Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Seth Kamuhanda (kulia) akimkabidhi Kombe la Ubingwa wa michuano ya klabu Bingwa ya netiboli kwa nahodha wa JKT Mbweni, Esther Fanuel ‘Mayai’ baada ya kuifunga Jeshi Stars kwa magoli 44-42 katika mchezo wa fainali uliofanyika kwenye viwanja vya TCC, Chang’ombe, Dar es Salaam, leo.

Kutokana na ushindi huo JKT wameweza kutetea Ubingwa wao kwa mara ya pili mfululizo.Katika mchezo wa kutafuta mshindi wa tatu timu ya Polisi Morogoro walipata zawadi ya kombe dogo baada ya kuitandika Polisi Dar kwa magoli 44-41 na timu ya Jeshi Stars walipata zawadi ya kikombe baada ya kushika nafasi ya pili.
(Picha na Francis Dande wa Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...