuly 07, 2010

    Ofisi kama hii ya Global inatakiwa iwe ina shift ya wafanyakazi wachache wa usiku, huku kukiwepo pia mlinzi, hiyo ndiyo dawa ya kuzuia 'udaku' kuporwa kirahisi toka ofisi za Global.

    Maana waliotumwa wakifika reception wataonwa na mlinzi+CCTV na kwa vile kuna staff wachache wa shift ya usiku basi patakuwa pagumu kunyakua habari 'nyeti' toka madroo ya wahariri.

    Mdau
    MagazetiYaUdaku-Ughaibuni

    ReplyDelete
  7. AnonymousJuly 07, 2010

    Watu wana usongo na story za udaku.

    ReplyDelete
  8. Sasa cha kushangaza baada ya nyie GP kuvamiwa, mbona mnaharibu "crime scene"? Sijui wamewaruhusu kivipi kwa haraka hivyo kuingia ndani ya jengo kabla ya hawa watu wa "forensic" kufanya kazi yao!
    Na huyo mtu wa "forensic" hana gloves wala magwanda ya plastic ya kutokui "contaminate" crime scene"?!
    yaani bado baongo mnafanya mambo kienjeji kabisa, ebu mwamngalie huyo jamaa na kabrashi, na kakopo kadogo kabisa ka majivu!
    Ni kichekesho na aibu!
    Tizameni CSI Miami, Vegas, New York na zingine muone wenzenu wanavyoishughulikia crime scene, na sio huo ujinga na usanii mnaoufanya!

    ReplyDelete
  9. AnonymousJuly 07, 2010

    Mnachukua finger prints wakati hakuna Database ya ku-search hizo prints na kugundua ni nani anaye husika! Jeshi la Polisi lipo nyuma sana na inaonesha kama lipo ktk karne ya 10 hivi! Mnashindwa kuvaa ata gloves! Ni aibu kubwa sana, yaani jeshi linaendeshwa kama Primary School!

    ReplyDelete
  10. AnonymousJuly 07, 2010

    Yani hata CCTV (KAMERA) jamani hamna. Acheni uzamani bwana, wala sio gharama. Hao jamaa mngewapata kiurahisi na kuweza jua kilichowafanya waje hapo na mengine mengi. Usikute wametumwa na mtu au kampuni flani, mngiweza jua hayo nakujua kwanini, kitu ambacho kinawaweka nyie ktk position ya kujua mko ktk mazingira gani na mjipange vipi. Haloo, mnaandika habari nzuuuuri kumbe hamuwezi fikiria vitu kama hivi, kuweni analytical in a bigger picture sio kwenye habari mnazoandika tu. Natamani nitukane, mmeniuzi kabisaaaaaaaaaa

    ReplyDelete
  11. AnonymousJuly 07, 2010

    kumbe ofice yenu yote hiyo inalala usiku ...mnatakiwa muwe na 24 hours shift..hata muigawanye kwa masaa 8 8 ...ndio maana mnasongoa hadithi kutwa kwa vile kazi hamna la kufanya.. weka wafanyakazi wachche kila shift..mkijaga huku hamwendi kutembelea vyombo vya habari muone jinsi wanavyowork work..hawalali wenzenu..

    ReplyDelete
  12. AnonymousJuly 07, 2010

    waosha vinywa wenzangu mlio changia kutoa madaa zenu mbona mna jazba sana jamani nyie eeh?
    poeni moto, cool down and cheel out,mnataka kuifananisha Tanzania nchi yetu tukufu na marekani,eti data basse za kuchukulia finger print hatuna,sijui haja vaa gloves sijui nini na nini, sasa mbona katika picha hii haionyeshi huyo jamaa aliye haribu crime scenery?

    uzushi mtupu na majungu ndo muwezayo na mdomo kaya, kama mnanaona tuko nyuma hebu saidiyeni nchi yenu mlioko huko majuu mbona hamfanyi hivyo domo kaya mkija katika website hii ya michuzi

    kuweni wastarabu kidogo na wekeni heshima huko huko kubaya vacation zenu mnakuja kila leo, mtu kwao na heshima hupewa kwao, huko uzunguni mnadhalilishwa mbona hamsemi kweli

    watu wanafanya kazi pesa zote zina ishia renti hata raha ya ulaya hamfaidi mkija nyumbani ndo mnajitia mabrother man na ma sister duu mchwara mchwara kwa kubeba maboksi au kupata makaratasi kwa vijizee vya kizungu na vijanajike na vijanadume vizima haya hamuoni kutembea na mababu zenu kwa karatasi ya kujia nyumbani

    wacheni hizo

    enzi ni chenu na heshimuni chenu, nchi yenu

    ReplyDelete
  13. AnonymousJuly 08, 2010

    hahahaha! wabeba box mnalo? huyo jamaa hapo juu kawapaka. ngoja waamke watakuja na jazba patakuwa hapatoshi!

    ReplyDelete
  14. AnonymousJuly 08, 2010

    Jamaa kawambia ukweli, watu kwa kuwa wako ulaya basi ni dharau tu. Mbona hayo yenu ya ulaya mabaya hamyasemi au mnadhani tuliopo huku hatujui? Watu kila siku Bongo mko nyuma bongo mko nyuma mlio mbele mmeleta mabadiliko gani sasa?

    ReplyDelete
  15. Mnaowaponda wasioenzi chao ebu niwaulize tuenzi kitu gani hapo? Hako kabrash au majivu? Au Tuenzi jinsi tusivyokua organised? Sio kwamba pesa hamna, pesa ipo ya kununulia hizo gloves, magwanda ya plastic, utepe wa kuonyesha neno police, n.k.
    Au ulitaka tuseme kwamba aise hawa watu wa forensic wako professional ile mbaya!
    Labda ulitaka tushauri mganga aje apiga ramli? Au Vitabu vya dini vije na watu wasomewe dua?
    Wabongo bwana?!

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...