DJ Emperor akiwajibika ghorofa ya Saba New Africa hotel enzi hizo
Haya DJs walikuwa, na bado ni watu muhimu katika shughuli za muziki Tanzania. Labda nikupe maelezo mafupi. Baada ya Biribi Discotheque kupumzika, akazuka kijana huyu, kwanza kwenye parties maeneo ya Upanga, na baadaye kuwa DJ maarufu aliyejulikana kama Dj Emperor, akiburudisha sana pale Motel Agip na kisha kuhamia ghorofa ya saba New Africa Hotel. Alifanya mambo makubwa Arusha pia. Wapenzi wa disco mnamkumbuka? na disko lake liliitwaje? Anauliza mwanamuziki nguli na mwana libeneke aliye juu katika tasnia ya muziki John Kitime a.k.a JFK. Kwa haya na mengi mengine katika muziki wa bolingo hebu mtembelee BOFYA HAPA

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. Hadj Drogba "mwana chelsea"July 17, 2010

    Huyo ni Big JOE Joseph kusaga enzi zake alipokuwa Dj na DISCO lake la mawingu ambalo baadae lilijigeuza na kuwa redio pendwa kwa sasa hapa bongo ikiitwa mawingu redio,mkidhungu unaweza kuiita REDIO CLOUDS a.k.a. REDIO YA WATU,na big JOE kwa sasa si DJ tena bali ni mkurugenzi wa REDIO hiyo pendwa.Hongera bwana JOE a.k.a. Big Boss,toka u dj mpaka ukurugenzi mzee pana hatua

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...