Hi Michuzi,
Pole na shughuli za ujenzi wa Taifa. Ningependa kujua chanzo cha mdomo kunuka na tiba yake. Nafikiri tooth gel kama hazina msaada vile!
Pole na shughuli za ujenzi wa Taifa. Ningependa kujua chanzo cha mdomo kunuka na tiba yake. Nafikiri tooth gel kama hazina msaada vile!
Wadau msaada tutani pls.
Thanks Ankal,
Affected.
Thanks Ankal,
Affected.


Kunuka ni kutopiga Mswaki kwenye meno na ulimi wako na kama unaongea maneno machafu machafu kutoka mdomoni Mungu atakusaidia yasiwepo maneno hayo kama hakuna maneno machafu, Piga Mswaki Asubuhi na ukienda kulala na ukitokea kula mchana pia nunuwa MINT SPRAY .
ReplyDeleteng'ata kimba lako la kwanza la asubuhui, hiyo ndiyo tiba madhubuti.
ReplyDeleteUkiona hivyo ujue mwanamke wako amekutolea uvivu.
ReplyDeleteKaka piga mswaki asubuhi na jioni kabla ya kwenda kulala.Ikishindikana nenda kwa madaktari wa meno
Sio kutokupiga mswaki tu ndio kunasababisha kunuka mdomo. Unaweza ukawa unapiga mswaki kila siku na still ukanuka mdomo.
ReplyDelete- unaweza kuwa na magonjwa kwenye intestine ambayo hayajagunduliwa
- gum desease
- chakula unachokula
- kama unavuta sigara
-kama unakunywa pombe
-stress
-tonsil na sinus
kama wewewew unafany good hygene na bado mdomo unanuka jaribu kufuatilia hayo hapo juu moja baada ya moja kama haiishi mwone doctor.
uwe unasafisha meno usiku kabla ya kulala na asubuhi ukiamka kula kifungua kinywa then ndo usafishe meno usisahau kusafisha ulimi pia.
ReplyDeletehalafu pia costipation(kukosa haja kubwa)ni cause nyingine ya kunuka mdomo kunywa maji mengi,matunda,mbogamboga ili uweze kuongeza msukumo wa utumbo na hivyo kupata gogo kirahisi.
natumaini itakusaidia..
dental floss
ReplyDeletelol! anko makoye jamani mie sisemi
ReplyDeletewe mdau wa pili hapo juu umerukwa na akili period! hivi kweli wewe unaweza kuongoza familia yako ikiwa ndio bonge la nunda mh kazi ipo, pole sana unahitaji msaada
ReplyDeleteDawa yake ni kuvuta sigara hivyo harufu ya mdomo inabadilika kuwa ya tumbaku,
ReplyDeleteDozi itabidi ujipimie chain smoker au kama haunuki sana ubaweza kupata tata kutwa mara tatu
Sukutua na mkojo wa beberu. Kwisha kazi, hutanuka mdomo tena. Ukinuka njoo nikupe kitu!
ReplyDeleteTatizo la mdomo kutoa harufu mara nyingi inasababishwa na diet (vyakula unavyo kula)
ReplyDeleteJaribu kupiga mswaki mara 3 kwa siku na tumia Mouth wash! pia jaribu kumuona doctar wa memo akupe ushauri mzuri!!!
http://www.facebook.com/pages/edit/?id=144971678852174&sk=basic#!/pages/I-am-a-FAN-of-YOUNG-AFRICANS-SC/144971678852174
ReplyDeleteAchana na wahuni hawa: Chukua mdarasini kijiko kimoja cha chai na asali mbichi jiko kimoja tayarisha.
ReplyDelete1. chemsha mdarasini wako chemsha kwenye vikombe viwili vya maji.
2. vikishachemka epua, joto likipungua tia asali yako koroga. Kunywa kama chai mchanganyiko huo asubuhi na jioni wakati unaenda kulala. hiyo ni dozi ya siku moja yaani mchana na jioni. Fanya hivyo kila siku, then niandikie: rosalindajenes@yahoo.com
Mswaki muhimu, hata mara tatu kwa siku: Asubuhi, mchana na kabla hujalala usiku.
ReplyDeleteLakini vile vile unapoamka hata baada ya ya mswaki kunywa hata nusu kikombe na biskuti au andazi moja.Harufu mbaya mdomoni inatoka tumbo ambalo halijapata chochote- na si lazima ule sana au unywe sana- kikombe kidogo kimoja na andazi moja vinatosha kabisa kuzuia kuibuka harufu mbaya mdomoni.
ACHENI KUMDHIHAKI NA MITUSI YENU NYAU NYIE, NDUGU MWATHIRIKA NTACHEKI NA WATAALAM WA TIBA YA KIARABU NTAKUFAHAMISHA, OTHERWISE UNAWEZA KUWAONA MADAKTARI BIGWA WA MAGONJWA YA KINYWA NA PUA
ReplyDeleteMZEE WA BUNJU
JAMANI MAJIBU GANI HAYA??KAMA UWEZI KUMSAIDIA BASI ACHA KUTOA COMMENT....AYO SIO MAJIBU KABISA..NDUGU YANGU MIE SIJUI TIBA NINGEJUA NINGEKUPA JIBU..POLE
ReplyDeletepole mdau. mara nyingi inakuwaga ni matatizo ya fizi. kwa kuanzia, piga mswaki KWA UFASAHA kila ulapo, meno ya chini juu na zaidi ulimi.pia tumia sana vyakula vya vitamini. yupo rafiki yangu alikuwa na tatizo kama lako, akaenda kwa daktari wa kinywa muhimbili ametibiwa na mpaka sasa imekuwa historia. pole, usikate tamaa, linapona kabisa.
ReplyDeleteHakikisha unasugua ulimi vizuri baada ya kupiga mswaki meno, na pia sukutua koo na kuhakikisha halina makoozi.
ReplyDeleteKwa kuongezea sukutua mdodmo na koo na mouth wash baada ya kupiga mswaki.
Yote hayo yakishindikana basi muone daktari meno kwa ushauri zaidi.
we anonymous wa pili ni mshenzi!
ReplyDeleteMdau soma hapa http://en.wikipedia.org/wiki/Halitosis
Nafikiri ni vitu viwili tu:
ReplyDelete1) Safisha meno kila baada ya kula.
2) Safisha meno kila upitapo muda mrefu bila ya kutumia mdomo. Kutumia mdomo ni aidha Kula au Kusema, kuimba nk.
comments za hapo juu zinatia kichefuchefu....kama hauna msaada si unanyamaza? ukiona mtu kaleta mada kama hiyo ujue ana shida anataka msaada....au hili ni jukwaa la mizaha?
ReplyDeleteIt could have been a GOOD and GENUINE question, but asked at a WRONG TIME. We need to be sensitive on the effect of what we say or do in public on others; otherwise we may end up in problems!!One of the key aspects to happiness in this world is the ability to COEXIST.
ReplyDeleteJAMANI MBONA HATUNA UTU!!!MTU AMEOMBA USHAURI KAMA HUNA CHA KUMSHAURI SI UKAE KIMYAAA INA HAJA GANI KUANDIKA MAMBO YA KISHENZI HUMU.
ReplyDeleteKAKA/DADA YANGU USIJALI DAWA YA KUNUKA MDOMO NI KUSUGUA SANAAAAA ULIMI WAKATI WA KULALA NA ASUBUI PIA PENDA KUTUMIA MOUTH WASH YOYOTE ILE BAADA YA KUPIGA MSWAKI. KAMA IKIENDELEA MUONE DAKTARI MAANA ITAKUWA NI KIKWAPA CHA MDOMO. POLE SANA
jamani mwenzako anauliza wewe ndio unamjibu huo uozo. sio ustaarabu hata kidogo. toka lini kimba likaliwa????duh lakini anyway inawezekana ndio dawa. mdau ebu jaribu then utupashe matokeo. ila kumbuka liwe kimba la kwanza la asubuhi.hahahahahaaaaaa
ReplyDeletetuweke comments za kujenga jamani tusiwe kama watu hatuna akili.... kama huyu mjumbe saa 01: 49:00 AM, huna msaada kaa kimya.
ReplyDeletehehehehe uwiiiiii !!!
ReplyDeletejamani watu wa humu wana visa
sasa huo ndo ushauri mnampa angate kimba lake la asubuhi !!! hehehe
kaazi kweli kweli ..
jamani wataamu msaidieni au waliokutwa na matatizo kama haya ..
duh kweli kuna watu hata wakipiga mswaki domo lina nuka !!
ReplyDeleteAnkal,
ReplyDeletemaana ya kuwa moderator ni kwamba si lazima kila comment inayotumwa ionekane kwenye blog yako. Upuuzi mwingine unauchuja na kuuacha. Swali la msingi mtu ameuliza kwa maana nzuri pengine mahusiano na girl friend au mke si mazuri kwa ajili ya harufu.. sasa unawezaje kuruhusu comment za ki puuzi! Hi blog yako ni ya mfano ankal si kila mpuuzi anaweza akaweka comment yake humu!!
Nenda kwa dentist ukasafishe kinywa kuna mashine specific kwa ajili hiyo.Mswaki peke yake hautoshi manake inatakiwa deep cleaning inawezekana kabisa una infections na bacteria ndio wanaoleta bad breath(halitosis).Ni muhimu kufanya regular check up and cleaning kwa dentist maana inawezekana kukawa na sababu tofauti zinazopelekea hali hiyo inayoabisha.
ReplyDeletewaone dentists au pia mitishamba huwa inasaidia.
ReplyDeletevilevile harufu inaweza ikawa inatokea tumboni hivyo angalia hilo na wataalam
May be sio tatizo lako ila huu upuuzi tuliokua nao watanzania wengi kupenda kuchekesha kuliko kujenga ndo unapelekea comment hizi za kipuuzi...watanzania bado tunalala..waloenda nje kidogo wana upeo atleast wa kuona ni kiasi gani wenzetu wanajitahidi kuimprove...just imagine..ukisha chekesha unapata nn..wadau (thu aug 26 01:16:oo na 01:49:00) try to improve shame on you.
ReplyDeleteHahaha Hizi Coment Nyingine Jamani! Mi Natarajia kila mtu anaeingia kucoment hapa ni Mtu mzima Sasa Hawa wengine utadhani wamekurupuliwa usingizi jamni ah ah this is not fair!! Ok achana na huyo zinamtosha mwenyewe!! Nakushauri wasiliana na Dr Ndodi Aliwahi kuelezea saana Swala la kunuka mdomo kuoza meno na mwengine mengi yanayohusiana na vinywa! Pole saana mwana Jamii mwenyetu!! Ila tu kwa "Knoledge" yangu ndogo Ni kwamba unapawswa ukipiga mswaki usugue pie na ulimi wako mpka maeneo karibia na Koo
ReplyDeletekunuka mdomo kunaweza pia kusababishwa na tatizo la tumbo au fizi na wala sio mdomo peke yake au meno kama tunavyofikiri. Kuna baadhi ya matatizo ya tumbo ukiwa nayo mdomo hauishi kunuka. Fuatilia zaidi suala hilo
ReplyDeleteKamuone daktari wa kinywa na meno,pengine huko na vijidonda mdomoni,au unatumia mswaki umekwisha makali yake,au wakati unasugua meno kwa kawaida huwa unafanya haraka unatumia muda mchache.
ReplyDeleteInawezekana pia meno yako yameeacha nafasi baina ya jino na jino hivyo vyakula kujificha humo na mswaki haufiki.
Piga mswaki kila siku asubuhi na kabla ya kulala.
Angalia vyakula unavyokula pia,na inawezekana pia tumbo lako ni chafu.
Badilisha mswaki kila baada ya mwezi moja,
ikiwezekana pia badili na dawa unazotumia mara kwa mara.
Sukutua mdomo kwa mouthwash zipo bei nzuri tu siku hizi.
Pole sana yaliwahi nikuta hayo wala sikung`ata kimba la asubuhi.
Muone daktari kwa ushauri zaidi
Nenda kwa dentist kusafisha meno; halafu baada ya hapo hakikisha unapiga mswaki asubuhi na usiku kabla ya kulala.
ReplyDeleteNenda kwa dentist akufanyie tooth cleaning na kuondoa hizo calcium deposits. Halafu piga msawaki asubuhi na jioni kabla ya kulala. Halafu acheni kula vyakula vya kihindi!
ReplyDeleteJaribu kutembelea kwenye masuper market makubwa kama mlimani,na jaribu kutafuta dawa za kusukutua mdomo. utakuta zingine wanandika masaa 24, mdomo uko swafi ahutoi harufu. kama upo. Dar pale mlimani, kwenye maduka kuna duka mmja linauza,kama umeshawai kuona chupa imeandikwa listern, sikosei
ReplyDeleteMdau ushauri wangu ni kuwa ungejaribu kutumia dawa za miti shamba nyingi zinasaidia kama si mpenzi wa mizizi ology basi ungejaribu kila siku kabla ya kulala ungesugua meno kwa mavi ya kuku.
ReplyDeletekwa dentist kukwangua meno, halafu piga mswaki na kuflosi (kama huna floss unaweza kutumia nyuzi za guzia za salfeti)
ReplyDeleteHalafu tafuna gum aina ya eclipse na mfano wake (zisizo na sukari halisi).
Yeah km unapiga mswaki ipasavyo na bado kuna harufu, kuna magonjwa mengine ktk utumbo mpana, mdogo na hata tumbo, ambayo pia husababisha harufu. Mfano wa magonjwa hayo ni Ulcerative Colitis, Chrohs disease, Inflamatory bowel disease, etc.
ReplyDeletechukua karafuu kavu moja na umumunye angalau mara 3 kwa siku, itasaidia
ReplyDeleteKama alivyosema mchangiaji wa 08:29 AM, tatizo linaweza kuwa tumboni. (muone daktari bingwa 'gastro-enterologists') Hata hivyo sukutua maji ya chumvi mara tatu kwa siku na kunywa maji ya moto kiasi kitu cha kwanza asubuhi.
ReplyDeleteMwathirika wa tatizo hili pole sana. Wadau, kuweni makini na mnachomshauri mwenzenu, kama hamna maoni ya maana Nyamazani! Dia, hilo tatizo wakati mwingine linatokea tumboni, yaani kutokula kwa wakati au kutoongea muda mrefu, jitahidi kutafuna tafuna, pia kula kitunguu saum 1x3 naamini vitasaidia. Ikishindikana kamuone mtaalamu wa kinywa. Pole sana. Rebby.
ReplyDeletemama fide wa ukonga we ni hatari kweli nimecheka sana ati, sukutua na mkojo wa beberu loh ha ha haaa!!
ReplyDelete