Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete akimtambulisha mgombea ubunge wa Mafia kupitia CCM,Bw. Abdulkarim Shah.
Mwenyekiti wa Taasisi ya wanawake na Maendeleo (WAMA) ,Mama Salma Kikwete,akiongea na wanachama wa UWT Wilaya ya Mafia katika ziara ya siku moja kuwahamasisha wanachama wa umoja wa wanawake Tanzania kuwachagua wagombea wa CCM katika uchaguzi ujao.
Wanachama wa UWT Wilayani Mafia Mkoa wa Pwani wakimsikiliza Mwenyekiti wa Taasisi ya Wanawake na Maendeleo (WAMA) Mama Salma Kikwete hayupo pichani katika mkutano wake na wanachama hao kuhusu kuwahamasisha masuala ya Uchaguzi Mkuu ujao hapo Oktoka 31 mwaka huu.
(picha zote na Mwanakombo Jumaa-Globu ya Jamii)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 14 mpaka sasa

  1. MdanganyikaAugust 28, 2010

    Kaka Michuzi hivi JK ana wake wangapi?Na je ana watoto wangapi? Tunaomba pia na majina yao. Huyo ni rais wa nchi lakini hatujui wake zake ni wangapi wala watoto wake ni akina nani. Naomba msada juu ya hili mheshimiwa Michuzi.

    ReplyDelete
  2. MdanganyikaAugust 28, 2010

    Kaka Michuzi hivi JK ana wake wangapi?Na je ana watoto wangapi? Tunaomba pia na majina yao. Huyo ni rais wa nchi lakini hatujui wake zake ni wangapi wala watoto wake ni akina nani. Naomba msada juu ya hili mheshimiwa Michuzi.

    ReplyDelete
  3. Habari Yako ya kazi Ankal, Tumefrahishwa na kazi ya kampein unayoedleza katika blog yako ikiwa Ni Ushaidi tosha kwa Takukulu ya Kuwa Kuna Rushwa Inaendelea Kaika Kampeni, kwa majonizi ni thahiri umelipwa kufanya hivyo,ikiwa si ni wadau wa blog hii yako tunaonelea ni bora ungebadili jina badala ya michuzi kuwa CCM blog. Mwaka huu ikiwa uchaguzi utaendehswa kwa Haki,bila shaka wapinzani wako CHADEMA ndie atakeyongoza Nchi, Hatufraishwi na Hali inayendelea katika blog yako!Ahsante

    ReplyDelete
  4. Kwa stahili hii,maadili ya uandishi wa habari yanachezewa!
    Hahiitaji mtu makini kuona kuwa taarifa kuhusiana na kampeni zinazoendelea ni za upande mmoja. No fair play. Maana hapa naona kijani tu, wakati na vyama vingine vimeshazindua kampeni zao,mfano CUF na leo CHADEMA,lakini hatujaona lolote.
    Ankal tunahitaji kupata taarifa/sera za vyama na mwisho wa siku watanzania wachague viongozi wenye sera nzuri na sio kutuonyesha sare za kijani kila siku. Historia itawahukumu nyie waandishi wa habari.

    Nawasilisha,najua utabana kama kawaida yako,liwalo na liwe nimefikisha ujumbe.

    ReplyDelete
  5. Kinachhonishangaza mimi ni siasa za tanzania, hawa akina mama waume zao wanapokuwa ni wanasiasa wadogo bila vyeo huwa wako kimya na hawamo kwenye siasa lakini mara tu waume zao wanapopata vyeo vikubwa nao hujitokeza na kuwa wanasiasa wakuu, isitoshe na jumuia za vyama nazo huwamwagia vyeo katika hizo jumuia ilhali hukio nyuma hawakuwa active member at all. Mfano ni huo umoja wa akina mama ni kama vile imewekwa sheria mkuu wao ni lazima awe mke wa rais.

    Mbona hatuoni waume wa wanasiasa wa kike kuruka kwenye majukwaa na kuanza kuhubiri siasa wake zao wanapopata vyeo?

    Mtanzani wa kuzaliwa

    ReplyDelete
  6. Michu hivi vyeo vingine katika kampeni inabidi visitajwe, sasa hapa WAMA inapigia kampeni CCM? Maana nauhakika wanaotoa misaada WAMA wanajua haikufungamana na chama. inabidi tujue kutofautisha hizi kofia (vilemba in this case) vya madaraka. Mimi nafikiri kidemokrasia ungemtambulisha kama Mke wa Mgombea Urais kupitia CCM nakuendelea kutaja vyeo vyake vya ndani ya chama.

    ReplyDelete
  7. Kaka mbona chadema umewasahau na wapo jangwani leo, na hamna habari za cuf za jana. Tunaomba uwe na usawa

    ReplyDelete
  8. Anon wa Sat Aug 28, 06:09:00 AM Hehehehehehehe tafadhali bwani wewe tafashzali njomba mbona unafukunyula yaliyopooza hehehehehe tupo pamoja TUNAOMBA JIBU
    Wadau wengine wala msiumize vichwa maadili yachezewe mara ngapi jibu liwe Oktoba panapo karatasi MPAKA KIELEWEKE
    michuzi blog aka CCMBlog

    ReplyDelete
  9. oooooooooooohhhh

    ReplyDelete
  10. michuzi unatuzingua

    ReplyDelete
  11. Nkonongwa, Safarini Kilwa KivinjeAugust 29, 2010

    Nasikia huyu mgombea ubunge wa Mafia, Abdulkarim Shah a.k.a Buji alimsambaratisha vibaya sana KIMBAU mkubwa katika uchaguzi uliopitana safari hii amewasambaratisha KIMBAU na MTOTO wake. Kila la kheri Mr. BUJI

    ReplyDelete
  12. SI mfungue blogu zenu jamani tumeshawachoka kwa kulalamika, kiila siku kazi yenu kulalamika. Hivi mbona wengi wenu mnaolalamika humu mna blogu zenu wekeni picha humo au hazitambaliwi!

    ReplyDelete
  13. mdau wa hapo juu(Anonymous 11.00) umechemsha, naomba michuzi ingilia kati ili uonyeshe hata kinafiki kuwa hupendelei pande kama unavyosema kila siku. hii blog Michuzi umeiita ya Jamii (watanzania wote) na nina imani hata wanaolipia matangazo yao wanalipa kwa kujua hii blog siyo ya dini ama chama fulani ingawa ni ya mtu amabye alishaeleza msimamo wake kuwa hii Blog ni ya jamii.kwa hiyo lugha za kuwa kila mtu akiwa na mtizamo tofauti, unamuharibia michuzi na si vinginevyo. Michuzi naomba ukemee please.

    ReplyDelete
  14. kaka michuzi mbona hata haieleweki, kwani rais anahangaika nini? yeye anajua anapita lakini bado yuko busy kukampei, atulie. hakuna mpinzani wa maana. Tulia mama kikwete.

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...