Jarida jipya la Kiswahili la uchambuzi wa habari za siasa, uchumi, utamaduni, michezo na burudani lenye hadhi inayolingana na majarida ya kimataifa yanayosifika ulimwenguni mfano wa Newsweek , Time, New African na The Economist lijulikanalo kama UMOJA limeingia katika soko kwa kishindo likiwa na habari-makala nzito.

Jarida hilo lililoandaliwa na timu ya wanahabari wachambuzi linapatikana nchi nzima likiwa na dodoso kuhusu mustakabali wa Taifa kama zile zinazohusu siasa za Zanzibar hususani kilichopo nyuma ya pazia katika uteuzi wa Dk. Ali Mohamed Shein kuwa mgombea urais wa CCM Visiwani.

Kama hiyo haitoshi UMOJA limefanya mahojiano mazito ya ana kwa ana na watu mashuhuri nchini, kama vile Zitto Kabwe, January Makamba, Tausi Likokola, na Lillian Mduda.

Jarida hilo pia lina wasifu wa mwanadiplomasia aliyetukuka nchini, Dk. Asha-Rose Migiro likiwa pia na makala nyingine nzito za kitaifa na kimataifa ikiwamo moja ya michezo inayogusa safari ya ukocha nchini ya Kocha Mbrazili Marcio Maximo aliyemaliza mkataba wake hivi karibuni.

Waandishi wenye majina nchini wakiongozwa na Mwenyekiti wa Jukwaa la Wahariri Tanzania, Absalom Kibanda, Ratifa Baranyikwa, Charles Mullinda, Alloyce Komba na wengine wengi wamejumuika ili kuwaandalia wakazi wa nchi za Afrika Mashariki wanaozungumza Kiswahili bidhaa ambayo haijapata kuwapo kabla hapa nchini.


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 1 mpaka sasa

  1. na siye kwa kuiga..hawakuweza kuja na lao creative thinking tz iko wapi

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...