Katika Kijiji cha Halukumbi Tarafa ya Katunguru kata Chifunfu wilayani Sengerema wanafunzi 18 kati ya 37 waliokuwa wakisafiri ziwani Victoria kwa Mtumbwi kwenda shule leo asubuhi majira ya saa 1:45 walizama na kufa maji. Mpaka sasa miili 12 ya watoto hao waliokufa imekwsiha patikana huku mingine 6 ikiendelea kutafutwa ndani ya ziwa Victoria.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

Kuna Maoni 8 mpaka sasa

  1. jamani,jamani nyie viongozi wa tanzania mnaokula mapesa wenzenu waliotoa kodi wanakufa kesho kwa Muumba mtasema nini,mpaka leo nchi ina uhuru miaka zaidi ya 40 katika karne ya 21 ya sayansi na teknologia na ari mpya kasi mpya bado matumia mitumbwi kama usafiri wa kud=safirishia watu...tukisema mnasema watu wa nje wanalonga sana ila kama hali ni hii wacha niendelee kupiga box tu...Mungu awalaze marehemu mahali pema peponi...na nyinyi viongozi siku yenu inakuja hamuwezi kuendelea hivi milele,remember you can fool some people for some time but you can't fool all people all the times...na wewe michuzi ibanie hii kwa kuwa umezoea kubana wakati tunakosoa wapumbavu fulani fulani.

    ReplyDelete
  2. Wapumzike kwa amani...Inasikitisha...Huku viongozi wana mwaga pesa kugombea watoto wanakosa hata maboya ya kusafiria ziwani...

    ReplyDelete
  3. serikali haiwezi kukwepa lawama hii ni nini kinafanyika wakati ni wiki chache tu zimepita toka watu 9 wafe kule rufiji ktk tukio km hilo??? hii haiwezekani sumatra mkowap, mmekabidhiwa kuangalia eneo hili linakwendaje ikiwa ni pamoja na kuangalia mambo ya usalama,mnafika maeneo husika au mnaishia hapo dzm tu? jitihada zifanyike tusiendelee kupoteza mawaziri na wabunge wajao wajameni?? inasikitihsa sn.
    mungu awalaze mahali pema amen....

    ReplyDelete
  4. terrible, poleni wazazi, ndugu na jamaa.
    Wajualo ni kukusanya ela za uchaguzi mengine wanafumbia macho sio kama hawaoni

    ReplyDelete
  5. poleni wazazi Mungu awatie nguvu katika kipindi hiki kigumu

    nyie viongozi jamani acheni kula hela za kodi na kusahau watu kiasi hiki

    ReplyDelete
  6. Afu wenyeji tuking'ang'ania kuishi kwenye nchi za watu wanasema turudi home tulijenge taifa, taifa lenyewe ndo hilo halina hata boti ya kubebea watu, lol! inasikitisha sana. swali bro Michuzi hivi hii serikali inasoma malalamiko yetu through this blog au tunalia tuu bure..

    ReplyDelete
  7. kwa kweli natumaini kwa sasa hawa sumatra wanatakiwa wabinafsishwe, unajua hakuna kitu kibaya kama utakuwa huna mbinu mpya ya kuweza kudhibiti matukio hasa ambayo yanawezekana kutatuliwa, leo hii kuna magari ambayo hayana mikanda lakini kwa kuwa ni ya fisadi fulani ambaye yupo serikalini basi hakuna wa kumfanya lolote.
    wizi na ubadhirifu wa rasilimali zetu ndio chanzo cha matatizo yote haya, viongozi wao wapo kwa ajili ya kuiba tu na sio kuangalia usalama wetu.
    poleni wafiwa na mungu yupo nanyi

    ReplyDelete
  8. Poleni wafiwa

    Roho za marehemu zipate rehema kwa Mungu na zipumnzike kwa amani. Amina

    Hivi we unaesema hutaki kurudi nyumbani kwakuwa hakuna maboya kweli umemaanisha au?

    Tusiwe wabinafsi tuwe na upendo kwani siajabub wewe ukirudi nyumbani ndo utakuwa mwenyekiti mzuri wa kijiji

    ReplyDelete

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...